Walimu wana maisha magumu sana

Walimu wana maisha magumu sana

Cherecheche

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2024
Posts
4,819
Reaction score
9,258
Wakati nasoma niliona haya kwa walimu yanayohuzunisha.
1. Kushindia mihogo ya 500 na mapera kuanzia asubuhi hadi jioni ili
kubana matumizi.
2. Kuvaa nguo zilezile kila siku hadi zinapauka.

3.Madeni mtaani na benki.
4.Kuvizia chakula cha wanafunzi wa bweni ili siku ipite.
5.Kuwa wachafu nywele walikuwa hawachani,soksi zimetoboka, viatu vimetoboka, nguo zenye viraka lukuki.

NB: Serikali iwahurumie walimu kwa kuwaongezea mshahara kazi wanayofanya ni kubwa.
 
Kuna mwalimu wangu alikuwa anasema "wao ni watu wa muhimu sana maana wao hutengeneza madaktari wanasheria na wengineo katika jamii"

Ila product yao inakula mshahara mnono ilhali wao ni shida shidani
 
Ni kweli wana maisha magumu lakini mada imekaa kimbeambea na uongo uongo, sijawahi kuona mwalimu akivaa nguo yenye kiraka, majobless mtaani wenyewe nguo zao hazina viraka vipi iwe kwa mwalimu?

Kuchana nywele inahusiana nini na umaskini? Kama hachani nywele huyo ni mchafu na haihusiani na umaskini
 
Sema baadhi ya walimu wasio na nidhamu kwenye mipango ya matumizi ya pesa ndio wenye hilo tatizo

Wako walimu kibao wana.magari binafsi na majumba hadi ya kupangisha na biashara na watoto wao husomesha English medium

Heshima kwenye matumizi ya fedha ndio kigezo kikuu kinachotofautisha hali walimu
 
Sema baadhi ya walimu wasio na nidhamu kwenye mipango ya matumizi ya pesa ndio wenye hilo tatizo

Wako walimu kibao wana.magari binafsi na majumba hadi ya kupangisha na biashara na watoto wao husomesha English medium

Heshima kwenye matumizi ya fedha ndio kigezo kikuu kinachotofautisha hali walimu
Unajua vyema kipato chao?
 
Sema baadhi ya walimu wasio na nidhamu kwenye mipango ya matumizi ya pesa ndio wenye hilo tatizo

Wako walimu kibao wana.magari binafsi na majumba hadi ya kupangisha na biashara na watoto wao husomesha English medium

Heshima kwenye matumizi ya fedha ndio kigezo kikuu kinachotofautisha hali walimu
Nakazia.
 
Ni walimu wa shule gani na mkoa gani hao hawajielewi?

Mimi hapa namiliki trekta lakununua cash.
Namiliki bajaji na nina miliki ng'ombe na mbuzi pia wengi tu.
Nimelima zaidi ya ekar 40 za ufuta na alizeti.

Usiwachafue walimu wanapiga kazi mbali mbali za kiuchumi na pia ndo wamekutoa tongotongo
 
Sema baadhi ya walimu wasio na nidhamu kwenye mipango ya matumizi ya pesa ndio wenye hilo tatizo

Wako walimu kibao wana.magari binafsi na majumba hadi ya kupangisha na biashara na watoto wao husomesha English medium

Heshima kwenye matumizi ya fedha ndio kigezo kikuu kinachotofautisha hali walimu
Ni kweli mkuu, kuna mwalimu jirani yangu anabeti mpaka laki tatu, kukicha anakuja kukukopa elfu kumi ya mboga nyumbani .
 
Back
Top Bottom