Katika tukio lingine la hivi karibuni lenye kudhihirisha kasi ya CCM kuibomoa CHADEMA, Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Tarime, kimevuna wanachama wapya 800 ambao awali walikuwa ni wanachama na wafuasi wa CHADEMA.
Wanachama hao ambao idadi yao imetimia takriban 800 wamekuwa wakiingia CCM kwa muda wa wiki tatu mfululizo tangu kumalizika kwa ziara ya Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA katika wilaya ya Tarime, ambapo wanachama zaidi ya 600 walijiunga wiki mbili zilizopita na 256 walijiunga na CCM jumanne iliyopita katika mikutano ya hadhara.
Mikutano hiyo ya hadhara ambayo inaendelea wilayani humo, jumanne ya juzi ilifanyika katika uwanja wa kituo cha Sirari, ukihutubiwa na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Rashid Bogomba, ulihudhuriwa na mamia ya wakazi wa eneo hilo na katika mkutano huo ndipo wanachama wengine 256 waliporudisha kadi za chadema na kujiunga na CCM na kutimiza idadi ya wanachama hao wapya kutoka chadema kutimia zaidi ya 800.
Wanachama hao wamedaiwa kuhamia CCM baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa , Freeman Mbowe kuwasimamisha uongozi viongozi wa CHADEMA wa wilaya hiyo ya tarime, ambao waliamua kuhamia CCM wakifuatwa na wafuasi wao kutoka katika chama hicho.
Source: Uhuru_ukurasa wa 8
Wanachama hao ambao idadi yao imetimia takriban 800 wamekuwa wakiingia CCM kwa muda wa wiki tatu mfululizo tangu kumalizika kwa ziara ya Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA katika wilaya ya Tarime, ambapo wanachama zaidi ya 600 walijiunga wiki mbili zilizopita na 256 walijiunga na CCM jumanne iliyopita katika mikutano ya hadhara.
Mikutano hiyo ya hadhara ambayo inaendelea wilayani humo, jumanne ya juzi ilifanyika katika uwanja wa kituo cha Sirari, ukihutubiwa na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Rashid Bogomba, ulihudhuriwa na mamia ya wakazi wa eneo hilo na katika mkutano huo ndipo wanachama wengine 256 waliporudisha kadi za chadema na kujiunga na CCM na kutimiza idadi ya wanachama hao wapya kutoka chadema kutimia zaidi ya 800.
Wanachama hao wamedaiwa kuhamia CCM baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa , Freeman Mbowe kuwasimamisha uongozi viongozi wa CHADEMA wa wilaya hiyo ya tarime, ambao waliamua kuhamia CCM wakifuatwa na wafuasi wao kutoka katika chama hicho.
Source: Uhuru_ukurasa wa 8