Kadi ni mali yetu na aturudishie
Mtatunga hadithi nyingi kama ni ukumbusho yeye Slaa mbona hakuwaachia wengine nao wakae na ukumbusho?
Ujinga uliotopea zaidi kupingana na ukweli
Kadi ni mali ya chama na ndio sababu chama husika kinaweza kukulazimisha urejeshe kadi yao!
Ulishamsikia wapi Dr analazimisha watu kurudisha kadi za ccm?? kama sio ushabiki wako wa kijinga, watu wenyewe wanaamua kuzikabidhi. Na tena ukichunguza kadi nyingi zinazorejeshwa ni zile zilizotolewa wakati wa Makamba, Nape, Mangula, et al. Lakini zile zilizotolewa wakati wa Nyerere watu wanazitunza kwaajili ya kumuenzi Mzee wetu. KEEP IT ON MINDWakili na yeye hamna kitu naye ni mjinga na ujinga unatofautiana,hebu tofautisha sheria na siasa.Anachosema Nape ile ni SIASA haiwezekani yeye Dr. apokee kadi za wengine wanaotoka CCM na hata hawaambii kwamba hizo ni mali zao hivyo wasirudishe sasa cha kushangaza mbona hawaambii.Huu nao ni upuuzi wa mwanasheria huyu anashindwa kutofautisha Siasa na Sheria.Tungekubali hoja yake endapo kama ipo kauli ya Dr. Slaa ya kuwaeleza wanaorudisha kadi za CCM waendelee kukaa nazo kwa vile ni mali yao.Huku ni kujidhalilisha kwa mwanataaluma.Anachofanya Nape ni kupiga Siasa ambapo kikawaida mtu anayehama chama anarusha kadi ukisema walikokufa warudishe sasa ye aliona wapi maiti inarudi?Hao waliokufa wamekufa wakiwa na itikadi hiyo tofauti na Dr.
Kadi ni mali yetu na aturudishie
acheni kumwonea Nape hoja ya kuwa Dr Slaa anamiliki kadi ya Ccm ipo hapa jamvini tangu mwezi wa tisa na mwazilushi wa hii hoja ni mimi Makupa
acheni kumwonea Nape hoja ya kuwa Dr Slaa anamiliki kadi ya Ccm ipo hapa jamvini tangu mwezi wa tisa na mwazilushi wa hii hoja ni mimi Makupa
Na pia hakuwalazimisha kuzirudisha ili zichomwe moto, ni watu tu na mapenzi yao waliamua kuzichoma moto. Na ukichunguza kadi nyingi zinazorudishwa na kuchomwa moto ni hizi zilizotoka kipindi cha mafisadi, nyingi zimesainiwa na mafisadi, wakati zile za wakati wa Nyerere watu wengi wanazihifadhi kwa kumbukumbu ya uadilifu wake na wala sio kwa mapenzi yao kwa ccm ya sasa hivi.
Hairudishi sasa mpelekeni mahakamani, au kampigeni na kitu kizito chenye ncha kali
Hakuna aliyepingana na ukweli. Dr amekiri kumiliki kadi na wala sio kuwa mwanachama wa gambaz. Kadi ya Dr ni miongoni mwa zile zilizotoka enzi zile chama kikimilikiwa na wakulima na wafanyakazi. Sio sasa hivi ambapo chama kimeshikiliwa na mijangili. Hata mimi ningekuwa na kadi ya enzi zile nisingeirudisha kamwe, lakini hizi za kina Nape ningeichoma bila kupepesa macho.
Haya ndiyo mapenzi yenyewe aliyonayo kwenu, mnahaha kujaribu kutumia vyombo vya dola kumhujumu Slaa na CDMYeye na akae nayo tunajua bado ana mapenzi na sisi
Je hakuna mtu ambaye hafahamu kama Dr alikuwa ccm hapo kale?
Je alipo kuwa ccm alikuwa kama nani?
Je kama alikuwa mwanachama nini kilikuwa kinamtambulisha uwanachama wake?
Kumbe ni lazima kikatiba unapotoka kwenye chama kimoja kwenda kingine inakubidi urudishe kadi?
Mwisho kama Nape anasema Dr bado analipia kadi hiyo na fikiri kuna ushahidi tosha wa risiti za malipo hivyo atuletee copy ili tujue kati ya yeye na Dr nani ndio muongo
La msingi hapa tuna lazimika kuwajulisha kina Nape kuwa Tanzania hatuhitaji kujua nani ana kadi sisi tunahitaji uwajibikaji kwenye mambo ya msingi, watu hawasomi, watu wana kufa kwa njaa, hakuna ajira, hakuna uwezeshaji mahiri wa kujiajiri nk. Haya ndio mambo ya kuangalia na kutujulisha watanganyika si sera za umiliki wa kadi.
ASEMA KUHOJI KADI YA DK. SLAA NI KUJIDHALILISHA
WAKILI maarufu wa kujitegemea jijini Arusha, Method Kimomogoro, amesema hoja ya Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nauye kuhusu uhalali wa Dk. Willibrod Slaa kumiliki kadi ya CCM ni ya kijinga na yenye nia ya kujidhalilisha mwenyewe.
Kimomogoro ambaye pia ni wakili wa baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA katika kesi mbalimbali za kisiasa zinazowakabili kwenye mahakama za jijini humo, alisema kuwa amelazimika kutoa ufafanuzi wa kisheria ili kufuta ujinga unaoenezwa.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, wakili huyo alisema kuwa wote wanaoungana na Nape, kueneza hoja hiyo ni wajinga kwa vile kadi ya chama ni mali ya mwanachama tofauti na zilivyo kadi nyingine za taasisi kama benki ambapo ni mali ya benki.
Ufafanuzi huo wa kisheria unakuja siku chache tangu, Nape aibue hoja hiyo akiwa ziarani jijini Mwanza ambako alidai kuwa Katibu Mkuu huyo wa CHADEMA, ni miongoni mwa viongozi wa upinzani wanaoendelea kumiliki kadi za CCM na kulipia ada licha ya kuhama.
Hata hivyo, Dk. Slaa alijibu hoja hiyo na kumtaka Nape aache kupiga mayowe badala yake awaeleze wananchi serikali ya chama chake imefanya nini kuwaondolea umaskini unaowakabili.
Pia alikiri kuwa na kadi hiyo, lakini akakanusha kuilipia ada, akisema ni kinyume kwa mujibu wa sheria mtu kuwa mwanachama wa vyama viwili, kwamba ameihifadhi kama mali yake ili iwe kumbukumbu kwa wajukuu zake.
Licha ya ufafanuzi huo, Nape bado ameendelea kueneza propaganda hiyo, huku akitambua wazi kuwa sharti mojawapo la Katiba ya CCM linabainisha kuwa uanachama wa mtu unakoma endapo atahamia chama kingine cha siasa.
Ni katika upotoshaji huo, wakili Kimomogoro alijitokeza kutoa ufafanuzi wa kisheria akisema, kadi ya CCM na hata vyama vingine ni mali ya mwanachama, hivyo anapohama anaweza kuipeleka popote atakapo na hata kuichoma moto akitaka.
Wanaoibua hoja hii ni wajinga, tena inasikitisha sana kuona kiongozi na msemaji wa chama kama Nape ndiye anaibua ujinga huu, kama haelewi taratibu za chama chake alipaswa kufanya utafiti kwanza, alisema.
Kimomogoro alisema kuwa, kadi ya chama ni sawa na cheti cha kuzaliwa au cha ndoa, kwamba mtu anapokufa au ndoa yake kuvunjika hakuna anapoulizwa ama kutakiwa kurejesha vyeti hivyo maana ni mali yake.
Kama wakina Nape wanataka Dk. Slaa na wengine walioondoka CCM wawarejeshee kadi zao, basi wabadili katiba yao na kuliweka kisheria kama ilivyo kwa kadi za mabenki ambazo huwa mali za benki husika, alisema.
Wakili huyo aliongeza kuwa, anachofanya Nape ni maajabu na hivyo wako watakaomtaka awaeleze kadi za CCM za hayati Mwalimu Julius Nyerere na viongozi wengine waliofariki zimerejeshwa kwa nani kama ni mali ya chama.
Alisema kuwa, Nape anatakiwa kujikita kwenye mambo ya msingi ya kuendeleza chama chake na serikali wanayoiongoza, badala ya kuibua hoja za kijinga zisizo na tija kwa wananchi.