Steven Sambali
JF-Expert Member
- Jul 31, 2008
- 352
- 170
WanaJamii,
Kuna watalii wasio wa kawaida na kwa sasa niandikavyo ni kuwa wapo tayari Tanzania. Wapanda mlima hao walifikia Kenya na huko wakapokelewa na makamu wa rais wa Kenya. Leo jioni kutokana na News ni kuwa tayari wameshafika Tanzania na wamefikia Arusha. Wameshangazwa na baridi ya pale kwani wao wanafikiri Africa ni Sahara tu. Safari yao imeandaliwa na Mama mmoja ambaye ni Actor aitwaye Anna Dymna. Lengo la safari ni kuja Tanzania na kupanda mlima Kilimanjaro.
Nisingeandika hii habari kama si kwamba, wapandaji wote ni vilema. Wengine hawana macho (Vipofu), wengine hawana mikono na wengine miguu. Katika hawa kuna bwana mdogo mmoja aitwaye Jan Mela ambaye na yeye ni kivutio kikubwa. Alikatwa mkono mmoja baada ya kuwa amenaswa na umeme. Pamoja na ulemavu huo, alijitahidi na kwenda na mwisho kufika kwenye POLE zote yaani North Pole na South Pole. Baridi la huko kwa kweli latisha.
Naandika ili kama kuna wahusika basi wachangamkie hili tukio kwani ni tangazo kubwa sana la utalii kwa Tanzania. Waandishi wa habari na wizara husika fuatilieni na muone twaweza watumiaje hawa vilema wapandao Kilimanjaro yetu. Mungu Ibariki Tanzania.
Kwa watao taka maelezo zaidi basi angalieni kurasa hizi. Ila zimeandikwa Kipolishi na itabidi mjaribu kutafasiri kwa kutumia Google.
FOTO
Wahusika wote wanaonekana hapa pamoja na maelezo yao kwa ufupi.
Kilimandżaro 2008 â Mimo Wszystko - Uczestnicy
Kuna watalii wasio wa kawaida na kwa sasa niandikavyo ni kuwa wapo tayari Tanzania. Wapanda mlima hao walifikia Kenya na huko wakapokelewa na makamu wa rais wa Kenya. Leo jioni kutokana na News ni kuwa tayari wameshafika Tanzania na wamefikia Arusha. Wameshangazwa na baridi ya pale kwani wao wanafikiri Africa ni Sahara tu. Safari yao imeandaliwa na Mama mmoja ambaye ni Actor aitwaye Anna Dymna. Lengo la safari ni kuja Tanzania na kupanda mlima Kilimanjaro.
Nisingeandika hii habari kama si kwamba, wapandaji wote ni vilema. Wengine hawana macho (Vipofu), wengine hawana mikono na wengine miguu. Katika hawa kuna bwana mdogo mmoja aitwaye Jan Mela ambaye na yeye ni kivutio kikubwa. Alikatwa mkono mmoja baada ya kuwa amenaswa na umeme. Pamoja na ulemavu huo, alijitahidi na kwenda na mwisho kufika kwenye POLE zote yaani North Pole na South Pole. Baridi la huko kwa kweli latisha.
Naandika ili kama kuna wahusika basi wachangamkie hili tukio kwani ni tangazo kubwa sana la utalii kwa Tanzania. Waandishi wa habari na wizara husika fuatilieni na muone twaweza watumiaje hawa vilema wapandao Kilimanjaro yetu. Mungu Ibariki Tanzania.
Kwa watao taka maelezo zaidi basi angalieni kurasa hizi. Ila zimeandikwa Kipolishi na itabidi mjaribu kutafasiri kwa kutumia Google.
FOTO
Wahusika wote wanaonekana hapa pamoja na maelezo yao kwa ufupi.
Kilimandżaro 2008 â Mimo Wszystko - Uczestnicy