Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,557
- 21,515
Imeelezwa kuwa wanawake waliokeketwa wanapojamiiana na mwathirika wa virusi vya UKIMWI (VVU) huwa katika hatari ya kupata maambukizi kwa asilimia 99 kuliko ambao hawajakeketwa.
Meneja wa Mradi wa Tokomeza Ukeketaji Serengeti unaotekelezwa na Shirika la Amref Health Africa Tanzania, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), halmashauri na wadau wengine kwa ufadhili wa UN Women, Godfrey Matumu alisema vitendo vya ukeketaji ni ukatili wa kijinsia.
Akizungumza mbele ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kisangura katika kampeni ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia, Matumu alisema kwamba ukeketaji una athari kubwa kiafya na kisaikolojia kwa watoto wa kike wanaotendewa kwa misingi ya kutimiza hitaji la mila.
“Idadi kubwa sana hufanyiwa ukatili wa kijinsia, utafiti unabainisha kuwa mwanamke aliyekeketwa anapojamiiana na mwathirika wa virusi vya UKIMWI ana asilimia 99 ya kupata maambuzi tofauti na ambaye hajakeketwa,” alisema.
Matumu aliwataka wanafunzi kuwa na ujasiri wa kukataa vitendo vya ukeketaji kwa kuwa ni chanzo cha ndoa na mimba za utotoni zinazokatisha ndoto zao.
Mwanafunzi wa kidato cha tatu, Neema Mahiri alisema kwamba watoto wengi wa kike wanakubali kukeketwa kwa kuwa hawaambiwi madhara yake.
Ofisa Ustawi wa Jamii, Maria Mchala alisema kwamba wanapokea migogoro mingi ya ndoa za utotoni ikiwamo ya wazazi kuwaoza watoto kwa wazee kwa ajili ya kupata mali.
“Ofisa vijana wa wilaya, Isaack Mwakyusye alisema kata ya Kisangura ni miongoni mwa maeneo yanayoongoza kwa ukatili wa kijinsia.
Mwananchi
Meneja wa Mradi wa Tokomeza Ukeketaji Serengeti unaotekelezwa na Shirika la Amref Health Africa Tanzania, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), halmashauri na wadau wengine kwa ufadhili wa UN Women, Godfrey Matumu alisema vitendo vya ukeketaji ni ukatili wa kijinsia.
Akizungumza mbele ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kisangura katika kampeni ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia, Matumu alisema kwamba ukeketaji una athari kubwa kiafya na kisaikolojia kwa watoto wa kike wanaotendewa kwa misingi ya kutimiza hitaji la mila.
“Idadi kubwa sana hufanyiwa ukatili wa kijinsia, utafiti unabainisha kuwa mwanamke aliyekeketwa anapojamiiana na mwathirika wa virusi vya UKIMWI ana asilimia 99 ya kupata maambuzi tofauti na ambaye hajakeketwa,” alisema.
Matumu aliwataka wanafunzi kuwa na ujasiri wa kukataa vitendo vya ukeketaji kwa kuwa ni chanzo cha ndoa na mimba za utotoni zinazokatisha ndoto zao.
Mwanafunzi wa kidato cha tatu, Neema Mahiri alisema kwamba watoto wengi wa kike wanakubali kukeketwa kwa kuwa hawaambiwi madhara yake.
Ofisa Ustawi wa Jamii, Maria Mchala alisema kwamba wanapokea migogoro mingi ya ndoa za utotoni ikiwamo ya wazazi kuwaoza watoto kwa wazee kwa ajili ya kupata mali.
“Ofisa vijana wa wilaya, Isaack Mwakyusye alisema kata ya Kisangura ni miongoni mwa maeneo yanayoongoza kwa ukatili wa kijinsia.
Mwananchi