Mada ya kiwendawazimu hii!! Bila shaka itakuwa imeletwa na mwenye uwendawazimu!
Kanisa Matoliki, hata siku moja haliombei uovu wali mwovu. Linaweza kumwomba Mungu ageuze mioyo ya waovu ili wamrudie YEYE aliye Mungu wa haki, lakini siyo kumwombea mwovu. Kwani unadhani Maduro alikuwa anafanya uovuwa kutesa, kuteka na kuua watu kwa sababu ya ukatoliki wake, au kwa sababu ya uovu wake? Kwani unadhani kujiita mkatoliki ndiyo kunaua uovu wako? HiyuMafuro muuaji, mtekaji na mtetezi wa uovu ana utofauti gani na akina Ludovick mwenye masuala ya kiimani? Akina Ludovivk wanatofautiana naye kwa sababu tu hawajapata nafasi ya kiyapoka madaraka, waliyapata watakuwa sawa naye au mtawala mwingine yeyote, kama huyu wa kwetu au Shekha wa Bangladesh.
Maduro anapokea malipo yake sawasawa na uovu wake. Mungu aamuapo kukuadhibu siyo lazima atume malaika toka mbinguni bali huweza kuwatumia wanadamu wenzako, na ndivyo alivyofanya tangu kale. Kwa mfano, Wayahudi walipokengeuka, aliwaletea mataifa adui yakawatandika na kuwachukua na kuwapeleka utumwani. Mungu si kiziwi wala bubu, hakuna sala isiyosikiwa na Mungu ila anatenda kwa kadiri ya hekima yake. Maombi ya Wavenezuela yamesikika, na Mungu ametenda, Maduro amekamatwa bila ya kusababisha maafa kwa wananchi aliokuwa akiwaonea. Ni vema Maduro akamalizia maisha yake jela, akitubu na kujutia uovu wake.
Nasi tuendelee kumwomba Mungu kwaajili ya hawa watekaji, wauaji na wadhulumaji wa haki zetu, nyakati zilizo sahihi, lazia watalilia uovu wao.