Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,420
- 40,405
Leo katika tafakari yangu na tathmini; nimegundua nina watoto nane, na wanaotambulika na mama zao kuwapa jina langu ni sita, wakike 3, na wa kiume 3; wa nje ya ndoa 3 mama tofauti.
Changamoto iliyopo kwa sasa ni namna ya kuwahudumia bila nyumba kubwa kuwafahamu; ingawa huwa nawatumia ada na vihela kidogo pale ninapokuwa navyo; kwa sasa wako chekechea (wa nje).
Kinachoniumiza kichwa kwa sasa, ni mama zao kuendelea kuniita 'mume wangu' na kunilazimisha tuendeleze mahusiano ya mapenzi; huku wakijua nina familia.
Wengine wanapiga simu usiku wa manane; mpaka nikatafuta laini nyingine ambayo awaijui na kuiweka usiku.
Wakuu, nitumie njia gani ili nisiwe nao kimapenzi na wao wanielewe, ila nibaki kuhudumia watoto tu?
Kwa sababu nikiendelea kuwa nao karibu kimahusiano; ni sawa na gari dogo kuendeshwa na madereva sita; nitazeeka mapema.
Changamoto iliyopo kwa sasa ni namna ya kuwahudumia bila nyumba kubwa kuwafahamu; ingawa huwa nawatumia ada na vihela kidogo pale ninapokuwa navyo; kwa sasa wako chekechea (wa nje).
Kinachoniumiza kichwa kwa sasa, ni mama zao kuendelea kuniita 'mume wangu' na kunilazimisha tuendeleze mahusiano ya mapenzi; huku wakijua nina familia.
Wengine wanapiga simu usiku wa manane; mpaka nikatafuta laini nyingine ambayo awaijui na kuiweka usiku.
Wakuu, nitumie njia gani ili nisiwe nao kimapenzi na wao wanielewe, ila nibaki kuhudumia watoto tu?
Kwa sababu nikiendelea kuwa nao karibu kimahusiano; ni sawa na gari dogo kuendeshwa na madereva sita; nitazeeka mapema.