Wale walio na wababa wanoko uwanja huu wenu

Wale walio na wababa wanoko uwanja huu wenu

google helper

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2013
Posts
9,667
Reaction score
13,868
salamu zenu wakuu.

Kama ilivyo kila mmoja ametoka katika familia tofauti tofauti kimalezi. Malezi ya familia nyingine kwa kweli mtihani. Baba ni kama Simba mbugani yaani muda wake wa kurudi watoto na mke wote hawana amani, raha wala furaha.

Japo sijatoka katika hizo familia ila nimekaa na familia moja karibu, yaaani Zee likifika lazima usikie kilio tu leo watoto, kesho mke wake mfanyakazi nk.

Wadau mliozaliwa na kulelewa katika hizo familia ebu tupeni mikasa yetu mlikuwa mnafanya nn mshua anakuwa mbogo kila siku? wapo na wale waliokuwa wakiambiwa wawalete wazazi, wako tayari kulipa mlevi yeyote mtaani awe kama mzazi kuliko ngumi na mateke, makofi, kutoka kwa mshua.
karibuni wadau.......

Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
 
Baba ni baba tu aijalishii yukoje bado ni baba inapaswa kumuheshimu, japo aliniharibu kisaikolojia mpaka Leo siwezi kukaa kuongea nae chochote kile labda yeye ndio awe na jambo la kunambia (Hofu alionijengea nilipokua mtoto mpaka Leo ipo) nimepitia mengi kutukanwa matusi ya ajabu nilipokua mtoto, kunibagua n.k still namuheshimu na siwezi kumuita mnoko kanisomesha mpaka nimefika hapa Mwenyezi Mungu amjalie maisha marefu ameen.
 
Baba ni baba tu aijalishii yukoje bado ni baba inapaswa kumuheshimu, japo aliniharibu kisaikolojia mpaka Leo siwezi kukaa kuongea nae chochote kile labda yeye ndio awe na jambo la kunambia (Hofu alionijengea nilipokua mtoto mpaka Leo ipo) nimepitia mengi kutukanwa matusi ya ajabu nilipokua mtoto, kunibagua n.k still namuheshimu na siwezi kumuita mnoko kanisomesha mpaka nimefika hapa Mwenyezi Mungu amjalie maisha marefu ameen.
kama mimi vileee
 
Baba ni baba tu hawezi kuitwa mnoko.

Baba yangu hakuwa na tabia ya kupiga piga ovyo na sijawahi kusikia tusi kinywani make, sijawahi kumuona anakunywa pombe wala kuvuta sigara, ni mtu wa dini sana kila ikifika siku ya ibada yupo na shughuli nyingi kama vikao kabla havijaanza anamtanguliza kwanza mungu.

Ila bado nilipofanya ujinga ujinga alinitandika vizuri, anaweza kusema baba kawahi kunipiga Mara saba tu toka nizaliwe, ila bado hofu ya baba ipo pale pale.

Kanisomesha shule ya msingi English medium, sekondari shule nzuri na chuo sikuwa na mkopo ila aliweza kunipa laki 3 kila mwezi haikuwa baba.

Pamoja na yote hayo, hofu ya baba ipo pale pale, kuongeleshana hivi siwezi labda yeye ndio aniite kuniambia au kunishauri jambo Fulani, na ushauri wake pamoja na maneno yake kwangu vina uzito sana.

Ila yote kwa yote mama ndio namuona kama besti tu, nakumbuka zamani hata nikichelewa kurudi nyumbani nlikuwa namfahamisha kwanza maza nikifika home anitetee kwa mzee.

Baba ni baba tu,
 
Baba ni baba tu aijalishii yukoje bado ni baba inapaswa kumuheshimu, japo aliniharibu kisaikolojia mpaka Leo siwezi kukaa kuongea nae chochote kile labda yeye ndio awe na jambo la kunambia (Hofu alionijengea nilipokua mtoto mpaka Leo ipo) nimepitia mengi kutukanwa matusi ya ajabu nilipokua mtoto, kunibagua n.k still namuheshimu na siwezi kumuita mnoko kanisomesha mpaka nimefika hapa Mwenyezi Mungu amjalie maisha marefu ameen.
Mungu akujalie hayo usemayo, alianzaje mpaka akaanza kuwa mkali ?

Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
 
Mi nakumbuka mdingi kitambo akija Msosi lazma au mwage mama so kipigo watoto tiali tusha fichwa na mama ila mzee wangu tuna mueshimu kama nini
 
Back
Top Bottom