Walimu nao wapewe Posho za mwezi kama maaskari

Gai da seboga

JF-Expert Member
Apr 19, 2019
482
969
Habar zenu mabibi na mababu,

Mwalimu ni mtu anaesaidia wengine kupata ujuzi, maarifa na tunu. Mwalimu ndie anaezalisha Madaktari, manesi, bwana afya, wanasiasa, wafanyabiashara n.k, na wote mnaweza kukubaliana nami kuwa bila mwalimu huenda usingeweza kusoma, kuhesabu na kuandika.

Pamoja na uzito huo alonao mwalimu lakini hakuna watumishi wa serikali wenye hali mbaya ya kiuchumi kama walimu yaani mishahara ni midogo, mikopo kwenye mabenki, hakuna nyongeza ya mshahara, hakuna kupanda madaraja, hana cha kulipwa over time, hakuna cha pesa za semina kama zamani, hakuna ata kudunduliza kupata hela ya tuisheni yani ni shida tupu zimewajaa.

Mbaya zaidi kwenye sekta ya ualimu kila mtu ni bosi wako yani hata mwenyekiti wa mtaa anaweza kuja ofisini kwako na akakugombesha na hata kukutia makofi, ni sekta ambayo imeshushiwa heshima kwa kiasi kikubwa sn.

Leo hii ukimkuta mwalimu barabarani anaongea peke yake unaweza kusema amemeza notes kumbe ni msongo wa mawazo unampeleka puta Vibaya mno akifikiria ni miaka mitano sasa lakini bado mshahara ni ule ule hakuna ata senti ya nyongeza, hajapanda daraja, anachopokea mwisho wa mwezi ni laki mbili akikatwa mkopo alochukua benki, huku ukizingatia gharama za maisha zimepanda na familia imeongezeka.

Kiukweli ukipasua vifua vya walimu utakutana na masononeko makubwa mnoo, walimu wamechooka sana ule uvumilivu walokuwa wanasifiwa nao sasa haupo tena nao ni binadamu, walimu wameshachoka na kutothaminiwa maslahi yao ni ule uoga tu wa kutosema hadharani wakihofia kupoteza ata hako kibarua. Leo hii bora ya bwana afya anaweza pata posho ya kukagua nyama na akarudi na kilo ya nyama nyumbani, heri ya maaskari wenye posho kila mwezi, heri ya watumishi wengine wenye hadi marupurupu ya overtime.. Leo hii kwa shida anazonuka mwalimu tukitaka kuwavalisha kiatu hiki cha mwalimu watumishi wengine wa serikali basi lazima kiwabane tu.

Asilimia 100% walimu waliamini kuwa kupata Rais ambae ni mwalimu kungepelekea kuboreshewa maslahi yao na mazingira ya kazi kwani anayajua yote yaliyomo kwenye sekta ya ualimu lakini mambo yamekuwa tofauti kabisa mpaka walimu wanawaza ni nani sasa atakuja kuwa mtetezi wao kama sio mwalimu mwenzao.! Mara nyingi Mh Rais Magufuli amekuwa akinukuliwa akisema kuwa serikali yake haitawaacha walimu (maneno ambayo yamezoeleka masikioni mwa walimu mwaka wa 6 huu) tena anaenda mbali kwa kusema kuwa yeye ni mwalimu, mkewe ni mwalimu, waziri mkuu ni mwalimu, mkewe ni mwalimu, huku baraza lake la mawaziri likiwa limesheheni walimu mbalimbali, lakini yote haya haijawahi kamwe kuwa chachu ya kuthaminiwa maslahi ya walimu. Kiasi kwamba walimu sasa wanamkumbuka na kumlilia mh Kikwete kwa namna alivyokuwa akiwapandishia watumishi mishahara yao.

Mheshimiwa Rais Magufuli walimu wako wamekata tamaa na wamechoka na maneno yako ya matumaini yasiyozaa matunda kila siku kuwa serikali yako iko pamoja na walimu lakin wapi! kiasi kwamba wanafanya kazi ilimradi siku ziende tu lakini hawana motisha yoyote wanayoipata ili kufanya kazi kwa moyo wote. Tena walimu wako wanatamani muda wako wa kuongoza (kutawala) uishe ata kesho ili wabadilishe upepo angalau Raisi ajae anaweza kuwaona na kujali maslahi yao.

Mheshimiwa Rais John Magufuli ikikupendeza walimu nao wapate posho za kila mwezi kama maaskari ili iwe sehemu ya kuwapa motisha wachape kazi kisawasawa, na ni imani yangu walimu wakiwekewa utaratibu wa kupata posho walau laki mbili basi tutaingia katika Mapinduzi makubwa ya elimu mana walimu watafanya kazi kufa kupona na kutakuwa na ushindani na hari ya kufundisha. Mhe Raisi wahurumie Walimu wenzako wanashindwa kukwambia ukweli kwasababu wanakuogopa.

~Gai da Seboga (Mwalimu wa Kujitolea)
 
Walimu hamna msimamo nyie, malalamiko kibao ukija uchaguzi mnachagua kijani! Acha namba zisomeke ili akili ziwarudie! Tena mtukufu ongeza hata makato ya bodi ya mikopo yafike 30% tujenge reli na madaraja!
 
Ungeandika mwalimu ambaka mwanafunzi wake, au mwalimu akimbia na pesa za ujenzi wa madarasa, watu was ofisi ya rais wangefungua haraka sana kuusoma huu uzi kwa lengo wapi uko waende mshugulikia uyo mwalimu ili wapate sifa

Mwalimu asikilizwi matatizo yake bali anashugulikiwa makosa yake kwaiyo mitano tena mwalimu usife moyo
 
Ungeandika mwalimu ambaka mwanafunzi wake, au mwalimu akimbia na pesa za ujenzi wa madarasa, watu was ofisi ya rais wangefungua haraka sana kuusoma huu uzi kwa lengo wapi uko waende mshugulikia uyo mwalimu ili wapate sifa

Mwalimu asikilizwi matatizo yake bali anashugulikiwa makosa yake kwaiyo mitano tena mwalimu usife moyo
Wewe una akili sana. Viongozi wengi wa serikali ni wajinga wakubwa. Hawapo tayari kushughulikia masuala ya msingi, isipokuwa tu yale ya kipuuzi.
 
Askari analipwa posho kwa sababu yuko kazini 24hrs na hii iko kwenye sheria zao imeandikwa kabisa.

Maana yake ni kwamba askari muda wowote akihitajika kazini anatakiwa kwenda, iwe ni mchana iwe ni usiku, yuko zamu hayuko zamu atatakiwa kuvaa uniform na kutekeleza majukumu aliyoitiwa muda huo.

Kwa mfano ile miezi ya mwisho wa mwaka ambayo walimu mnaenda sikukuu kada zote za uaskari likizo zote husimamishwa kwa sababu suala la ulinzi linakuwa muhimu sana wakati huo kwahiyo askari wanakuwa standby kwa 75%+.

Mwalimu ukishapiga kazi masaa yako 8 kwa siku unarudi home kucheza na watoto wako huoni ni scenario tofauti sana? Askari anakuwa zamu alaf muda wa kutoka anapewa amri ya kuongeza masaa hata kumi au 20 kazini au pengine siku kadhaa tena bado unaona mnafanana?
 
Utakufa maskini iwapo utaendelea kulia lia na kujiona mnyonge. Unapoteza muda wako kumpigia mbuzi gitaa! Kujiongeza kwa wafanyakazi wote hakukwepeki kwa sasa!

Ni bora kuhamishia nguvu na akili zetu kwenye mambo yetu binafsi badala ya kazi yenye manyanyaso. Dawa ya moto ni moto tu. Huduma zikiendelea kudorora, akili zao zitawakaa sawa tu.

Fungua biashara, anzisha shughuli za kilimo na ufungaji, endesha boda boda, nk. Ili kujiongezea kipato. Ukipata wasaa wa kumuibia muda mwajiri, iba kama huna akili nzuri vile! Ndivyo wanavyotaka tufanye.

Haiwezekani miaka zaidi ya sita tuishi kwa mishahara ile ile!
 
Utakufa maskini iwapo utaendelea kulia lia na kujiona mnyonge. Unapoteza muda wako kumpigia mbuzi gitaa! Kujiongeza kwa wafanyakazi wote hakukwepeki kwa sasa!

Ni bora kuhamishia nguvu na akili zetu kwenye mambo yetu binafsi badala ya kazi yenye manyanyaso. Dawa ya moto ni moto tu. Huduma zikiendelea kudorora, akili zao zitawakaa sawa tu.

Fungua biashara, anzisha shughuli za kilimo na ufungaji, endesha boda boda, nk. Ili kujiongezea kipato. Ukipata wasaa wa kumuibia muda mwajiri, iba kama huna akili nzuri vile! Ndivyo wanavyotaka tufanye.

Haiwezekani miaka zaidi ya sita tuishi kwa mishahara ile ile!!
 
Mshahara wa mwalimu na askari ni sawa kabisaaaa...... Kama huyu mwalimu anahitaji tumuongezee posho afanye yafuatayo

Kama ilivyo askari...
Akubali kufundisha usiku kama ambavyo askari ana zamu za ulinzi usiku na doria za mara kwa mara.

Awe kazini siku saba za wiki kama ambavyo jumamosi na juma pili vituo vya polisi na majeshi yapo kazini.

Akubali standby muda wowote ya siku zaidi ya 30 bila kuiona familia yake.

Kama mwalimu hatakubaliana na haya afanye yafuatayo.
Atumie muda wake wa ziada kutengeneza kipato na wapo wengi waliofanikiwa kwa mfumo huu.. ingia asubuhi toka sa nane tafuta kazi ya ziada. Wengine wana hadi shift wanafanya kazi kwa masaa manne tu kwa siku.

Waboreshe taasisi zao ikiwemo Benki ya walimu iwe ni sehemu pekee kwao kukopa na kwa riba nafuu...

CWT waiondoe katika mfumo wa chama kwa.maslahi yao vinginevyo wasitegemee mimi mfanyakazi wa TANAPA ntawasema.


Kila la kher mwalimu katika kutafuta mabadiliko
 
Utakufa maskini iwapo utaendelea kulia lia na kujiona mnyonge. Unapoteza muda wako kumpigia mbuzi gitaa! Kujiongeza kwa wafanyakazi wote hakukwepeki kwa sasa!

Ni bora kuhamishia nguvu na akili zetu kwenye mambo yetu binafsi badala ya kazi yenye manyanyaso. Dawa ya moto ni moto tu. Huduma zikiendelea kudorora, akili zao zitawakaa sawa tu.

Fungua biashara, anzisha shughuli za kilimo na ufungaji, endesha boda boda, nk. Ili kujiongezea kipato. Ukipata wasaa wa kumuibia muda mwajiri, iba kama huna akili nzuri vile! Ndivyo wanavyotaka tufanye.

Haiwezekani miaka zaidi ya sita tuishi kwa mishahara ile ile!!
Tatizo unarahisisha Sana ndugu yangu,hii kada isikie tu ila usiingie humo ndani.
Kwanza hii kada walimu kwa walimu hawapendani kabisa full kuoneana wivu ,kuchomana kwa wakubwa Ni Jambo la kufikia.

Ukijiongeza kufanya biashara hasa kwa sehemu nyingi walimu wenzio watakupiga Sana vita full figisu za kuhakikisha hutoboi kabisa.

Wakuu wa shule ,walimu wakuu ,waratibu elimu kata hawa ndio virus kwa walimu maana wao Wana posho na wamepewa hiyo posho kwa Kaz maalum ya kuhakikisha wanakandamiza walimu ,hivyo ukionekana unataka kuleta mageuz jiandae kushughulikiwa na hili kundi.

Pia Kuna baadhi ya walimu Tena walio wengi Ni masnitch balaaa yaan kusalitiana wenyew kwa wenyew ,yaan ukikaa na baadhi ya walimu hata maongez yao unaona kabisa hawa Ni watu wa kujipendekeza ,hata upeo wao mara nyingine unaleta mashaka Sana pind wakiwa wanajieleza.

Kwahiyo hiyo point yako sio rahis Kama ulivyowaza ni vigum Sana kuitekeleza inahitaj uwe mafia Sana na uwe tayal kupambana na figisu na kuwa tayal kuacha hata Kaz kma hauna njaa kiivo.
 
Tatizo unarahisisha Sana ndugu yangu,hii kada isikie tu ila usiingie humo ndani.
Kwanza hii kada walimu kwa walimu hawapendani kabisa full kuoneana wivu ,kuchomana kwa wakubwa Ni Jambo la kufikia.

Ukijiongeza kufanya biashara hasa kwa sehemu nyingi walimu wenzio watakupiga Sana vita full figisu za kuhakikisha hutoboi kabisa.

Wakuu wa shule ,walimu wakuu ,waratibu elimu kata hawa ndio virus kwa walimu maana wao Wana posho na wamepewa hiyo posho kwa Kaz maalum ya kuhakikisha wanakandamiza walimu ,hivyo ukionekana unataka kuleta mageuz jiandae kushughulikiwa na hili kundi.

Pia Kuna baadhi ya walimu Tena walio wengi Ni masnitch balaaa yaan kusalitiana wenyew kwa wenyew ,yaan ukikaa na baadhi ya walimu hata maongez yao unaona kabisa hawa Ni watu wa kujipendekeza ,hata upeo wao mara nyingine unaleta mashaka Sana pind wakiwa wanajieleza.

Kwahiyo hiyo point yako sio rahis Kama ulivyowaza ni vigum Sana kuitekeleza inahitaj uwe mafia Sana na uwe tayal kupambana na figisu na kuwa tayal kuacha hata Kaz kma hauna njaa kiivo.
Duh!! Ni hatari.
 
Askari polisi mwenye elimu ya kidato cha nne:-kipato chake kwa mwezi ni kama ifuatavyo hapa chini:-

Basic salary ni Tsh.430,000/=
Posho ya chakula Tsh.300,000/=
Posho ya vinywaji Tsh.100,000/=
Posho ya mavazi Tsh. ............/=
Posho ya nyumba Tsh............./=

Bado unaweza kukuta askari huyu ni traffic barabarani,yupo idara ya upelelezi au katika vitengo vingine ambavyo sent nje ya mshahara haikosekani.

Hapo hujamgusa graduate wa jeshi la polisi!!Dah walimu tuna hali ngumu sana ndg zangu.
 
hongereni sana lakini maana bado mnaendelea kufaulisha pamoja na changamoto zote hizo
 
Mshahara wa mwalimu na askari ni sawa kabisaaaa...... Kama huyu mwalimu anahitaji tumuongezee posho afanye yafuatayo

Kama ilivyo askari...
Akubali kufundisha usiku kama ambavyo askari ana zamu za ulinzi usiku na doria za mara kwa mara.

Awe kazini siku saba za wiki kama ambavyo jumamosi na juma pili vituo vya polisi na majeshi yapo kazini.

Akubali standby muda wowote ya siku zaidi ya 30 bila kuiona familia yake.

Kama mwalimu hatakubaliana na haya afanye yafuatayo.
Atumie muda wake wa ziada kutengeneza kipato na wapo wengi waliofanikiwa kwa mfumo huu.. ingia asubuhi toka sa nane tafuta kazi ya ziada. Wengine wana hadi shift wanafanya kazi kwa masaa manne tu kwa siku.

Waboreshe taasisi zao ikiwemo Benki ya walimu iwe ni sehemu pekee kwao kukopa na kwa riba nafuu...

CWT waiondoe katika mfumo wa chama kwa.maslahi yao vinginevyo wasitegemee mimi mfanyakazi wa TANAPA ntawasema.


Kila la kher mwalimu katika kutafuta mabadiliko
Askar hawez mfikia Mwalimu kwa mshahara Hilo Nina uhakika nalo kabisa .kinachomboost askar Ni ile posho ambayo kwenye mafao Haina madhara yoyote Yale .

So hapa kwa upande wa mafao mwalim lazima ampige gepu kubwa Sana askar ila nae askar anakuja mpiga gepu Mwalimu kwenye kaposho tu .

Take home ya askar anaeanza Kaz Ni around 350 wakat Mwalimu grade A 360,Diploma 450,bachelor 550 hizo Ni makadirio maana sijaweka visent .
 
Back
Top Bottom