Wale funza wa miguu waliishia wapi?

Wale funza wa miguu waliishia wapi?

Braza Kede mara ya mwisho lini kufika Kigoma? Maeneo ya Manyovu, uvinza, Kakonko Nyakanazi n.k
Huko bado funza wametia kambi
Funza ni Wadudu wenye asili ya America ya Kusini na ya Kati. Walikuja Africa kwa kupitia meli za Wareno na waathirika wa kwanza walikuwa Angola.

Ni bahati mbaya kama bado wapo Kigoma lakini kwa sehemu kubwa ya jamii za Kitanganyika hawa wadudu wasumbufu kwa binadamu wametokomezwa kabisa
 
Kama ushawahi kuona mtu ana funza au walikushambuli bas ni muda sahihi wa kuandika wosia watu wagawane Mali zako
 
Hawa hapa
Kwa faida ya wote hasa vijana wa kileo ni hivi hapo zamani sehemu kubwa za miji mingi haikuwa na lami.

Barabara nyingi zilikuwa ni za vumbi. Sasa hawa funza walikuwa ni wadudu wadogo mithiri ya viroboto wanaokaa kuzunguka sehemu ya jicho la kuku hawa wakijificha ndani ya hilo vumbi la barabarani. Wewe ukipita tu hapo basi tayari unao!

Funza aliingia kidoleni pale sehemu ya chini au juu ya ukucha na kuweka himaya yake hapo. Usipomtoa anataga mayai yasiyo idadi na kuzaliana hapo.

Ukichelewa zaidi kumtoa yale mazalia yanaenea maeneo mengine ya mguu. Usipokaa sawa mguu unapinda kuelekea upande mmoja yani kama ni wa kulia utapinda kuelekea kulia na kama ni wa kushoto utaelekea kushoto. bdae unaweza ukashindwa kabisa kutembea.

Hawa funza walikuingia kama umepita sehemu yenye vumbi hasa vumbi lile laini sana bila kuvaa viatu vya kufunika. Yaani ukivaa ndala, sendo, kobazi lazma uondoke nao. Leo hii ukimuona mhenga aliyepinda miguu kuna uwezekano mkubwa alipitiwa na funza miaka hiyoo!

Leo hii kwa maeneo mengi funza wamebaki kuwa ni hadithi ya kale kwani walitokomea wenyewe tu. Hadi sasa hakujawa na maelezo rasmi ya nini kilichosababisha funza kutokomea.
Hawa hapa:
Screenshot_20240419-221956_cropped.png
 
Braza Kede mara ya mwisho lini kufika Kigoma? Maeneo ya Manyovu, uvinza, Kakonko Nyakanazi n.k
Huko bado funza wametia kambi
ndio inawezekana siwezi kukubishia kwa hilo. ila nachojua kwa maeneo mengi ya nchi wadudu hawa hawapo tena.
 
Funza n noma Sana kipindi hicho Ludewa uko funza wa kutosha,wakizidi kweli mguu unapinda, asubuhi huwa Wana washa miguu
Haahaa ni kweli wakiingia kuna kamuwasho fulani katamu ila ukizubaa tu kusikilizia ladha ya huo utamu unakuta ameshataga mayai na ana watoto tayari
 
Matumizi ya maji na sabuni yamechangia sana kupungua kwa funza ingawa bado wapo sehemu zilizosahauliwa, zisizo na lami. Funza chawa na kunguni ni kielelezo cha uchafu wa mwili na kutokujali kanuni za afya.
labda kuna sababu zingine kiongozi ila ivyo vyote havikuwa shida vilikuwepo
 
Kwanza nimshukuru raisi wa awamu ya sita kwa kuhakikisha Jamii yetu inapitia mabadirko makubwa, mbili nimshukuru kuwapa afya njema viongozi wetu wa serikali haswa makamu wa raisi na waziri mkuu,
Niseme bila yeye Funza wangekuwepo mpaka leo hii
 
Daah ila stori zingine bwana🤣🤣 kwamba funza inafanya miguu ipinde?
 
Mliteseka sana poleni aisee!!
-kiongozi shida hazijawahi kuisha.
-maisha ya wkt huo yalikuwa mazuri tu tena pengine bora zaidi ya leo hii.
-mambo mengi tu mazuri yaliwepo. watu wakiishi kwa ubinadam/utu/uaminifu/unyenyekevu halisi. watu wengi wazuri walikuwepo.
-watu hawakuwa wengi km leo.
-hewa safi ya kutosha ilikuwepo.
-heshima iliitangulia pesa.
kwa mazingira ya leo sio rahisi sana ukamuelezea mtu akaelewa ila ni hivyo.
 
Back
Top Bottom