Habarini friends,
Hapa ofisini nina mfanyakazi mwenzangu, tumezoeana na kuwa very close friends. Yeye kaolewa huu mwaka wa tano na mumewe kwao wanajiweza kifedha (wakwe), karibu kila siku ananung'unika jinsi wakwe zake na mawifi wanavyoingilia ndoa yao ikiwemo mipango yao ya maendeleo. Wakwe zake na mawifi wote wanaishi mkoa mmoja kinachomkera ni kutwa mama, baba mkwe na dada wa mume kuja hapo kwao na wanakaa hadi usiku. Faragha yao ni usiku na hana uhuru na mumewe. Mbaya zaidi hawawezi kununua kitu chochote cha ndani mfano redio bila kuwashirikisha wakwe japo malipo wanalipa wao. Au hawawezi kwenda hata outing au safari over the weekend bila ruhusa ya wazazi wa mume.
Mwanzoni alivumilia sana ila siku zinavyozidi anakosa raha na mumewe keshaongea nae yeye anasema haoni tatizo la nduguze.
Je hii ni kawaida? Kwa nini wakwe wanataka kujua kila linaloendelea kwa wawili hawa? Afanyeje ili walau awe na muda wa kutosha na mumewe bila kuhofia wakwe kuwakuta?
Binafsi nimemshauri wahamie mbali au ajaribu kuongea na mdhamini wao wa ndoa au hata mchungaji wao kwa ushauri zaidi, yeye anaogopa maana anahofia wakwe kumchukia.
Naomba mawazo yenu ili nimuokoe rafiki yangu, muda wote huwa mnyonge akifikiria ndoa yake.
Thanx in advance
Hapa ofisini nina mfanyakazi mwenzangu, tumezoeana na kuwa very close friends. Yeye kaolewa huu mwaka wa tano na mumewe kwao wanajiweza kifedha (wakwe), karibu kila siku ananung'unika jinsi wakwe zake na mawifi wanavyoingilia ndoa yao ikiwemo mipango yao ya maendeleo. Wakwe zake na mawifi wote wanaishi mkoa mmoja kinachomkera ni kutwa mama, baba mkwe na dada wa mume kuja hapo kwao na wanakaa hadi usiku. Faragha yao ni usiku na hana uhuru na mumewe. Mbaya zaidi hawawezi kununua kitu chochote cha ndani mfano redio bila kuwashirikisha wakwe japo malipo wanalipa wao. Au hawawezi kwenda hata outing au safari over the weekend bila ruhusa ya wazazi wa mume.
Mwanzoni alivumilia sana ila siku zinavyozidi anakosa raha na mumewe keshaongea nae yeye anasema haoni tatizo la nduguze.
Je hii ni kawaida? Kwa nini wakwe wanataka kujua kila linaloendelea kwa wawili hawa? Afanyeje ili walau awe na muda wa kutosha na mumewe bila kuhofia wakwe kuwakuta?
Binafsi nimemshauri wahamie mbali au ajaribu kuongea na mdhamini wao wa ndoa au hata mchungaji wao kwa ushauri zaidi, yeye anaogopa maana anahofia wakwe kumchukia.
Naomba mawazo yenu ili nimuokoe rafiki yangu, muda wote huwa mnyonge akifikiria ndoa yake.
Thanx in advance