Wakazi wa Ilala kota watimuliwa kama mbwa; damu yaweza kumwagika

domokaya

JF-Expert Member
Apr 22, 2010
3,545
1,719
Wakazi wa Ilaka Kota katika nyumba za NHC wamefukuzwa kama mbwa na kupewa fidia ya shilingi laki tatu baada ya kuwa wapangaji katika nyumba hizo kwa zaidi ya miaka arobaini.

Nyumba hizo ambazo zilijengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini sasa zimeamriwa zivunjwe kupisha maendeleo ya watu wastaarabu na kuwaacha masikini hao raia wa Tanzania wasijue la kufanya.

Wanajamii, wanaharakati na taasisi za kushughulikia haki za binadamu angalieni suala hili kuona kama haki inakiukwa basi ipatikane kwa hawa wananchi masikini ambao walipewa fulana na t-shirt lakini sasa wananyanganywa moja ya hitaji kuu la banadamu ambalo ni malazi.
 
Wakazi wa Ilaka Kota katika nyumba za NHC wamefukuzwa kama mbwa na kupewa fidia ya shilingi laki tatu baada ya kuwa wapangaji katika nyumba hizo kwa zaidi ya miaka arobaini.

Nyumba hizo ambazo zilijengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini sasa zimeamriwa zivunjwe kupisha maendeleo ya watu wastaarabu na kuwaacha masikini hao raia wa Tanzania wasijue la kufanya.

Wanajamii, wanaharakati na taasisi za kushughulikia haki za binadamu angalieni suala hili kuona kama haki inakiukwa basi ipatikane kwa hawa wananchi masikini ambao walipewa fulana na t-shirt lakini sasa wananyanganywa moja ya hitaji kuu la banadamu ambalo ni malazi.

Viongozi wao wa kisiasa wanatoka chama gani katika eneo hilo?
 
Inaonekana wana taarifa ya kutakiwa kuondoka zaidi ya miezi nane sasa
 
Wakazi wa Ilaka Kota katika nyumba za NHC wamefukuzwa kama mbwa na kupewa fidia ya shilingi laki tatu baada ya kuwa wapangaji katika nyumba hizo kwa zaidi ya miaka arobaini.

Nyumba hizo ambazo zilijengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini sasa zimeamriwa zivunjwe kupisha maendeleo ya watu wastaarabu na kuwaacha masikini hao raia wa Tanzania wasijue la kufanya.

Wanajamii, wanaharakati na taasisi za kushughulikia haki za binadamu angalieni suala hili kuona kama haki inakiukwa basi ipatikane kwa hawa wananchi masikini ambao walipewa fulana na t-shirt lakini sasa wananyanganywa moja ya hitaji kuu la banadamu ambalo ni malazi.


Wakoje hao??????????????????
 
Wakazi wa Ilala kota amboa ni wapangaji katika nyumba za Ilala experimental nao wanatarjiwa kufanyiwa kama walivyofanyiwa wenzao wa Dodoma kwa baadhi yao kuonyesha adhma ya kutotaka kuondoka baada ya kuwa wapangaji kwa zaidi ya miaka 41.

Wakazi hao ambao wanaamini sheria za kiupangaji zinawapa haki ya kuwa wamiliki wa nyumba hizo wanatakiwa kuondoka baada ya kulipwa "huruma" ya shilingi laki tatu kwani NHC wanadai hawatakiwi kuwalipa wakazi hao chochote.

Wakazi hao ambao waliomba kuuziwa nyumba hizo mwaka 2002 wameamriwa kuondoka kwa notisi ya siku 30 ambapo notisi hiyo iliandamana na barua ya kujibiwa kuwa ombi lao la kuuziwa nyumba limekataliwa na barua hiyo kurishwa tarehe nyuma na kuonekana iliandikwa mwaka 2003.

Wanasheria haki, wapenda amani, wanaharakati na taasisi za haki za binadamu nawasihi chondechonde tujutokeze kuona haki ikitendeka kwa jamii hii masikini ya watanzania
 
Dah!Wacha tusubiri wanaoifahamu hiyo ishu kwa undani watufahamishe kama taratibu zilifuatwa ama kulikuwa na ukiukwaji!
 
Hivi juzi kulikuwa na zoezi kama hilo Mwanza,Arusha nako likawepo,Dodoma nako na sasa Mchikichini Dsm.Kote huko jeshi na serikali ya magamba wanatumia nguvu.Naamini kwamba licha jeshi na vyanzo vingine vya kulinda amani watumie mbinu nyingine za juu zaidi ya kutumia nguvu.Unakwenda kufukuza watu uko full guns,full bombs,full magari,full polisi wakati unaweza kupita nyumba hadi nyumba na utoe notice ya 24hrs,kweli baada ya muda nenda full greda,magamba sintokulaumu.Lakini wakati mwingine full magamba & full masaburi
 
Hii hali inabidi iendelee ili ifikie hatua watu wanyoke kwenye mstari wa kujitambua kifikira, hii itasaidia tumwagane vinyesi ili tujenge heshima iliyopotea
 
Wapangaji ni wapangaji tuu, mwenye haki ni mwenye nyumba. Sheria yetu ya upangaji ndio sheria bora kuliko zote duniani. Mwenyenyumba akiitaka nyumba yake, kwanza anakupa notice ya miezi mitatu ukae bure, ikipita, anatakiwa akutafutie nyumba ya kodi kama unayolipa mpangaji na yenye hadhi sawa, ndipo akuhamishe. Akikuta nyumba yenye hadhi sawa lakini kodi iko juu, basi mwenyenyumba huyo lazima aitop up hiyo kodi kwa miezi mitatu!.

Wakazi hao wa Ilala ni wapangaji, nyumba sio zao, wamepewa notice ya miaka 8 wakikaa bure!. Wamepewa kodi ya pango ya nyumba za hadhi hiyo kwa miezi mitatu. Wamesaini mkataba wa hiyari wa kuhama, kwa ahadi kuwa wao ndio watapewa preference ya kwanza kuhamia kwenye nyumba mpya zitakazo jengwa hapo.

Kusema ukweli, msiwasikitikie kufukuzwa kama mbwa, kwa sababu mpaka kodi za makazi mapya wamelipiwa!. Kitu cha kuwasikitikia na kuwahurumia ni changa la macho walilosainishwa eti wao ndio watakuwa wapangaji wa mwanzo wa hizo nyumba mpya!. Kama wamekaa bure miaka 8 bila kulipa kodi, hiyo kodi ya pango jipya kila mtu kalipwa kodi ya laki kwa mwezi, hayo majengo mapya, kodi yake itakuwa ni milioni kwa mwezi, hata wakipewa wao hiyo preference, wataweza kulipa?.

Hilo ndilo changa lenyewe la macho, wamesainishwa kama wapangaji na wataendelea kuwa wapangaji only if kama wataweza kulipa. The good deal, walitakiwa wawe wabia katika mradi huo kwa mkataba wa kupatiwa nyumba moja moja kwenye hayo maghorofa mapya, jambo ambalo halikufanyika!.
 
Wakati mwingine ni vizuri kutumia nguvu kuweka heshima. Kama wanakaa hovyo au hawalipi kodi basi wacha watolewe. Maisha lazima ugharamie hata kwa wenzetu wameendelea kwa sababu wanalipia gharama za maisha
 
Wakazi wa Ilaka Kota katika nyumba za NHC wamefukuzwa kama mbwa na kupewa fidia ya shilingi laki tatu baada ya kuwa wapangaji katika nyumba hizo kwa zaidi ya miaka arobaini.

Nyumba hizo ambazo zilijengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini sasa zimeamriwa zivunjwe kupisha maendeleo ya watu wastaarabu na kuwaacha masikini hao raia wa Tanzania wasijue la kufanya.


Wanajamii, wanaharakati na taasisi za kushughulikia haki za binadamu angalieni suala hili kuona kama haki inakiukwa basi ipatikane kwa hawa wananchi masikini ambao walipewa fulana na t-shirt lakini sasa wananyanganywa moja ya hitaji kuu la banadamu ambalo ni malazi.

Lengo la kujengwa hizo nyumba pamoja na zile za magomeni ni ili kuwasaidia watu wa hali ya chini- na tuko wengi wa aina hiyo, sasa nyie miaka yote arobaini mmeng'ang'ania ndani ya hizo nyumba hamtupishi wengine kwa nini? Baadhi mmejenga majumba yenu maeneo mengine na mnapangisha watu kwa bei mbaya lakini hizi mziachii, wacha wabomoe zijengwe zingine za kisasa zitakazobeba watu wengi zaida!!!
 
Wakazi wa Ilaka Kota katika nyumba za NHC wamefukuzwa kama mbwa na kupewa fidia ya shilingi laki tatu baada ya kuwa wapangaji katika nyumba hizo kwa zaidi ya miaka arobaini.

Nyumba hizo ambazo zilijengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini sasa zimeamriwa zivunjwe kupisha maendeleo ya watu wastaarabu na kuwaacha masikini hao raia wa Tanzania wasijue la kufanya.

Wanajamii, wanaharakati na taasisi za kushughulikia haki za binadamu angalieni suala hili kuona kama haki inakiukwa basi ipatikane kwa hawa wananchi masikini ambao walipewa fulana na t-shirt lakini sasa wananyanganywa moja ya hitaji kuu la banadamu ambalo ni malazi.


Hivi ni wao tu ndiyo watanzania maskini wanaostahili kukaa kwenye nyumba za shirika la UMMA kwa zaidi ya miaka 40? Hivi maskini wengine tukifukuzwa kwenye nyumba baada ya kupewa notes tunapewa pia pesa za kupanga nyumba miezi mitatu? Hivi hizo pesa walizopewa wao ni mali ya nani na ni kwa nini ni wao tu wapewe na siyo sisi pia tulio watanzania wenye haki sawa na wao?
 
Inaelekea Watanzania wanaipenda hali ya kuwa wakimbizi ndani ya nchi yao, Ilikua Dodoma hata wiki haijaisha haya yana mwisho haya....!
 
Wapangaji ni wapangaji tuu, mwenye haki ni mwenye nyumba. Sheria yetu ya upangaji ndio sheria bora kuliko zote duniani. Mwenyenyumba akiitaka nyumba yake, kwanza anakupa notice ya miezi mitatu ukae bure, ikipita, anatakiwa akutafutie nyumba ya kodi kama unayolipa mpangaji na yenye hadhi sawa, ndipo akuhamishe. Akikuta nyumba yenye hadhi sawa lakini kodi iko juu, basi mwenyenyumba huyo lazima aitop up hiyo kodi kwa miezi mitatu!.

Wakazi hao wa Ilala ni wapangaji, nyumba sio zao, wamepewa notice ya miaka 8 wakikaa bure!. Wamepewa kodi ya pango ya nyumba za hadhi hiyo kwa miezi mitatu. Wamesaini mkataba wa hiyari wa kuhama, kwa ahadi kuwa wao ndio watapewa preference ya kwanza kuhamia kwenye nyumba mpya zitakazo jengwa hapo.

Kusema ukweli, msiwasikitikie kufukuzwa kama mbwa, kwa sababu mpaka kodi za makazi mapya wamelipiwa!. Kitu cha kuwasikitikia na kuwahurumia ni changa la macho walilosainishwa eti wao ndio watakuwa wapangaji wa mwanzo wa hizo nyumba mpya!. Kama wamekaa bure miaka 8 bila kulipa kodi, hiyo kodi ya pango jipya kila mtu kalipwa kodi ya laki kwa mwezi, hayo majengo mapya, kodi yake itakuwa ni milioni kwa mwezi, hata wakipewa wao hiyo preference, wataweza kulipa?.

Hilo ndilo changa lenyewe la macho, wamesainishwa kama wapangaji na wataendelea kuwa wapangaji only if kama wataweza kulipa. The good deal, walitakiwa wawe wabia katika mradi huo kwa mkataba wa kupatiwa nyumba moja moja kwenye hayo maghorofa mapya, jambo ambalo halikufanyika!.

kuna watu wanafanya mambo ya kijinga kwa sababu wanajua tuna serikali dhaifu, hivi siku hayo magorofa/nyumba zilizochakaa zikiwashukia watasema hayo wanayosema?
na kama hizo nyumba zingekuwa za tajiri mmoja hapa nchi wangelipwa fidia kuhama
tu hache siasa makazi bora ni lazima yajengwe sasa kwa ghalama yoyote
 
Wakazi wa Ilaka Kota katika nyumba za NHC wamefukuzwa kama mbwa na kupewa fidia ya shilingi laki tatu baada ya kuwa wapangaji katika nyumba hizo kwa zaidi ya miaka arobaini.

Nyumba hizo ambazo zilijengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini sasa zimeamriwa zivunjwe kupisha maendeleo ya watu wastaarabu na kuwaacha masikini hao raia wa Tanzania wasijue la kufanya.

Wanajamii, wanaharakati na taasisi za kushughulikia haki za binadamu angalieni suala hili kuona kama haki inakiukwa basi ipatikane kwa hawa wananchi masikini ambao walipewa fulana na t-shirt lakini sasa wananyanganywa moja ya hitaji kuu la banadamu ambalo ni malazi.

Mkuu angalizo kwanza, zile nyumba si za NHC ni za halmashauri ya jiji. Nakumbuka kabla ya mradi huo kuanza wakazi wale walihakikishiwa kupewa priority katika upangaji wa mijengo hiyo mipya (something unrealistic) lakini kulikuwa na modality ya ni namna gani wakazi wale wangekuwa accomodated. Sasa inashangaza kusikia kwamba wamefukuzwa. Lakini hii haiwezi kutokea bila baraka za wakuu wa jiji. Zungu inabidi akomae nao hao lakini pia wananchi wakomae na huyu Masaburi. Nadhani ameamua kufanya safisha safisha, UDA sasa Ilala kota.
 
Wapangaji ni wapangaji tuu, mwenye haki ni mwenye nyumba. Sheria yetu ya upangaji ndio sheria bora kuliko zote duniani. Mwenyenyumba akiitaka nyumba yake, kwanza anakupa notice ya miezi mitatu ukae bure, ikipita, anatakiwa akutafutie nyumba ya kodi kama unayolipa mpangaji na yenye hadhi sawa, ndipo akuhamishe. Akikuta nyumba yenye hadhi sawa lakini kodi iko juu, basi mwenyenyumba huyo lazima aitop up hiyo kodi kwa miezi mitatu!.

Wakazi hao wa Ilala ni wapangaji, nyumba sio zao, wamepewa notice ya miaka 8 wakikaa bure!. Wamepewa kodi ya pango ya nyumba za hadhi hiyo kwa miezi mitatu. Wamesaini mkataba wa hiyari wa kuhama, kwa ahadi kuwa wao ndio watapewa preference ya kwanza kuhamia kwenye nyumba mpya zitakazo jengwa hapo.

Kusema ukweli, msiwasikitikie kufukuzwa kama mbwa, kwa sababu mpaka kodi za makazi mapya wamelipiwa!. Kitu cha kuwasikitikia na kuwahurumia ni changa la macho walilosainishwa eti wao ndio watakuwa wapangaji wa mwanzo wa hizo nyumba mpya!. Kama wamekaa bure miaka 8 bila kulipa kodi, hiyo kodi ya pango jipya kila mtu kalipwa kodi ya laki kwa mwezi, hayo majengo mapya, kodi yake itakuwa ni milioni kwa mwezi, hata wakipewa wao hiyo preference, wataweza kulipa?.

Hilo ndilo changa lenyewe la macho, wamesainishwa kama wapangaji na wataendelea kuwa wapangaji only if kama wataweza kulipa. The good deal, walitakiwa wawe wabia katika mradi huo kwa mkataba wa kupatiwa nyumba moja moja kwenye hayo maghorofa mapya, jambo ambalo halikufanyika!.
nafikiri kuna mchangiaji moja kaeleza hapo mtu akikaa kupita miaka kadha basi sheria ina mpa haki ya kwanza kununua nyumba hiyo ikiwa nyumba hiyo ina uzwa, pili uingereza wana sheria ambayo inawapa haki squaters kuingia na kuishi kwenye nyumba ambayo mwenyewe hayupo au ana nyumba nyingi na hiyo alio kupangisha ni ya ziada au za ziada, na pia ukiwa mpangaji wa muda mrefu, halafu ukawa una shindwa kulipa mahakama itaangalia haki zako , na pia ujerumani kuna mthungu moja ana nyumba kadhaa ambazo hapati kodi kwani squaters wamw vamia nyumba zake na kuwatoa ni issue, na ndio maana nhc kwa kuwatia ujinga wamejaribu kuwapa hiyo tshs laki tatu kupoza mambo, lakini ikiwa nhc wanataka kufanya haki, kwenye hizo nyumba mipya si watatoa nyingi, yaani maflat, ya chumba kimoja, viwili, vitatu nk nk hivyo kwa hesabu rahsi kwenye nyumba 100 watatoa 300 kwanini hizo 100 wasiwape wapangaji wa zamani na hizo mpya 200 wapangaji wapya?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom