Walimu tunarudi kazini lakini.........

Kitaeleweka

JF-Expert Member
Jul 30, 2012
394
88
Kama rais alikua na hukumu ya kesi tangu jana ina maana yy yuko juu ya sheria coz yale yaliyoamuliwa leo jana alishasema mf kurudi kazini na kufidia muda uliopotezwa, notisi kucheleweshwa nk hivi anategemea walimu wawe na moyo wa kufundisha kweli? Mwalimu na mwanajukwaa unategemea nini kama reaction ya hukumu hii?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Kama rais alikua na hukumu ya kesi tangu jana ina maana yy yuko juu ya sheria coz yale yaliyoamuliwa leo jana alishasema mf kurudi kazini na kufidia muda uliopotezwa, notisi kucheleweshwa nk hivi anategemea walimu wawe na moyo wa kufundisha kweli? Mwalimu na mwanajukwaa unategemea nini kama reaction ya hukumu hii?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

kama kuna wakati serikali yetu imelikoroga basi ni sasa, na kama hawaamini basi wasubiri, watoto hawatafundishwa, lakini ubaya wa serikali unatakiwa kusambazwa popote Tanzania ili iwe rahisi kuiondoa serikali dhalimu isiyojali watu wake. Tuungane kama tulivyoungana ili kieleweke.
 
Hilo ndo haswa la kufundisha mashuleni ni kutapakaza sumu ya udhlimu wa serikali sio walimu wa arts wala scn hapa hata topic za hesabu zitakua na siasa ndani yake. Solodarity forever mpaka hii nchi serikali mbovu itoke.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Hata hiyo nguvu ya kufundisha stil sijajua naitoa wapi'hapa nilipo ninafull mawenge'kweli nimeamini mahakimu wa Tz wanapelekwa ka Ming'ombe....'
 
Ndio maana sitaki kufanya kazi serikalini full ujinga ujinga kama vp walimu sepeni tu ajira private xul zipo nyingi achaneni na kubwa jinga!
 
Ndio maana sitaki kufanya kazi serikalini full ujinga ujinga kama vp walimu sepeni tu ajira private xul zipo nyingi achaneni na kubwa jinga!

Sema wana UD hawaja ajiriwa wa kutosha. Endapo katika CWT wengi wanaenda kukiongoza chama ni Madiplo holder. Mfumo mzima utabadilika na nchi itaelewa tu. Wewe tulia huko private. Wadau tutakomaa tu.
 
YAANI Sa hivi wataisoma namba! Nikiingia vipindi double class nafundisha dk 15 tu hizo nyingine napiga porojo na ole wake mwanafunzi aniulize swali! Atajuta. Ila navionea huruma vianafunzi vyangu vya form maana tulipoishia ndo hapo hapo siendelei wala nini, na notice siwapi watafelije? Ila itakuwa funzo kwa wazazi wao siku nyingine wavote wisely, sio wana chagua viongozi wasio wathamini. MUHIMU WALIMU KWA NAMNA YEYOTE ILE TUJITAHIDI KUWASAIDIA WATOTO WA WALIMU WENZETU NA TUJARIBU KUWAIDENTIFY MASHULENI ILI TUWASAIDIE KIELIMU!
 
nikweli serikali imelikoroga! ila labda kizazi cha uwalimu wa wazazi wetu kife kama bado kipo, basi naamini dhahiri kuwa wao watawasaidia ndugu zetu wa kayumba kwa dhati kama walivyokuwa wakifanya mana wl wamezarauliwa hata zaidi ya hapa! ila kama kipo kizazi cha vijana wenzangu wa sasa wenyechangamoto mbalimbali na kutaka mabadilko basi ni dhahiri elimu ya ndugu zetu wa kayumba imekwisha! na watoto wa kupanda school bus ndo watakaokuja kukalia nafasi mbalimbali serikalini na kwenye private! hata kama ni wito lakini sio huu, hata huo wito kuna kuukuali na kuukataa! tz govt go to hell
 
YAANI Sa hivi wataisoma namba! Nikiingia vipindi double class nafundisha dk 15 tu hizo nyingine napiga porojo na ole wake mwanafunzi aniulize swali! Atajuta. Ila navionea huruma vianafunzi vyangu vya form maana tulipoishia ndo hapo hapo siendelei wala nini, na notice siwapi watafelije? Ila itakuwa funzo kwa wazazi wao siku nyingine wavote wisely, sio wana chagua viongozi wasio wathamini. MUHIMU WALIMU KWA NAMNA YEYOTE ILE TUJITAHIDI KUWASAIDIA WATOTO WA WALIMU WENZETU NA TUJARIBU KUWAIDENTIFY MASHULENI ILI TUWASAIDIE KIELIMU!

wewe sio mwalimu bali ni MCHONGANISHI kweli! kama ni hivi, sasa tz ifikie wakati kila profession iamue unachokiamua wewe kulinda watoto! hatutafika mana tutabaki palepale tunanyanyasana wenyewe tu but govt wao wanapeta! mfano madokta nao wakaamua kuwa wanatibia vzr watoto wao wawenzao wanawatibia ovyo ili wafe au kupata vilema, na watu washughuli nyingine pia wamue kutokana na shughului zao kama dereva, nk.! wewe kama kweli prof yako ni mwalimu sidhani kama huu ni uwamuzi sahihi!
 
Mtajuuuuuta kumfahamu kikwete na ccm. Na bado miaka 3. Pigeni keleleeeee yeye hana habari mshahara wake wa maana anapata posho za kufa mtu na watoto wake wanavitega uchumi km ilivyokuwa kwa watoto wa ghadafi.
 
waalimu mbona mmegoma toka 2005....sema mlikuwa hamjadhihirisha tu.....we mtoto wa dalasa la saba hajui kuandiks jina lake...kama sio mgomo ni nini:??...mmeacha kufundisha toka zamani taarifa tunazo....
 
Serikali kukimbilia mahakamani si suluhisho la mgomo unaoendelea. Hata wakiubana uongozi wa CWT na kuusulubu kwa kadri wanavyoweza, bado haitoshi kuondoa dhana ambayo tayari imejengeka ndani ya walimu ambao ndio wadau wakubwa na si CWT. Ushauri, Serikali iongeze kiwango kinachoombwa na wadau hao na ikumbukwe kuwa vita ya panzi haiamuliwi kwa bunduki.
 
wewe sio mwalimu bali ni MCHONGANISHI kweli! kama ni hivi, sasa tz ifikie wakati kila profession iamue unachokiamua wewe kulinda watoto! hatutafika mana tutabaki palepale tunanyanyasana wenyewe tu but govt wao wanapeta! mfano madokta nao wakaamua kuwa wanatibia vzr watoto wao wawenzao wanawatibia ovyo ili wafe au kupata vilema, na watu washughuli nyingine pia wamue kutokana na shughului zao kama dereva, nk.! wewe kama kweli prof yako ni mwalimu sidhani kama huu ni uwamuzi sahihi!

Mimi ni professional teacher Dip Monduli TTC Geography & Mathematics nilimaliza MWEZI aw Sita nkaanza kazi Mwezi wa 9 same year Loksale Sec School, mwaka uliofuata MWEZI wa tisa nikajiunga chuo kikuu Iringa Bed in Mathematics nikamaliza July 2010, February nkaajiriwa tena kituo kingine coz ajira yangu Loksale ilifutwa, Sasa nafundisha Shule moja kongwe hapa Arusha Manispaa una la zaidi? "Zimwi likujualo halikuli likakwisha" msaada kwa mwanafunzi hadi niwe nakujua vinginevyo mfate JK,KAAMBWA,NA HAO MAJAJI labda watawasaidia
 
Watoto sawa twawaonea huruma ila kwa nn wazazi wao hawatuungi mkono? Na hii yote ni kwa sababu ya kupakata hili loba la kinyesi (mafisadi) wazazi ndo wanawaweka serikalini ngoja tuwafunze adabu miaka miwili ijayo 1 na 2 zitoke private tu ndo wataona uchungu.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 

Mimi ni professional teacher Dip Monduli TTC Geography & Mathematics nilimaliza MWEZI aw Sita nkaanza kazi Mwezi wa 9 same year Loksale Sec School, mwaka uliofuata MWEZI wa tisa nikajiunga chuo kikuu Iringa Bed in Mathematics nikamaliza July 2010, February nkaajiriwa tena kituo kingine coz ajira yangu Loksale ilifutwa, Sasa nafundisha Shule moja kongwe hapa Arusha Manispaa una la zaidi? "Zimwi likujualo halikuli likakwisha" msaada kwa mwanafunzi hadi niwe nakujua vinginevyo mfate JK,KAAMBWA,NA HAO MAJAJI labda watawasaidia

kweli ndo mana walimu mnadharaulika! kama elimu yenyewe ndo imekufikisha hapa! poor teacher! kale vumbi.
 
YAANI Sa hivi wataisoma namba! Nikiingia vipindi double class nafundisha dk 15 tu hizo nyingine napiga porojo na ole wake mwanafunzi aniulize swali! Atajuta. Ila navionea huruma vianafunzi vyangu vya form maana tulipoishia ndo hapo hapo siendelei wala nini, na notice siwapi watafelije? Ila itakuwa funzo kwa wazazi wao siku nyingine wavote wisely, sio wana chagua viongozi wasio wathamini. MUHIMU WALIMU KWA NAMNA YEYOTE ILE TUJITAHIDI KUWASAIDIA WATOTO WA WALIMU WENZETU NA TUJARIBU KUWAIDENTIFY MASHULENI ILI TUWASAIDIE KIELIMU!

Kweli wewe mchonganishi... wanangu bahati hawasomi saint Kayumba!
 
kweli ndo mana walimu mnadharaulika! kama elimu yenyewe ndo imekufikisha hapa! poor teacher! kale vumbi.

Markj wewe hujajua mateso ya hii taaluma u wouldn't write such words hatupendi kaa madr walivyogoma na kuwaacha helpless patients kwa vitanda wodini bt what do we do kama hata wewe tu hutuonei huruma?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom