Wale funza wa miguu waliishia wapi?

Niseme tu wazi wengi tuliozaliwa kidogo 90 kurudi nyuma, 80, 70 aisee hii nchi imetutesa sana, ufukara ulikuwa wa kiwango cha juu sana, ukianza uvaaji wa viatu shida, chupi za VP, mafuta yalikuwa petroleum jelly tu, yani zao la kutoka ktk bidhaa ya petrol, ustaarabu ulikuwa bado sana, usafiri shida ile mbaya kabisa.

Watu walikuwa wanavuta sigara kama fashion, iwe kwenye basi, mgahawani au popote pale akiona watu anawasha manake ni fashion.

Viatu shida, kama ukipata sana unakuwa na araiyoo au ng'inyira, familia yenu ikiwa safi basi unapata chachacha, au kama wa kike utapata loso, zikaja zico n.k

Usafiri full tabu, basi likipita sahau lingine mpaka kesho yake, idadi ya waliosimama ni wengi kuliko walio na siti, mwaka 89 niliwahi safiri toka moshi mjini mpaka iringa mjini nikiwa nimesimama, basi la kampuni ya comfort la mchaga wa marangu, plate number MSB......

Yani mzee mkapa ashukuriwe mno na asamehewe madhambi yake.

Funza kuwa nazo haikuwa aibu manake ilikuwa kampeni mpaka mashuleni kutoana.
 
Kwa faida ya wote hasa vijana wa kileo ni hivi hapo zamani sehemu kubwa za miji mingi haikuwa na lami.

Barabara nyingi zilikuwa ni za vumbi. Sasa hawa funza walikuwa ni wadudu wadogo mithiri ya viroboto wanaokaa kuzunguka sehemu ya jicho la kuku hawa wakijificha ndani ya hilo vumbi la barabarani. Wewe ukipita tu hapo basi tayari unao!

Funza aliingia kidoleni pale sehemu ya chini au juu ya ukucha na kuweka himaya yake hapo. Usipomtoa anataga mayai yasiyo idadi na kuzaliana hapo.

Ukichelewa zaidi kumtoa yale mazalia yanaenea maeneo mengine ya mguu. Usipokaa sawa mguu unapinda kuelekea upande mmoja yani kama ni wa kulia utapinda kuelekea kulia na kama ni wa kushoto utaelekea kushoto. bdae unaweza ukashindwa kabisa kutembea.

Hawa funza walikuingia kama umepita sehemu yenye vumbi hasa vumbi lile laini sana bila kuvaa viatu vya kufunika. Yaani ukivaa ndala, sendo, kobazi lazma uondoke nao. Leo hii ukimuona mhenga aliyepinda miguu kuna uwezekano mkubwa alipitiwa na funza miaka hiyoo!

Leo hii kwa maeneo mengi funza wamebaki kuwa ni hadithi ya kale kwani walitokomea wenyewe tu. Hadi sasa hakujawa na maelezo rasmi ya nini kilichosababisha funza kutokomea.
Watu wengi sana hawajui kuwa hawa funza (jiggers) wanatokana na viroboto (flea). Kwa hiyo ukisema funza wamepotea ina maana viroboto siku hizi hakuna.

Kuenea kwa funza miguuni mara nyingi ni suala la uzembe tu. Hii hapa chi labda ni worst case ya kuwa na funza

1713561340269.png
 
Upatikanaji wa maji ndio umekomesha hao funza, maeneo yenye maji huw hao wadudu hawazalianz na hufa
 
Kwa faida ya wote hasa vijana wa kileo ni hivi hapo zamani sehemu kubwa za miji mingi haikuwa na lami.

Barabara nyingi zilikuwa ni za vumbi. Sasa hawa funza walikuwa ni wadudu wadogo mithiri ya viroboto wanaokaa kuzunguka sehemu ya jicho la kuku hawa wakijificha ndani ya hilo vumbi la barabarani. Wewe ukipita tu hapo basi tayari unao!

Funza aliingia kidoleni pale sehemu ya chini au juu ya ukucha na kuweka himaya yake hapo. Usipomtoa anataga mayai yasiyo idadi na kuzaliana hapo.

Ukichelewa zaidi kumtoa yale mazalia yanaenea maeneo mengine ya mguu. Usipokaa sawa mguu unapinda kuelekea upande mmoja yani kama ni wa kulia utapinda kuelekea kulia na kama ni wa kushoto utaelekea kushoto. bdae unaweza ukashindwa kabisa kutembea.

Hawa funza walikuingia kama umepita sehemu yenye vumbi hasa vumbi lile laini sana bila kuvaa viatu vya kufunika. Yaani ukivaa ndala, sendo, kobazi lazma uondoke nao. Leo hii ukimuona mhenga aliyepinda miguu kuna uwezekano mkubwa alipitiwa na funza miaka hiyoo!

Leo hii kwa maeneo mengi funza wamebaki kuwa ni hadithi ya kale kwani walitokomea wenyewe tu. Hadi sasa hakujawa na maelezo rasmi ya nini kilichosababisha funza kutokomea.
Watu wa zaman usafi mlikuwa hamtilii mkazo lakin pia issue ya afya na chanjo hazikuwa zinapatikana.

Kifupi maisha yameimarika sana kwa sasa.
 
nishawah pata mara moja aseee,ila kale ka muwasho n fantastic 😂🙌🏾
 
Niseme tu wazi wengi tuliozaliwa kidogo 90 kurudi nyuma, 80, 70 aisee hii nchi imetutesa sana, ufukara ulikuwa wa kiwango cha juu sana, ukianza uvaaji wa viatu shida, chupi za VP, mafuta yalikuwa petroleum jelly tu, yani zao la kutoka ktk bidhaa ya petrol, ustaarabu ulikuwa bado sana, usafiri shida ile mbaya kabisa.

Watu walikuwa wanavuta sigara kama fashion, iwe kwenye basi, mgahawani au popote pale akiona watu anawasha manake ni fashion.

Viatu shida, kama ukipata sana unakuwa na araiyoo au ng'inyira, familia yenu ikiwa safi basi unapata chachacha, au kama wa kike utapata loso, zikaja zico n.k

Usafiri full tabu, basi likipita sahau lingine mpaka kesho yake, idadi ya waliosimama ni wengi kuliko walio na siti, mwaka 89 niliwahi safiri toka moshi mjini mpaka iringa mjini nikiwa nimesimama, basi la kampuni ya comfort la mchaga wa marangu, plate number MSB......

Yani mzee mkapa ashukuriwe mno na asamehewe madhambi yake.

Funza kuwa nazo haikuwa aibu manake ilikuwa kampeni mpaka mashuleni kutoana.
ni kweli uchumi ulikuwa mbaya. ni matokeo ya vita ya amin. marehemu mzee ruksa na mkapa walifanya makubwa sana kuifungua nchi na kuitoa nchi kwenye maisha ya ujima ya kuwasha vijinga vya moto na vibatari (hiki kibatari najua kuna wengi tu humu wasiokijua nitakielezea siku moja kilikuwaje na jinsi kilivyofanya kazi)
 
Watu wengi sana hawajui kuwa hawa funza (jiggers) wanatokana na viroboto (flea). Kwa hiyo ukisema funza wamepotea ina maana viroboto siku hizi hakuna.

Kuenea kwa funza miguuni mara nyingi ni suala la uzembe tu. Hii hapa chi labda ni worst case ya kuwa na funza

View attachment 2968732
uko sawa mkuu funza ni zao la viroboto km wale wanaoonekana kwa mbwa au kuku. lakini hawa walikuwa spesho maana walikuwa na uwezo wa kuingia ndani ya ngozi laini ya binadamu na kuzaliana humo.
 
Funza ilikuwa tishio sana miaka hiyo. Yaani kwa tuliozaliwa hadi miaka ya 80 na 90 ni ngumu kukuta mtu hajawahi kutembelewa na funza kabisa. Kimsingi Tanzania ya zamani ilikuwa ngumu sana. Kwa mfano zamani unasafiri kwenye basi wanavuta sigara bila wasiwasi. Ustaarabu haukuwepo. Tanzania nzima ilikuwa inanuka ufukara. Hayati Mkapa ndo alianza kufanya mabadiliko mengi sana.
Mabasi yameandikwa kabisa "USITEME MATE NDANI"
 
Nakumbuka kuna kipindi nikiwa secondary tulienda kibosho aisee tulimkuta binamu yangu ana funza wengi jamani mpaka hawezi kutembea vizuri.Tukamshika(alikua mdogo kwangu) na kuanza kumtoa.
 
Niseme tu wazi wengi tuliozaliwa kidogo 90 kurudi nyuma, 80, 70 aisee hii nchi imetutesa sana, ufukara ulikuwa wa kiwango cha juu sana, ukianza uvaaji wa viatu shida, chupi za VP, mafuta yalikuwa petroleum jelly tu, yani zao la kutoka ktk bidhaa ya petrol, ustaarabu ulikuwa bado sana, usafiri shida ile mbaya kabisa.

Watu walikuwa wanavuta sigara kama fashion, iwe kwenye basi, mgahawani au popote pale akiona watu anawasha manake ni fashion.

Viatu shida, kama ukipata sana unakuwa na araiyoo au ng'inyira, familia yenu ikiwa safi basi unapata chachacha, au kama wa kike utapata loso, zikaja zico n.k

Usafiri full tabu, basi likipita sahau lingine mpaka kesho yake, idadi ya waliosimama ni wengi kuliko walio na siti, mwaka 89 niliwahi safiri toka moshi mjini mpaka iringa mjini nikiwa nimesimama, basi la kampuni ya comfort la mchaga wa marangu, plate number MSB......

Yani mzee mkapa ashukuriwe mno na asamehewe madhambi yake.

Funza kuwa nazo haikuwa aibu manake ilikuwa kampeni mpaka mashuleni kutoana.
Mabadiliko mengi yameanzia kwa mzee Ruksa msijisahaulishe.
 
Nadhani waliishia Kigoma. Haswa Kasulu na Kibondo, ni hatari. Zamani jamaa wengi wa hiyo miji walikuwa wanatembea kama Charlie Chaplin.

chaplin standing1.jpg
 
Back
Top Bottom