Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,168
- 18,012
Nikiwa najiandaa kwenda kula Pasaka nje ya mji nimeona niache swali hapa ili hata nikiwa nje ya kamji kangu kaitwacho Cyber Village ntapata nafasi ya kuona kwamba huku tukiila Pasaka tunaweza kuwepo hapa jamvini JF kubadilishana mawazo.
Sasa leo nina swali kuhusu shirika la reli ya kati Tanzania.
Sote twajua kwamba njia za reli hii zilijengwa na watanzania wakisimamiwa na wakoloni na ilikuwa ni katika kuhakikisha malighafi, na mazao vinasafirishwa katika muda muwafaka bila kusahau watu.
Lakini pia ujenzi wa reli yoyote ile unaweza kuleta manufaa makubwa kwa chi husika.
Baadhi ya manufaa hayo ni pamoja na urahisishaji wa usafiri kwa watu ambao huweza kusafiri kutoka kona moja ya nchi hadi ingine.
Kisiasa, watu huweza kupata mwanga wa nini kinaendelea nchini mwake na pia kuwa na uhakika wa kupata habari kupitia magazeti ambayo huweza kusafirishwa na kufika kila mahala.
Kiuchumi ndio kabisa watu wataweza kusafirisha bidhaa zao kwa ufanisi kupitia miji mbalimbali na shughuli za kibenki kuweza kusamba kila kona ya nchi kutoka mijini hadi vijijini.
Pia katika hili la uchumi ndio unaweza kuona kwamba sehemu kama Dodoma au Singida inaweza kufanzwa kama ndio kituo kikubwa (trading centre) ya Tanzania ambapo watu kutoka mikoa yote nchini huweza kukutana na kufanza mikakati mbalimbali ya biashara.
Kwa hio reli tu ni moja ya njia kuu za kukuza uchumi wa Tanzania.
Sasa baada ya miaka 47 sijui, ya uhuru bado watanzania tumeshindwa kusimamia shughuli za reli nchi mwetu ambapo tumefikia kuwa na mizozo ya watumishi wake na pia kufikia kuuza moja ya njia kuu za uchumi wa nchi.
Mimi katika maisha yangu hapa Cyber Village huwa natumia sana usafiri wa reli na huwa najiuliza kila siku kwamba sisi tumeshindwa nini kusimamia njia hii.
Kwa mfano nchi ya Uingereza bado serikali inamiliki shirika la reli nchini humo. Walichofanza ni kutoa leseni kwa makampuni mbalimbali kama Virgin,North Great Western na zingine, hutumia njia za reli na kulipa kodi tu na kampuni ingine itwayo Network Rail ndio yenye jukumu la kuhakikisha njia za reli ziko imara na salama kila kukicha.
Kwa hio hapa hizi kampuni hupata mapato yake kupitia mtaji wa kwanza ambao hupewa na serikali kuanzisha biashara hio na nauli mbalimbali kutoka kwa watumiaji wa huduma hio.
Hapa moja kwa moja serikali inakuwa imetoa mwanya kwa wananchi kupata ajira, bidhaa kusafirishwa kwa ufanisi kama barua na kadhalika kwa hio sula la ajira linakuwa limetatuliwa kwani watu watakuwa wanajenga, wanaendesha na kusimamia huduma za reli.
Faida zingine ni pamoja na wabunge kuweza kusafiri kwa kutumia njia ya reli na kuokoa fwedha kibao ambazo zinapotezwa kwa kununua magari yenye gharama kubwa.
Sasa je tumeitumia vipi njia hii muhimu kwa uchumi wa Tanzania?
Kwa wale ambao wangependa kujiendeleza kwa kusoma zaidi masuala ya uhandisi wa reli mnaweza kubarizi link hio hapo chini.
http://www.railway.bham.ac.uk/index.htm
Kheri ya Pasaka.
Sasa leo nina swali kuhusu shirika la reli ya kati Tanzania.
Sote twajua kwamba njia za reli hii zilijengwa na watanzania wakisimamiwa na wakoloni na ilikuwa ni katika kuhakikisha malighafi, na mazao vinasafirishwa katika muda muwafaka bila kusahau watu.
Lakini pia ujenzi wa reli yoyote ile unaweza kuleta manufaa makubwa kwa chi husika.
Baadhi ya manufaa hayo ni pamoja na urahisishaji wa usafiri kwa watu ambao huweza kusafiri kutoka kona moja ya nchi hadi ingine.
Kisiasa, watu huweza kupata mwanga wa nini kinaendelea nchini mwake na pia kuwa na uhakika wa kupata habari kupitia magazeti ambayo huweza kusafirishwa na kufika kila mahala.
Kiuchumi ndio kabisa watu wataweza kusafirisha bidhaa zao kwa ufanisi kupitia miji mbalimbali na shughuli za kibenki kuweza kusamba kila kona ya nchi kutoka mijini hadi vijijini.
Pia katika hili la uchumi ndio unaweza kuona kwamba sehemu kama Dodoma au Singida inaweza kufanzwa kama ndio kituo kikubwa (trading centre) ya Tanzania ambapo watu kutoka mikoa yote nchini huweza kukutana na kufanza mikakati mbalimbali ya biashara.
Kwa hio reli tu ni moja ya njia kuu za kukuza uchumi wa Tanzania.
Sasa baada ya miaka 47 sijui, ya uhuru bado watanzania tumeshindwa kusimamia shughuli za reli nchi mwetu ambapo tumefikia kuwa na mizozo ya watumishi wake na pia kufikia kuuza moja ya njia kuu za uchumi wa nchi.
Mimi katika maisha yangu hapa Cyber Village huwa natumia sana usafiri wa reli na huwa najiuliza kila siku kwamba sisi tumeshindwa nini kusimamia njia hii.
Kwa mfano nchi ya Uingereza bado serikali inamiliki shirika la reli nchini humo. Walichofanza ni kutoa leseni kwa makampuni mbalimbali kama Virgin,North Great Western na zingine, hutumia njia za reli na kulipa kodi tu na kampuni ingine itwayo Network Rail ndio yenye jukumu la kuhakikisha njia za reli ziko imara na salama kila kukicha.
Kwa hio hapa hizi kampuni hupata mapato yake kupitia mtaji wa kwanza ambao hupewa na serikali kuanzisha biashara hio na nauli mbalimbali kutoka kwa watumiaji wa huduma hio.
Hapa moja kwa moja serikali inakuwa imetoa mwanya kwa wananchi kupata ajira, bidhaa kusafirishwa kwa ufanisi kama barua na kadhalika kwa hio sula la ajira linakuwa limetatuliwa kwani watu watakuwa wanajenga, wanaendesha na kusimamia huduma za reli.
Faida zingine ni pamoja na wabunge kuweza kusafiri kwa kutumia njia ya reli na kuokoa fwedha kibao ambazo zinapotezwa kwa kununua magari yenye gharama kubwa.
Sasa je tumeitumia vipi njia hii muhimu kwa uchumi wa Tanzania?
Kwa wale ambao wangependa kujiendeleza kwa kusoma zaidi masuala ya uhandisi wa reli mnaweza kubarizi link hio hapo chini.
http://www.railway.bham.ac.uk/index.htm
Kheri ya Pasaka.