Tangu juzi tumeona Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali ikiwaleta Wakuu wa Mikoa kueleza kilichofanyika katika mikoa yao katika kipindi cha miaka minne ya uongozi uliopo madarakani.
Ni wazi kuwa katika kila mafanikio changamoto hazikosekani. Sasa mimi hupenda kufuatilia mawasilisho hayo, lakini ajabu hakuna anayeeleza mapungufu yaliyopo. Kweli Mkuu anaposema kila kitu kipo sawa na maisha ni mazuri, aaah...hajatutendea haki.
Ni wazi mafanikio ni mengi na mazuri yamefanywa na serikali yetu. Lakini hii haijawanyima fursa ya kusema wapi tumekwama na wapi tunapungukiwa ili parekebishwe.
Nachelea kila Mkuu akija akasema mambo yote kwake ni safi, sasa tunaenda kuuza sera gani kwa uchaguzi ujao?
Labda mi ndiye mjinga sielewi kinachoendelea!
Ni wazi kuwa katika kila mafanikio changamoto hazikosekani. Sasa mimi hupenda kufuatilia mawasilisho hayo, lakini ajabu hakuna anayeeleza mapungufu yaliyopo. Kweli Mkuu anaposema kila kitu kipo sawa na maisha ni mazuri, aaah...hajatutendea haki.
Ni wazi mafanikio ni mengi na mazuri yamefanywa na serikali yetu. Lakini hii haijawanyima fursa ya kusema wapi tumekwama na wapi tunapungukiwa ili parekebishwe.
Nachelea kila Mkuu akija akasema mambo yote kwake ni safi, sasa tunaenda kuuza sera gani kwa uchaguzi ujao?
Labda mi ndiye mjinga sielewi kinachoendelea!