Ndugu zangu wa jf, pole sana kwa majukumu mengi ya kujenga Taifa letu, bila kupoteza muda napenda kupata maoni yenu juu ya hoja ambazo miezi michache tu iliyopita zilikuwa zikisikika sana na hasa wale waliikuwa waongeaji sana juu ya kauli hizo walikuwa vigogo wa chama tawala, kati ya watu niliowasikia kwa masikio yangu mwenyewe ni pamoja na Mh Stephen Wassira, Mh Mwigulu Lameck Nchema na Mh Willium Lukuvi.
Nilikuwa najiuliza maswali mengi sana juu ya kauli hizi, na hasa nilitaka kujua chadema inaweza kufa ni sawa lakini
1. Itakufa kwa namna gani
2. Kwanini wanaotabiri kifo hicho wote watoke chama tawala?
3. Ikifa kwa kifo hicho wanachotuambia ni nini faida yake kwa Taifa letu?.
Hayo ni baadhi ya maswali niliyojiuliza.
Sasa ningependa kujua kwa yeyote mwenye ufahamu anijuvye tafadhali, hivi haya yanayotokea ya Mh Zitto ndiyo matokeo ya unabii wa akina Nchemba au tusubiri mengine?
Tafadhali kama unajua lolote unijulishe.
Nilikuwa najiuliza maswali mengi sana juu ya kauli hizi, na hasa nilitaka kujua chadema inaweza kufa ni sawa lakini
1. Itakufa kwa namna gani
2. Kwanini wanaotabiri kifo hicho wote watoke chama tawala?
3. Ikifa kwa kifo hicho wanachotuambia ni nini faida yake kwa Taifa letu?.
Hayo ni baadhi ya maswali niliyojiuliza.
Sasa ningependa kujua kwa yeyote mwenye ufahamu anijuvye tafadhali, hivi haya yanayotokea ya Mh Zitto ndiyo matokeo ya unabii wa akina Nchemba au tusubiri mengine?
Tafadhali kama unajua lolote unijulishe.