Habari wakuu
Nina Dada yangu anasumbuliwa na vidonda vya tumbo ,huwa tumbo linamuuma mpaka namuonea huruma ,analia kama mtoto mdogo ,anasema anahisi tumbo linawaka moto hatarii ..!
Kwa anayejua dawa wakuu ni nini, kupunguza maumivu au tiba take kabisa msaada tafadhari.
Mambo, mi nlikua nazo nilikua nalia kama dada yako... sijui zake zipo stage gan coz i hear kuna wanaotapika damu so at first nlikua nakunywa maziwa mixed na asali na kiini cha yai zinapoa in 10mins hvi... ila nikaona attacks zinazidi so nikamtafuta Rahab wa Fiterawa, honestly sijui kama ni dawa au ni vyakula that helped ila nimepona japo dawa sikumaliza but i was strict na yale masharti.... matatizo mengi ya vidonda ni acid inakua imezidi sana mwilini so inabidi detox ya mwili ifanyike.
Niliacha: wali, nazi, jamii zote za kunde, maziwa, mayai, nyama nyekundu, nyanya, pilipili, ndimu, mchcha, kisamvu, mboga zote zenye kijani kibichi,ndizi aina zote, chips,mihogo au chapati, karanga, korosho,maembe, nanasi, chungwa, passion, matunda yenye acid na mbegu nyingi kama mapera, no alcohol, no vinywaji vya baridi, hamna soda wala juice za matunda yaliyokatazwa, mtindi, uji wa ulezi, majani ya chai, kahawa, chumvi nyingi na magadi, usitumie dawa zenye acid, sulphur wala caffeine no sigara.
VINAVYOFAA:
Asubuhi:
Chai ya Soya au
Mchaichai
VITAFUNWA
mkate, andazi au vitumbua- atafune sana kabla ya kumeza
Mchana/Jioni
Ugali laini, viazi mviringo vya kuchemsha au tambi
Mboga
Kbichi, bamia, nyama nyeupe ila no dagaa
Carrot, vitunguu maji na saumu, hoho,
Matunda: tango, papai, tikiti na parachichi
Vinywaji: maji na juisi za matunda tajwa hapo juu
Asikae na njaa muda mrefu, ale kwa wakti na atafune vizuri aache stress...
Nimetype mpaka vidole vinauma. All the best kwake... kwa maswali pia nipo. Mpe pole hayo maumivu nayajua jamani