Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,243
- 44,520
CCM ni sawa mwembe ambao hurushiwa mawe kutokana na matunda yake - mama salma kikwete
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete (katikati) akiwanadi wagombea Ubunge wa jimbo la Lilundi,Bw. Jarome Bwanausi na wa jimbo la Masasi, Bi.Maryam Kasembe mkoani Mtwara juzi.
Baadhi ya wagombea Udiwani wa Jimbo la Masasi,Mtwara wakinadiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete katika mkutano uliofanyika juzi jimboni humo.
(Kutoka kwa Michuzi Blog)
My Take:
Ninaelewa Ridhiwani anapofanya kampeni anafanya kama kiongozi wa Jumuiya ya Vijana wa CCM (japo kimsingi anampigia kampeni babake kwani wapo viongozi wengine wa vijana ambao wana nafasi ya juu kuliko yeye na hawapati nafasi na ujiko kama wa wake). Sina tatizo sana na Ridhiwani kufanya hivyo.
Lakini mama Salma naye ni kiongozi ndani ya CCM nadhani ni mjumbe wa CCM wa nafasi fulani sikumbuki! Lakini katika hizi kampeni kila anakoenda anatambulishwa kama kiongozi wa Taasisi ya wa Kina Mama (WAMA). Nina maswali:
a. Taasisi hii ni kitengo cha Ikulu (Ofisi ya First Lady)?
b. Taasisi ni NGO iliyoanzishwa kwa sheria ya NGOs? Kama ndiyo je NGOs nyingine zina haki ya viongozi wake kumpigia mgombea wanayemtaka au chama wanachotaka kampeni? Sema kwa mfano TASWA au LEAT wanaweza kuanza kupiga kampeni waziwazi za chama au mgombea wanayemtaka?
c. Gharama za mama Salma zinalipwa na CCM (kama Kinana alivyotaka tuamini) au zinalipwa na WAMA au na Serikali?
d. Kama mama Salma anafanya hivyo kama kiongozi wa CCM kwanini wanatumia ujiko wa WAMA?
e. Yumkini WAMA ni chombo kimojawapo cha CCM?
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete (katikati) akiwanadi wagombea Ubunge wa jimbo la Lilundi,Bw. Jarome Bwanausi na wa jimbo la Masasi, Bi.Maryam Kasembe mkoani Mtwara juzi.
Baadhi ya wagombea Udiwani wa Jimbo la Masasi,Mtwara wakinadiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete katika mkutano uliofanyika juzi jimboni humo.
(Kutoka kwa Michuzi Blog)
My Take:
Ninaelewa Ridhiwani anapofanya kampeni anafanya kama kiongozi wa Jumuiya ya Vijana wa CCM (japo kimsingi anampigia kampeni babake kwani wapo viongozi wengine wa vijana ambao wana nafasi ya juu kuliko yeye na hawapati nafasi na ujiko kama wa wake). Sina tatizo sana na Ridhiwani kufanya hivyo.
Lakini mama Salma naye ni kiongozi ndani ya CCM nadhani ni mjumbe wa CCM wa nafasi fulani sikumbuki! Lakini katika hizi kampeni kila anakoenda anatambulishwa kama kiongozi wa Taasisi ya wa Kina Mama (WAMA). Nina maswali:
a. Taasisi hii ni kitengo cha Ikulu (Ofisi ya First Lady)?
b. Taasisi ni NGO iliyoanzishwa kwa sheria ya NGOs? Kama ndiyo je NGOs nyingine zina haki ya viongozi wake kumpigia mgombea wanayemtaka au chama wanachotaka kampeni? Sema kwa mfano TASWA au LEAT wanaweza kuanza kupiga kampeni waziwazi za chama au mgombea wanayemtaka?
c. Gharama za mama Salma zinalipwa na CCM (kama Kinana alivyotaka tuamini) au zinalipwa na WAMA au na Serikali?
d. Kama mama Salma anafanya hivyo kama kiongozi wa CCM kwanini wanatumia ujiko wa WAMA?
e. Yumkini WAMA ni chombo kimojawapo cha CCM?
