Wakuu kwa dar wapi ntapata suti nzuri za harusi?

Wakuu kwa dar wapi ntapata suti nzuri za harusi?

Japo sijajua uko wapi lakini suti unapata nzuri,pia kuna mafundi wazuri sana wanashona mpaka za dukani hazioni ndani. Lakini fuata ushauri mzuri ili kufanikisha azma yako, achana na watoa mapovu!

Mafundi michosho tu wanashona vizuri lkn kero tupu unafuatilia utafikiri unashona bure.Wanakera sana mafundi
 
designer kweli au copy ya mchina...nshawai kununua nguo pale haikuchukua muda ikaanza kutoa uzi...
Sijui kwa nini Tz hakuna vitu quality...akati nchi za wenzetu kuna suti za bei poa na bado quality ya juu..sie masikini afu vitu feki na bei juu...

kuna duka unaingia unaangalia nguo zote malonya lonya afu bei unapangusa macho kama umesoma vizuri au umekosea...

Nadhani kwa wafanya biashara bado kuna fursa kwenye suala la nguo...leteni nguo quality na affordable...hata mkivizia sale za nje poa...


Mariedo jengo la Mkapa posta kuna designers suits ila bei jipange kweli kweli
 
Mkuu Kikwaka kwanza nakupongeza kama unaenda funga ndoa.
Kwa bei hyo ya 300k-400k pale Brand unapata bt hazina tofauti sana na za kariakoo coz hata mimi nilinunua pale Brand house posta mpya niliporudi kariako nikakuta kwenye duka moja lipo Agrey na Uhuru adjasent to Megido Pharmacy kuna aina nyingi sana ambazo hazina tofauti na zile za brand hse, na nililazimika kununua suti ya pili hapo duka la kko coz niliipenda zaid na ilikua na quality na material sawa na ile niliyonunua brand hse na ndo niliyoivaa hyo ya kko kwenye harus yangu,
so nakushaur fanya kutembelea hzi sehemu then lazma utakuja na conclusion ya unachokitaka
 
nilinunua pale ... Agrey na Uhuru adjasent to Megido Pharmacy a

Jiografia na mahesabu vinagongana hapa, kwa ufahamu wangu hii mitaa iko "parallel haikutani kamwe mfano wa mitaa inayokutana na uliyotaja ni km Km Msimbazi, Kongo, Sikukuu n.k
 
Back
Top Bottom