Wamiliki wa Frem za Biashara

Wamiliki wa Frem za Biashara

Tman900

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2017
Posts
969
Reaction score
3,067
Sisi ambao Tunatafuta Ridhiki kupitia Biashara, Vidogo Vidogo.

Mara Nyingi kupandishiwa Kodi mara kwa Mara, Ukilipia Kodi ya mwaka, au miezi 6 Tegemea mda wowote kukutana Bonge la waraka wa kupandishiwa Kodi.

Wengine wanakupandishia Kodi Ili ushindwe uhame akiona unakomaa zaidi anazidi kupandisha Kila mara, ukifunga Biashara na Kuhama, mwenye Nyumba anafungua Biashara ambayo wewe ulikua unafanya ktk eneo hilo...

Daaa Wabongo Tabia Zetu jau sana
Wanaishia kuchemka ktk Biashara
 
Kuna mama mmoja wa kichaga kamfanyia mpemba ujinga huo kilichomkuta sehemu hyo baada ya mpemba kuiachia baada ya figisu nyingi Ili huyo mama aendeleze mpemba alichokuwa anafanyaa ,yule mama alifanya wiki tu baada ya hapo paka Leo pameoteana majani😄😄😄

Wapembaa shikamooniii🙌🙌🙌
 
Kuna mtu kaanza kuniletea huo Ujinga toka mwaka Jana, naona visa vinazidii.
 
Miaka kadhaa nyuma nilikuwa na jamaa yangu ambae alikuwa anafanya kazi kwa wa pakistan waliokuwa wanauza spices (viungo vya vyakula) kwa jumla.

Kulitokea tatizo baina ya hao wa pakistan ikabidi wafungashe virago vyao ghafla na kusepa.
Inasadikika ilikuwa wauza ngada na hizo spices ilikuwa geresha.

Ilikuwa wameingiza mzigo wa kutosha wa biashara kabla ya kuondoka. Na jamaa yangu ndio alikuwa mtu wao wa karibu kibiashara hivyo wakaishia kumuachia kila kitu.

Jamaa akaamua kufungua duka kabisa ili auze mzigo maana wa pakistani walikuwa wanauza kutoka godauni kwa order.

Kwa vile jamaa alikuwa na mzigo wa dezo alikuwa anauza spice bei rahisi mno kiasi kwamba duka lilikuwa linafurika wateja kila muda.

Mwenye frame akaanza kupatwa na wivu na kuanza kupandisha bei ya kodi kila baada ya miezi 3. Jamaa alipoona mzigo unaelekea kuisha na kodi inapandishwa akarudisha frame.

Mwenye frame akaanzisha yeye biashara ile ile. Na alivyo juha akaunganisha frame 2 na kujaza mzigo.
Tatizo likaja kwenye bei. Hakuweza kuweka bei za chini maana mzigo ulimgharimu sana kuagizia. Mwisho wa siku akamfuata jamaa yangu na kutaka kumpunguzia kodi tena na amuuzie mzigo wake uliobaki.

Jamaa alishaachana na hiyo biashara hivyo akakataa. Mwisho wa siku mwenye frame akafunga duka na kupangisha tena ma frame yake na mzigo mwingine uliishia ku expire.
 
Back
Top Bottom