Wale walinda BRAND mnakaza sio?🔥

Wale walinda BRAND mnakaza sio?🔥

Scott junior

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2022
Posts
3,240
Reaction score
4,686
1. Siku ya kwanza mnaona kawaida tuu Kila mtu anahisi mwenzake atamtafuta. kisanga kinaanza siku ya pili ya ukimya.

2 : Siku ya pili inaisha hapo Kila mtu anaanza kupata wasiwasi, Kila mtu anajiuliza maswali mengi

3: Wote mnaanza kuishiwa Raha, notification zikiingia unafungua haraka, unakuta Airtel wamekuambia Airtel watawasiliana na wateja wao kupitia namba 100 tuu.

4: Mnafatiliana kimya kimya
Yan unafatilia Kila anachopost na yeye anafatilia sana ila hamtafutani

5: Mood itapotea hupati usingizi unamuwaza huskii hamu ya chakula, na yeye ni hivyo hivyo
ila mtafanyaje Sasa si mmeamua kulinda Brand.

6: Usiku Kila mtu
anamuwaza mwenzie huyu mbwa atakua ananicheat

7 Kila mtu anatafuta campan ili apunguze mawazo, lla ukiisha achana na hiyo campan moto upo pale pale.😂

8: Kila mtu anajilaumu kimya kimya, Kila mtu anasema labda ningemtafuta tusingekua hapa.

9: mnakuwa na hasira na upendo kwa wakati mmoja Unamkumbuka... lakini bado unaumwa
Unampenda... lakini hutaki kuonekana dhaifu.

10. mmoja anaishiwa pawa anaamua tuu kumtafuta mwenzake anaona yanazungumzika

😂😂😂🔥🔥
 
Tunalinda brandi
20260423_220609.jpg
 
kwenye mahusiano bila mmoja kujishusha hakuna mahali hayo mahusiano yatafika, ni sawa ndani ya familia lazma unyenyekevu uwepo vinginevyo ugomvi hauta kaa uishe.

BRAND hizo ni kwaajili ya vijana wadogo ambao wapo tu bado kwenye stage ya hit and run ila kwa upande wa familia lazma mmoja ajishushe mzani uweze kubalance

napia nna wasiwas sana hao walinda brandy ndo watu wa CHAPUTA 😃 .
 
Hivi kuna watu bado huwa wanafanya hayo mambo!, mbona ni issues zilizopitwa na wakati ni sawa na kuleta zana za u bush men nyakati hizi za akili mnemba!.

Mi kuna mtoto mmoja kipotabo alitaka kuninyima game kwa kujufanya ati amepandisha majini nikaona huyu hajui wahuni ni wanani nilimtekenya yani nilidili na mbavu zake tu!, alipozidiwa alianza kucheka mpaka unaona kidaka tonge!!.. baada ya hapo mambo mengine yakaendelea!. mkuu hata hao wanaojifanya wana ego zipo dawa zao!.
 
kwenye mahusiano bila mmoja kujishusha hakuna mahali hayo mahusiano yatafika, ni sawa ndani ya familia lazma unyenyekevu uwepo vinginevyo ugomvi hauta kaa uishe.

BRAND hizo ni kwaajili ya vijana wadogo ambao wapo tu bado kwenye stage ya hit and run ila kwa upande wa familia lazma mmoja ajishushe mzani uweze kubalance

napia nna wasiwas sana hao walinda brandy ndo watu wa CHAPUTA 😃 .
Hahaha ni kweli mkuu, ila si unajua siku izi watu wanavimbiana hakuna kuonekana DHAIFU
 
kwenye mahusiano bila mmoja kujishusha hakuna mahali hayo mahusiano yatafika, ni sawa ndani ya familia lazma unyenyekevu uwepo vinginevyo ugomvi hauta kaa uishe.

BRAND hizo ni kwaajili ya vijana wadogo ambao wapo tu bado kwenye stage ya hit and run ila kwa upande wa familia lazma mmoja ajishushe mzani uweze kubalance

napia nna wasiwas sana hao walinda brandy ndo watu wa CHAPUTA 😃 .
Mwanangu kuwa na heshima kidogo na Tonye
 
Back
Top Bottom