Wakulima Jiandaeni Kisaikolojia na Kuporomoka Kwa Bei ya Mahindi Mwaka huu 2023, Kenya Gunia la Mahindi Imeshuka hadi Tsh. 80,000

The Sunk Cost Fallacy 2

JF-Expert Member
Nov 8, 2022
7,382
8,437
Habari ndugu wakulima wenzangu.

Leo natoa taarifa tuu ya Hadhara kwamba mjiandae kisaikolojia maana bei ya Mahindi itaenda kushuka sana.

Kenya ambayo ndio soko kuu la Mahindi ya Tanzania bei imeshuka kutoka Tsh 130,000 Kwa gunia la kilo 100 Hadi Tsh.80,000.Ikumbukwe Kenya ndio soko kuu la Mahindi ya Tanzania..

Hii imetokana na sera ya Ruto ya kuingiza mahindi ya GMO kutoka Nje ya Nchi tena bila ushuru wowote.

Aidha Msimu huu mvua zimekubali maeneo mengi ya Nchi plus mbolea ya ruzuku so mazao yatakuwa mengi sana na hivyo yatakutana na hali mbaya ya bei.

Ambae anauwezo ni kuandaa stoo vinginevyo msimu wa mavuno usije shangaa gunia kuuzwa 30,000 na wateja hakuna,maana wafanyabiashara wengi watakimbilia kwenye mchele/mpunga ambao naona bei zitashuka ila Kwa kiasi kidogo.

Nitoe wito Kwa serikali Kupitia bodi ya mazao Mchanganyiko PBZ na wakala wa Hifadhi wa Chakula NFRA chini ya Wizara ya Kilimo kutenga Bajeti ya kutosha Ili kuja kununua mazao Kwa mkulima Ili Kuokoa uzalishaji msimu utakaofuata maana mfanyabiashara hawezi nunua wakati hakuna soko.

Pia Serikali iangalie uwezekano wa kutafuta Soko Ethiopia,Sudan Kusini na Somalia Moja kwa Moja badala ya kutegemea Kenya pekee.

 
Swali la kujiuliza kwanini yameshuka ?

Tatizo la hii nchi tunakwenda kwa matukio na bahati mbaya we are always one step behind kwahio kila tukifanya kitu tunajikuta tumechelewa...... Ndio maana majuzi nikauliza....

 
Napia nafaka za Maharage nazo zimeshuka sana kwa upande wa Kenya Bei sawa na Tsh @kg

Maharage @kg Tsh 2,900-3,200

Choroko @kg Tsh 2,100-2,400

Wakati huku Tanzania Bei ziko juu hatari Yan tafsiri yake unaeza enda nunua maharage Kenya ukaja kuuza Tanzania aisee shilingi ya Kenya soon inaimarika dhidi ya Tsh
 
Swali la kujiuliza kwanini yameshuka ?

Tatizo la hii nchi tunakwenda kwa matukio na bahati mbaya we are always one step behind kwahio kila tukifanya kitu tunajikuta tumechelewa Ndio maana majuzi nikauliza.

Kwani hujasoma sababu za kushuka? Biashara huwenda Kwa matukio na msimu na hasa kwenye Kilimo..

Ndio maana nakubaliana na sera ya serikali ya kutoingilia bei ya soko,wao wapambane kutafuta masoko mapya na pia kuongeza thamani mazao.

Mfano Bodi ya Mazao Mchanganyiko Ina kiwanda pale Dodoma wanasaga unga wa nafaka mbalimbali na kuzi pack hivyo wanauza mazao yalioogezwa thamani.

Sasa Ili kujihakikishia soko tunatakiwa kukuza viwanda vya hivi na pia kukuza sekta ya ufugaji iwe ya Kisasa na kutoa soko kwenye mazao ya Kilimo.
 
Kwani hujasoma sababu za kushuka? Biashara huwenda Kwa matukio na msimu na hasa kwenye Kilimo..

Ndio maana nakubaliana na sera ya serikali ya kutoingilia bei ya soko,wao wapambane kutafuta masoko mapya na pia kuongeza thamani mazao.

Mfano Bodi ya Mazao Mchanganyiko Ina kiwanda pale Dodoma wanasaga unga wa nafaka mbalimbali na kuzi pack hivyo wanauza mazao yalioogezwa thamani.

Sasa Ili kujihakikishia soko tunatakiwa kukuza viwanda vya hivi na pia kukuza sekta ya ufugaji iwe ya Kisasa na kutoa soko kwenye mazao ya Kilimo.
Kenya bei imeshuka sasa hivi baada ya mizigo ya imported duty free cereals kuingia sokoni na hilo wala sio ajabu na lilikuwa la kutegemea (yaani hakuna cha ajabu kitakachotokea ambacho hakiwezi kuwa planned beforehand); Kwahio with plans wala huu mfumuko wa bei wa sasa usingetokea na wala hicho unachosema wakulima kukosa soko miaka inayokuja ingawa itatokea lakini wizara ingefanya kazi yake wala kungekuwa hakuna uwezekano wa kutokea.... Lakini sababu tunakwenda kwa reactiveness na sio kuwa pro-active tegemea mazao ya wakulima kuozea shambani.... Na wasiasa kupiga siasa wakati huku wengine wanasifia sera with nothing to show for it....
 
Acha upuuzi,uruhusu mchele wa Nje Ili kumkomoa nani na kumdaidia nani?
Sio wewe uliyeongelea soko huria hapo juu ? Haya mambo mtu inabidi kuyaangalia kwa ujumla wake na sio kwa mafungu inabidi ufanye upembuzi yakinifu na weigh out pros and cons...., na wakati unafanya hivyo ugundue kwamba chakula ni basic need na wakati wote bei lazima iwe rafiki..., na bila kusahau wakati unafikiri hayo kumbuka Ushauri wa Adam Smith....

It is the maxim of every prudent master of a family, never to attempt to make at home what it will cost him more to make than to buy.”
 
bAada ya mwez wa kwanza mahindi kushuka huku kwetu mwanza,mwez huu wa pili yamepanda tena kwa speed ya 5G

Nasema hivi huo ni uongo gharama za chakula zitaendelea kupaa tu
 
Habari ndugu wakulima wenzangu..

Leo natoa taarifa tuu ya Hadhara kwamba mjiandae kisaikolojia maana bei ya Mahindi itaenda kushuka sana.

Kenya ambayo ndio soko kuu la Mahindi ya Tanzania bei imeshuka kutoka Tsh 130,000 Kwa gunia la kilo 100 Hadi Tsh.80,000.Ikumbukwe Kenya ndio soko kuu la Mahindi ya Tanzania..

Hii imetokana na sera ya Ruto ya kuingiza mahindi ya GMO kutoka Nje ya Nchi tena bila ushuru wowote.

Aidha Msimu huu mvua zimekubali maeneo mengi ya Nchi plus mbolea ya ruzuku so mazao yatakuwa mengi sana na hivyo yatakutana na hali mbaya ya bei.

Ambae anauwezo ni kuandaa stoo vinginevyo msimu wa mavuno usije shangaa gunia kuuzwa 30,000 na wateja hakuna,maana wafanyabiashara wengi watakimbilia kwenye mchele/mpunga ambao naona bei zitashuka ila Kwa kiasi kidogo.

Nitoe wito Kwa serikali Kupitia bodi ya mazao Mchanganyiko PBZ na wakala wa Hifadhi wa Chakula NFRA chini ya Wizara ya Kilimo kutenga Bajeti ya kutosha Ili kuja kununua mazao Kwa mkulima Ili Kuokoa uzalishaji msimu utakaofuata maana mfanyabiashara hawezi nunua wakati hakuna soko.

Pia Serikali iangalie uwezekano wa kutafuta Soko Ethiopia,Sudan Kusini na Somalia Moja kwa Moja badala ya kutegemea Kenya pekee.

Kamwe ubaya hauwez dumu, soon we will breath fresh air
 
Back
Top Bottom