mwalimu em fanyeni kufelisha madogo.. yaan hakikisheni watakaofeli mwakani wanavunja record ya mwaka huu... yaan mnaongea kwa vitendo mbona serikali itatia adabu... bampa tu bampa hakuna haja ya kulalamika!
Unajua mi walimu wa nchi hii nawaona wajinga kiasi cha kupindukia.
Nadiriki kuwafananisha na mpishi wa ndani, anayepika chakula cha bosi wake, anapakua chote anampelekea bosi bahati mbaya anamwambia hakitoshi, na wakati yeye ni mpishi tu halafu mpishi yule anahangaika kwenda kukopa dukani ampikie bosi cha kutosha,
Mpishi mzuri ni yule kwanza anahakikisha bosi wake anakula chakula ambacho hata yeye amekula, kisipo tosha aviache aone kama bosi asiposhiba mara mbili mara tatu na wakati mwingine akose kabisaaa uone ataamua nini.
Sasa tuje kwa walimu, utamkuta mwalimu anahangaika mpaka kununua vitu vya kufundishia halafu anabwabwaja eti mshahara hautoshi,
Mwalimu unajijua kabisaa nyie ndio chesesi ya nchi yoyote, mnaweza amua hivi:-
1. Wacheni maneno fanyeni kwa vitendo.
Sio kufoka tu kwenye kibodi kama watoto huko mnadai haki zenu.
2. Tafute miaka kama 7 au 10 ya kuhakikisha hakuna divi 4 yaani zianzue 0 kushuka chini. Na atakaewauliza mumwambie bayana.
Ili ualimu uheshimike, kwanza nyie vizazi vya walimu mliopo mjitoe muhanga sawasaw na wale wazee waliouza maisha yao kutafuta ukombozi.
Wazee walikufa sanaa ndio maana sisi leo tupo hapa tunafurahi,
3. Daini masilahi mapana na sie yale ya kiu tuu.
Eti mwalimu unasimama unadai hela ya likizo, na ambaye hajaenda likizo jee ajitoe kwenye harakati?? Muache ubinafsi
Mnakua na kiu kama ya mvuta sigara, atahaha kuitafuta weeee hata kwa gharama akivuta mikupuo miwili akianza kurudi alichokipata hakipo tena??
4. Amueni kufanya mapinduzi kifikra kwanza kabla ya kitu kingine.
Walimu waliowengi wametekwa ki fikra kuliko kada yoyote ile, mi mwanzoni nilifikiri kutojiamini kwa mwalimu kunatokana labda kwa kuwa matokeo yake huko nyuma sio mazuri.
Lakini wapo watu ambao mwalimu anawazidi ki elimu kwa mbaali sana, matharani ulinzi na usalama, afya hasa hawa wa chini, nafundi n.k
Lakini wao wanajiamini tatizo ni kwa walimu tuu
5. Kataeni kutumika kisiasa
Hii itawafanya mjisimamie vema katika maamuzi yenu.
Mwishooo
Kama haw wasikii tafuteni miaka kama 7 au 10 ya kufelisha kwa kiwango cha divi zerooo.
Pia,
Daini haki zenu kwa pamoja sio kila mtu anakuja na vilisiti vyake, utakuta unapiga kelele weee unachodai hakifiki hata milioni tatu, hiyo ni njaaa itakua inakusumbua.
Fanyeni mapinduzi na maamuzi magumu kama babu zetu.
MASLAHI MAPANA NA MAZINGIRA BORA YA KUFANYIA KAZI KWA WALIMU, YAKO NDANI YA FIKRA PEVU MTAVYOTAKA NINYI NA SI SERIKALI
NYINYI NDIO MNAPASWA MUIAMBIE NINI SERIKALI CHA KUFANYA NA SI SERIKALI KUWAAMBIA CHA KUFANYA.
MFANO TU MDOGO
UKIMUAJIRI FUNDI AKUJENGEE NYUMBA, MWISHO WA SIKU ATAKUELEKEZA VITU VYA KUFANYA NA KUKUSANYA, NA SIO WEWE KUANZA KUSHIKA PIMA MAJI NA KUMUELEKEZA FUNDI CHA KUFANYA.
NARUDIA TENA WALIMU JIVISHENI MIOYO YA KISHUJAA KUWAANDALIA MAZINGIRA MAZURI WALIMU WAJAO.
UKOMBOZI HAUJI BILA KUMW........