kinepi_nepi
JF-Expert Member
- Aug 16, 2007
- 869
- 239
• ASEMA KUHOJI KADI YA DK. SLAA NI KUJIDHALILISHA
WAKILI maarufu wa kujitegemea jijini Arusha, Method Kimomogoro, amesema hoja ya Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nauye kuhusu uhalali wa Dk. Willibrod Slaa kumiliki kadi ya CCM ni ya kijinga na yenye nia ya kujidhalilisha mwenyewe.
Kimomogoro ambaye pia ni wakili wa baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA katika kesi mbalimbali za kisiasa zinazowakabili kwenye mahakama za jijini humo, alisema kuwa amelazimika kutoa ufafanuzi wa kisheria ili kufuta ujinga unaoenezwa.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, wakili huyo alisema kuwa wote wanaoungana na Nape, kueneza hoja hiyo ni wajinga kwa vile kadi ya chama ni mali ya mwanachama tofauti na zilivyo kadi nyingine za taasisi kama benki ambapo ni mali ya benki.
Ufafanuzi huo wa kisheria unakuja siku chache tangu, Nape aibue hoja hiyo akiwa ziarani jijini Mwanza ambako alidai kuwa Katibu Mkuu huyo wa CHADEMA, ni miongoni mwa viongozi wa upinzani wanaoendelea kumiliki kadi za CCM na kulipia ada licha ya kuhama.
Hata hivyo, Dk. Slaa alijibu hoja hiyo na kumtaka Nape aache kupiga mayowe badala yake awaeleze wananchi serikali ya chama chake imefanya nini kuwaondolea umaskini unaowakabili.
Pia alikiri kuwa na kadi hiyo, lakini akakanusha kuilipia ada, akisema ni kinyume kwa mujibu wa sheria mtu kuwa mwanachama wa vyama viwili, kwamba ameihifadhi kama mali yake ili iwe kumbukumbu kwa wajukuu zake.
Licha ya ufafanuzi huo, Nape bado ameendelea kueneza propaganda hiyo, huku akitambua wazi kuwa sharti mojawapo la Katiba ya CCM linabainisha kuwa uanachama wa mtu unakoma endapo atahamia chama kingine cha siasa.
Ni katika upotoshaji huo, wakili Kimomogoro alijitokeza kutoa ufafanuzi wa kisheria akisema, kadi ya CCM na hata vyama vingine ni mali ya mwanachama, hivyo anapohama anaweza kuipeleka popote atakapo na hata kuichoma moto akitaka.
"Wanaoibua hoja hii ni wajinga, tena inasikitisha sana kuona kiongozi na msemaji wa chama kama Nape ndiye anaibua ujinga huu, kama haelewi taratibu za chama chake alipaswa kufanya utafiti kwanza," alisema.
Kimomogoro alisema kuwa, kadi ya chama ni sawa na cheti cha kuzaliwa au cha ndoa, kwamba mtu anapokufa au ndoa yake kuvunjika hakuna anapoulizwa ama kutakiwa kurejesha vyeti hivyo maana ni mali yake.
"Kama wakina Nape wanataka Dk. Slaa na wengine walioondoka CCM wawarejeshee kadi zao, basi wabadili katiba yao na kuliweka kisheria kama ilivyo kwa kadi za mabenki ambazo huwa mali za benki husika," alisema.
Wakili huyo aliongeza kuwa, anachofanya Nape ni maajabu na hivyo wako watakaomtaka awaeleze kadi za CCM za hayati Mwalimu Julius Nyerere na viongozi wengine waliofariki zimerejeshwa kwa nani kama ni mali ya chama.
Alisema kuwa, Nape anatakiwa kujikita kwenye mambo ya msingi ya kuendeleza chama chake na serikali wanayoiongoza, badala ya kuibua hoja za kijinga zisizo na tija kwa wananchi.
WAKILI maarufu wa kujitegemea jijini Arusha, Method Kimomogoro, amesema hoja ya Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nauye kuhusu uhalali wa Dk. Willibrod Slaa kumiliki kadi ya CCM ni ya kijinga na yenye nia ya kujidhalilisha mwenyewe.
Kimomogoro ambaye pia ni wakili wa baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA katika kesi mbalimbali za kisiasa zinazowakabili kwenye mahakama za jijini humo, alisema kuwa amelazimika kutoa ufafanuzi wa kisheria ili kufuta ujinga unaoenezwa.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, wakili huyo alisema kuwa wote wanaoungana na Nape, kueneza hoja hiyo ni wajinga kwa vile kadi ya chama ni mali ya mwanachama tofauti na zilivyo kadi nyingine za taasisi kama benki ambapo ni mali ya benki.
Ufafanuzi huo wa kisheria unakuja siku chache tangu, Nape aibue hoja hiyo akiwa ziarani jijini Mwanza ambako alidai kuwa Katibu Mkuu huyo wa CHADEMA, ni miongoni mwa viongozi wa upinzani wanaoendelea kumiliki kadi za CCM na kulipia ada licha ya kuhama.
Hata hivyo, Dk. Slaa alijibu hoja hiyo na kumtaka Nape aache kupiga mayowe badala yake awaeleze wananchi serikali ya chama chake imefanya nini kuwaondolea umaskini unaowakabili.
Pia alikiri kuwa na kadi hiyo, lakini akakanusha kuilipia ada, akisema ni kinyume kwa mujibu wa sheria mtu kuwa mwanachama wa vyama viwili, kwamba ameihifadhi kama mali yake ili iwe kumbukumbu kwa wajukuu zake.
Licha ya ufafanuzi huo, Nape bado ameendelea kueneza propaganda hiyo, huku akitambua wazi kuwa sharti mojawapo la Katiba ya CCM linabainisha kuwa uanachama wa mtu unakoma endapo atahamia chama kingine cha siasa.
Ni katika upotoshaji huo, wakili Kimomogoro alijitokeza kutoa ufafanuzi wa kisheria akisema, kadi ya CCM na hata vyama vingine ni mali ya mwanachama, hivyo anapohama anaweza kuipeleka popote atakapo na hata kuichoma moto akitaka.
"Wanaoibua hoja hii ni wajinga, tena inasikitisha sana kuona kiongozi na msemaji wa chama kama Nape ndiye anaibua ujinga huu, kama haelewi taratibu za chama chake alipaswa kufanya utafiti kwanza," alisema.
Kimomogoro alisema kuwa, kadi ya chama ni sawa na cheti cha kuzaliwa au cha ndoa, kwamba mtu anapokufa au ndoa yake kuvunjika hakuna anapoulizwa ama kutakiwa kurejesha vyeti hivyo maana ni mali yake.
"Kama wakina Nape wanataka Dk. Slaa na wengine walioondoka CCM wawarejeshee kadi zao, basi wabadili katiba yao na kuliweka kisheria kama ilivyo kwa kadi za mabenki ambazo huwa mali za benki husika," alisema.
Wakili huyo aliongeza kuwa, anachofanya Nape ni maajabu na hivyo wako watakaomtaka awaeleze kadi za CCM za hayati Mwalimu Julius Nyerere na viongozi wengine waliofariki zimerejeshwa kwa nani kama ni mali ya chama.
Alisema kuwa, Nape anatakiwa kujikita kwenye mambo ya msingi ya kuendeleza chama chake na serikali wanayoiongoza, badala ya kuibua hoja za kijinga zisizo na tija kwa wananchi.