sifi leo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2012
- 5,013
- 8,369
Kumekucha waswahili usema!
Nianze na salamu wana jamvi Igweeee!
Wakati Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano akiwa ziarani mkoani Kigoma, siku ya jana alifanikiwa kumtumbua Mweka hazina wa Halmashauri kwa kosa la kukusanya ushuru na kuto kutokuingiza kwenye MFUMO!
Baada ya hatua hiyo imemuibua Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngudu Kwimba na kuamua kuwabandika wakusanya ushuru pamoja na Watendaji wote ambao wamekuwa wakusanya ushuru na kutoingiza katika Mfumo na kuwapa siku kadhaa wahakikishe wameingiza hizo fedha kwenye akaunt za Halmashauri.
Wakiongea kwa nyakati tofauti watumishi wa Halmashauri ya ambao huwa wanaingia kwenye vikao vya management wamesema kuwa watumishi hao wa Halmashauri wamekuwa wakijadiliwa sana kwenye vikao vya management na hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi yao.
"SISI watumishi ambao huwa tunaingia kwenye vikao vya management huwa tunawajadili sana ila huwa hatua hazichukuliwi dhidi yao yaani ilifkia hatua tukaisi labda wanakula na boss wetu hawa" aliongea Afisa ambaye hakuwa tayari kutajwa jina lake kwenye vyombo vya habari
Mwandishi wa habari alienda mpka kwenye ofisi za Halmashauri ya Ngudu Kwimba kudhibitisha kama kweli Majina hayo yamebandikiwa na kubahatika kukuta Tangazo ilo lilirokuwa na majina pamoja na kiasi kinachodaiwa kupigwa na wakusanya ushuru hao ambapo
Jina no moja ambalo liliandikwa hiv, Almasi Mwichete, alionekana kuwa na kiasi cha Miloni 7,000,000/= ambaye ndo wa kwanza na kufatiwa na wengine ambao wanadaiwa milioni 4000,000/= na wengine kuonekana wanadaiwa mpk sh 100,000/=
Sambamba na kubandikwa kwenye mbao wananchi wanao ishi karbu na ofisi hizi za Almashauri wamelalamika kuwa kuna watendaji ambao walishakuwa watumishi wa Almashauri hii na sasa wamestafu wamekuwa wakipelekewa madai hayo ya kurejesha fedha ili hali sio watumishi tena kitu kinachoonesha kuwa kuna kauzembe fulani huwa kanafanika hapo Almashauri.
"Mfano wewe angalia Wakati Waziri Mkuu akismamisha watumishi wa Namna ile ambao wamekusanya fedha na kutoziingiza kunakousika huyu mkurugenzi wetu anawabandika kwenye Ubao,kwa nini hasichukue hatua kama Alizo zichukua Boss Wake?""alihoji Mzee aliyejitambulisha kwa jina la Matambo.
Aliendelea kwa kusema kuwa" hii ni inshara tosha kuwa wakati Mh Rais,Makamu,na Waziri Mkuu wakicheza mziki aina ya Rumba,wapo wateule wao wanacheza Bongo Fleva na kukwamisha utendaji kazi,haiwezekani Waziri Mkuu anawafukuza wabadhilifu wewe unawapa muda wa kurejesha walitakiwa warejeshe wakiwa nje ya mfumo wa ajira na ili linawezekana katika serikali hii ya awamu ya Tano."
Sent using Jamii Forums mobile app
Nianze na salamu wana jamvi Igweeee!
Wakati Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano akiwa ziarani mkoani Kigoma, siku ya jana alifanikiwa kumtumbua Mweka hazina wa Halmashauri kwa kosa la kukusanya ushuru na kuto kutokuingiza kwenye MFUMO!
Baada ya hatua hiyo imemuibua Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngudu Kwimba na kuamua kuwabandika wakusanya ushuru pamoja na Watendaji wote ambao wamekuwa wakusanya ushuru na kutoingiza katika Mfumo na kuwapa siku kadhaa wahakikishe wameingiza hizo fedha kwenye akaunt za Halmashauri.
Wakiongea kwa nyakati tofauti watumishi wa Halmashauri ya ambao huwa wanaingia kwenye vikao vya management wamesema kuwa watumishi hao wa Halmashauri wamekuwa wakijadiliwa sana kwenye vikao vya management na hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi yao.
"SISI watumishi ambao huwa tunaingia kwenye vikao vya management huwa tunawajadili sana ila huwa hatua hazichukuliwi dhidi yao yaani ilifkia hatua tukaisi labda wanakula na boss wetu hawa" aliongea Afisa ambaye hakuwa tayari kutajwa jina lake kwenye vyombo vya habari
Mwandishi wa habari alienda mpka kwenye ofisi za Halmashauri ya Ngudu Kwimba kudhibitisha kama kweli Majina hayo yamebandikiwa na kubahatika kukuta Tangazo ilo lilirokuwa na majina pamoja na kiasi kinachodaiwa kupigwa na wakusanya ushuru hao ambapo
Jina no moja ambalo liliandikwa hiv, Almasi Mwichete, alionekana kuwa na kiasi cha Miloni 7,000,000/= ambaye ndo wa kwanza na kufatiwa na wengine ambao wanadaiwa milioni 4000,000/= na wengine kuonekana wanadaiwa mpk sh 100,000/=
Sambamba na kubandikwa kwenye mbao wananchi wanao ishi karbu na ofisi hizi za Almashauri wamelalamika kuwa kuna watendaji ambao walishakuwa watumishi wa Almashauri hii na sasa wamestafu wamekuwa wakipelekewa madai hayo ya kurejesha fedha ili hali sio watumishi tena kitu kinachoonesha kuwa kuna kauzembe fulani huwa kanafanika hapo Almashauri.
"Mfano wewe angalia Wakati Waziri Mkuu akismamisha watumishi wa Namna ile ambao wamekusanya fedha na kutoziingiza kunakousika huyu mkurugenzi wetu anawabandika kwenye Ubao,kwa nini hasichukue hatua kama Alizo zichukua Boss Wake?""alihoji Mzee aliyejitambulisha kwa jina la Matambo.
Aliendelea kwa kusema kuwa" hii ni inshara tosha kuwa wakati Mh Rais,Makamu,na Waziri Mkuu wakicheza mziki aina ya Rumba,wapo wateule wao wanacheza Bongo Fleva na kukwamisha utendaji kazi,haiwezekani Waziri Mkuu anawafukuza wabadhilifu wewe unawapa muda wa kurejesha walitakiwa warejeshe wakiwa nje ya mfumo wa ajira na ili linawezekana katika serikali hii ya awamu ya Tano."
Sent using Jamii Forums mobile app