Nyani Ngabu mimi binafsi ni muumini wa serikali moja lakini kinachosababisha mjadala kuwa wa serikali mbili au tatu ni kutokana na msimamo wa chama tawala juu ya serikali mbili ambayo ni sera yao rasmi sambamba na vyama vikuu vya upinzani kusimamia serikali tatu.Zimekosekana taasisi zenye ushawishi ili kuibua mjadala wa serikali moja.
Lakini kuna baadhi ya vitu kuhusu serikali moja ni dhahiri haitekelezeki kwa mfano Wazanzibar wanataka serikali yao yenye mamlaka kamili kama nchi hili ni gumu kulibadili kwa hapa tulipofikia.Watanganyika ni rahisi kuwashawishi kukubali serikali moja lakini si Wazanzibar hivyo kupona kwa muungano ni kuwa na mfumo au muundo ambao hautawameza.
Fact ya ugumu wa kuwashawishi Wazanzibar kukubali serikali moja ndio inayonifanya binafsi kukubali option ya serikali tatu kama ilivyopendekezwa na tume badala ya hiki kiini macho cha serikali mbili ambacho hata kama imedumu kwa miaka 50 lakini ilipofikia hatuwezi kujidanganya tutakwenda tena miaka mingine 50 kwa mfumo huu huu tukabaki salama.