Wakili Kimomogoro amuelimisha Nape

Wakili Kimomogoro amuelimisha Nape

Ujinga wa mtoa hoja na muenezaji unatofautiana.

unafikiri nani mjinga zaidi, aliyeitoa au aliyeichukua kama ilivyo na kuipigia debe?

Ujinga uliotopea zaidi kupingana na ukweli
 
Ritz unaheshimika kwa hoja propaganda zinakupeleka kwingine kwa kujiingiza kundi la wajinga. Kwani wewe hujui kadi yako ya CCM ni mali yako haiwahusu Lumumba wala Chadema. Kama hujui huo ni ujinga.

Kadi ni mali ya chama na ndio sababu chama husika kinaweza kukulazimisha urejeshe kadi yao!
 
Mkuu Ritz
Wakili voda faster; ulimshamsikia kwenye kesi yoyote ya maana?
 
Last edited by a moderator:
Jamani hili mpaka leo bado tunalo tu humu?Tuachane nalo kwani halitusaidii.
 
Nape hana hoja za kijinga tu bali za kipumbavuuu. Mbona yeye ana kadi ya chama chake cha jamii na hakuna anayemgusa? Kweli nyani haoni kundule na wanaomuunga mkono nadhani ni wale wale wenye mawazo mgando kama yeye.

Kama hoja ingekuwa ya kipumbavu babu angenyamaza kimya; lakini mpaka kainua mdomo na kuijibu jua fika haikuwa ya kipumbavu
 
Awaeleze kadi za CCM za hayati Mwalimu Julius Nyerere na viongozi wengine waliofariki zimerejeshwa kwa nani kama ni mali ya chama.

Hili nalo neno!
 
acheni kumwonea Nape hoja ya kuwa Dr Slaa anamiliki kadi ya Ccm ipo hapa jamvini tangu mwezi wa tisa na mwazilushi wa hii hoja ni mimi Makupa

Najua ukiacha boss wako ashambuliwe hautapata mshahar wa mwezi huu.
Mpiganie mwanaume mwenzako ili uweze kula.
 
Wala msipoteze muda wenu kumjadili yule jamaa. Atakupotezeeni muda wenu bure!
 
Kadi ni mali ya chama na ndio sababu chama husika kinaweza kukulazimisha urejeshe kadi yao!

Hujui hata katiba ya chama chako. Ebu lete kifungu cha katiba yenu kinachosemqa Kadi ni mali ya chama.
 
Masikini mtoto wa kinyaturu mlenda ulimuathiri tangu utotoni,mbuna hajahoji ccm walimfanyia nini baba yake?anafikiri ccm wazuri?wangemjengea baba yake kijijini kwenu singida
 
je hakuna mtu ambaye hafahamu kama dr alikuwa ccm hapo kale?

Je alipo kuwa ccm alikuwa kama nani?

Je kama alikuwa mwanachama nini kilikuwa kinamtambulisha uwanachama wake?

Kumbe ni lazima kikatiba unapotoka kwenye chama kimoja kwenda kingine inakubidi urudishe kadi?

Mwisho kama nape anasema dr bado analipia kadi hiyo na fikiri kuna ushahidi tosha wa risiti za malipo hivyo atuletee copy ili tujue kati ya yeye na dr nani ndio muongo


la msingi hapa tuna lazimika kuwajulisha kina nape kuwa tanzania hatuhitaji kujua nani ana kadi sisi tunahitaji uwajibikaji kwenye mambo ya msingi, watu hawasomi, watu wana kufa kwa njaa, hakuna ajira, hakuna uwezeshaji mahiri wa kujiajiri nk. Haya ndio mambo ya kuangalia na kutujulisha watanganyika si sera za umiliki wa kadi.

kwa upeo wangu nafahamu kuwa hakuna jambo jema kama kutunza kumbukumbu hasa zile ambazo baadae zinaweza kukusaidiakatika kuleta uhakika wa hoja au jambo lolote linalohitaji uthibitisho, kubaki na na kadi kama kuwa kumbukumbu sio maana yake kuwa mwanachama hai, wangapi wana kadi za tanu na a.s.p? Je bado ni wanachama hai? Mchungaji mtikila anabendera ya tanganyika je na yeye tumsemeje?
 
CCm wana mambo ya kijinga sana. Agenda ya kadi ya ccm na Dr Slaa imefungwa. Sasa tafuteni kashfa nyingine tena. Na the more mnavyoibue na hoja pumba zenu, mnampa nafasi ya ku clarify Dr na kuonekana yuko mbali sana na ninyi ki maarifa na kibali. Pole NApe. Kazi kwako.
 
acheni kumwonea Nape hoja ya kuwa Dr Slaa anamiliki kadi ya Ccm ipo hapa jamvini tangu mwezi wa tisa na mwazilushi wa hii hoja ni mimi Makupa

So you are proud of being the author of the so called stupid motion here?
 
Kwa hiyo NAPE Mkeo akipika na Kupakuwa kwa mume mwingine ATABAKI Kuwa MKEO Eti kwakuwa Hajarudisha CHETI CHA NDOA!
 
Ukiona watu wanahangaika na mambo madogo madogo wanaacha makubwa ujue wana tatizo kubwa zaidi ya ujinga. Nape hayupo sawasawa kichwani. Kwa cheo alicho nacho ndani ya chama tawala hakustahili hata kufikiria kuongelea hoja za kipumbavu kiasi hicho achilia mbali kwenda kusimama mbele ya watu na kuzitamka. Unapokuwa na watu wa mawazo na reasoning kama hii ya Nape halafu ndiyo watu waliokabidhiwa kuongoza nchi inakatisha tamaa kabisa.

Mimi nina kadi mbili za CCM, zote nilipewa wakati nikitumikia JKT, bila ya hiari yangu. Kule jeshini walikuwa wanakata hela yako ya posho kisha wanakupa kadi ya CCM. Walikata pesa yangu nikiwa JKT Masange, nilipoenda Buhemba wakakata hela yangu tena kwa mara ya pili. Wakati nikiwa nimepewa kule Buhemba nikaletewa na nyingine kutoka Masange. Kwa sababu kwangu makaratasi hayo hayakuwa chochote zaidi ya kuwa njia ya kuiba hela yangu, sikuwa kulipia hata mwaka mmoja. Ninayo kama kumbukumbu ya udhalimu. Je, CCM mnaniona kuwa ni mwanachama wenu kwa sababu ya yale magamba niliyopewa?

Mtatunga hadithi nyingi kama ni ukumbusho yeye Slaa mbona hakuwaachia wengine nao wakae na ukumbusho?
 
acheni kumwonea Nape hoja ya kuwa Dr Slaa anamiliki kadi ya Ccm ipo hapa jamvini tangu mwezi wa tisa na mwazilushi wa hii hoja ni mimi Makupa
Kama unashindwa kuelewa maelezo ya kisheria, umeamua kuutetea UJINGA na UNAPE, yetu macho
 
Ni kweli Makupa, huyu wakili anatakiwa akutafute wewe uliofichua hii kitu sio Nape...huyu wakili ndio mjinga anataka kupingana na ukweli.
Mh Ritz nakuheshimu sana, lakini kupinga maelezo ya kisheria na kumwita "huyu wakili ndio mjinga" naanza kutilia wasiwasi umakini wako. Hoja ya kisheria haipingwi na propaganda, tuonyeshe ni kifungu gani cha katiba ya CCM kinachotamka kurudisha kadi?
 
acheni kumwonea Nape hoja ya kuwa Dr Slaa anamiliki kadi ya Ccm ipo hapa jamvini tangu mwezi wa tisa na mwazilushi wa hii hoja ni mimi Makupa
Kweli mheshimiwa ulianzisha, lakini Nape kudandia hoja bila ya kufanya uchunguzi wa kikatiba ni UJINGA. Nape ni kiongozi mkubwa ndani ya CCM na mwenye elimu kubwa, lazima awe makini na hoja anazodandia. Nape na CCM ni adui wa maendeleo
 
Back
Top Bottom