Walaji wa Kambale Dar es Salaam poleni

Walaji wa Kambale Dar es Salaam poleni

Kambale wa hivyo ndio watamu,achana na wale wanaolishwa virutubisho.
Yaani kambale umpate na tui bubu la nazi, nyanya chungu, bamia....hoho na karoti afu umkamulie na kandimu kidogo, tafadhali bhana, pembeni sima ya bada.....mchana wako lazima uwe murua.
Kambale watamu sana maana unakula mpaka miba na kichwa chake.
 
Hivi hawa kambale ndio huku kanda ya ziwa wanaitwa mumi??
Ndo wenyewe ila tofauti ipo kwenye ukubwa.

Size ndogo wanaitwa Sira (kambale) Mumi ni wakubwa sana unaweza ukamkuta ana kilo hata 10 but ni ukoo ule ule
 
Kambale ni samaki mtamu Sana na mwenye minofu yakutosha tuu.. Lakini kwa wapenzi wa kambale hapa bongo poleni kwa kulishwa kambale wanaovuliwa kwenye maji taka ya Mabibo, msasani na kwingineko....
af99cd2413c636b8d6452c9a8da82e5a.jpg
c0e87e2d7748d185c291203009b91587.jpg
Mkuu ukifuatilia hilo wale samaki wa baharini ndo wanakula uchafu zaidi tena mabomba ya taka za hospitali kubwa Dar yanapeleka taka zake baharini lakin mbona bado tunakula ?
 
Kambale anaishi kwenye maji ya hivyo... akiishi swimming pool atakufa, hasa pale itakapokauka, kama hamtaki samaki wa Mabibo na Msasani- wafugeni kambale wenu huku mkiwanywesha maji ya uhai na soda za baridi coca au pepsi... hata keki wapeni... TUONE KAMA WATAKUWA WATAMU.. kama hujasoma biology kila kitu utahoji... hichi chala nini, kile je?.. hata mimea nayo je?.. kwenye mifereji ya uswazi... ila sokoni hutajua atiii!...KULA TULE TUU MUNGU YUPO KAZINI... ILA UPIKE KIIVE KUUA VIJIDUDU
 
Nahisi vijana wetu biology inawahusu japo mpitie vitu basic tu. Kiumbe kinapokula kitu utumbo hufyonza vitamin na madini muhimu kukiwezesha kuishi. Na mabaki na sumu hutolewa nje ya mwili. Pia kuna exceptions....Hv mnajua mavi ya dar maeneo fulani yanamwagwa baharini pale mbele ya ikulu. Na wateja kibao wanajaa ferry kunua samaki kila siku.
hihihihiihihihihihihihih, Mavi kitu gani mi watu wanaojitia kinyaa wananiudhi mno wakati wanachezea mavi yao kila wakienda toilet
 
Hivi huko kanda ya ziwa kambale siyo kamongo? Kambongo wana ile kipande ya mkiani inaitwa lubhee. Hatari sana. Kamongo tamu kusinda nyaaama.
Kambale ndio wanaitwa mumi mkuu, ila wa kanda ya ziwa ni wakubwa mno tofauti na wa kanda ya pwani, maana wao ni wa asili, hawafugwi mabwawani.

Kamongo yeye ni tofauti, anafanana na nyoka, ukimuona anapita kwenye maji kama humfahamu unaweza dhani ni nyoka uatimua mbio.
 
Mimi sili kabisaaa hao Samaki ...vyakula vya watu wa bara
 
hihihihiihihihihihihihih, Mavi kitu gani mi watu wanaojitia kinyaa wananiudhi mno wakati wanachezea mavi yao kila wakienda toilet
Hahahaah ile ya mugabe, kwamba ujanja gani baada ya kuoga unajifutia taulo hadi mku...ni na kesho yake unafutia taulo hilohilo usoni
 
Kambale ndio wanaitwa mumi mkuu, ila wa kanda ya ziwa ni wakubwa mno tofauti na wa kanda ya pwani, maana wao ni wa asili, hawafugwi mabwawani.

Kamongo yeye ni tofauti, anafanana na nyoka, ukimuona anapita kwenye maji kama humfahamu unaweza dhani ni nyoka uatimua mbio.
Kamongo, mumi, mbofu, gogogo, nembe, ningu, soga, furu na wengineo nawafahamu sana mkuu. Ila huko kanda ya ziwa baadhi ya watu uwaita hao kamongo kwa jina la kambale. Japo wengine utumia jina la kambale kumaanisha mumi. Je unajua kwamba kuna aina fulani ya furu wanaitwa nyarukuku?
 
Hausgangai ngombe anakula nyasi anatoa maziwa? Kwani hiyo nyama na kambale akivuliwa inakua na kinyesi au ime-made up of kinyesi? Si ni nyama tu we kula.
 
unashangaa kambale wa mtaroni hushangai kuku mla kinyesi na bata mla vilivyooza ?
 
Back
Top Bottom