Wakati umefika kuigawa CRDB Bank

Wakati umefika kuigawa CRDB Bank

Huyu mzungu wa NMB kaiboresha sana benki hiyo, kutoka kwenye benki iliyokuwa na huduma duni , foleni kutoka hapa na masaki, majengo mabovu lakini sas hivi hakuna foleni, majengo yameboreshwa ni ya kisasa kabisa na wanafanya open office systerm ambapo kuanzia meneja mpaka watendaji hawajajifungia mavyumbani wapo wazi wanaonekana jinsi wanavyo fanya kazi. Hakuna kutegea. Wamejiunga na VISA hivyo fedha unachukulia popote, wana ATM za kutosha na wanafungua matawi kila mahali, huku magari yao ya mobile bank yaizunguka vijijini. Bank zingine zikae chonjo

Hello Wanajukwaa,

Asante sana Avogadro kwa kutambua jitihada zinazochukuliwa na viongozi wetu hapa NMB, ni faraja kwetu kuskia kuwa juhudi zetu zinatamalaki kila kona na kuwanufaisha Watanzania wengi zaidi kwa kwa kupitia maboresho ya huduma na bidhaa zetu. Pia bila kusahau salaam zako tutazifikisha kwa Mkurugenzi Mtendaji Bi Ineke Bussemaker

Tunaendelea kuweka mipango na mikakati thabiti kuweza kuwafikia na kuwafikishia huduma watanzania wengi zaidi ili waweze kuingia kwenye mfumo rasmi wa kifedha na kunufaika na huduma za kibenki hasa ukizingatia matumizi sahihi ya teknolojia.

Endelea kuwa pamoja nasi na tusaidie kuwafikishia habari watanzania wengi zaidi kuwa sasa wanaweza kujiunga na benki yao kupitia kiganjani tu kwa kutumia *150*66# na kufungua akaunti kwa urahisi zaidi au kutumia NMB KLIK App inayopatikana iOS Store na Google Play.

Tunaendelea kuwa karibu yako zaidi #NMBKaribuYako
 
Katika dunia ya leo kufungua bank account kinatakiwa kuwa tendo la dakika zisizozidi 10, na tena ni kitu unachoweza kufanya online.

Kuna hii kasumba imejengeka katika wafanyakazi hasa sekta ya umma ya kudhani ufanisi unapimwa kwa kiasi gani unasumbua na kuwatilia ngumu wateja/wananchi na kuwapa wakati mgumu badala ya kutatua matatizo yao haraka iwezekanavyo. Hilo ndiyo inabidi iwe kipaumbele na kama kuna kasoro zozote katika rekodi au documents zake unakuja kuzitatua baadae. Kuna wakati wanatumia visingizio tu kwa sababu wamepotoka, hawajui majukumu yao ni nini hasa. Inabidi kweli tubadilike.
 
Hello Wanajukwaa,

Asante sana Avogadro kwa kutambua jitihada zinazochukuliwa na viongozi wetu hapa NMB, ni faraja kwetu kuskia kuwa juhudi zetu zinatamalaki kila kona na kuwanufaisha Watanzania wengi zaidi kwa kwa kupitia maboresho ya huduma na bidhaa zetu. Pia bila kusahau salaam zako tutazifikisha kwa Mkurugenzi Mtendaji Bi Ineke Bussemaker

Tunaendelea kuweka mipango na mikakati thabiti kuweza kuwafikia na kuwafikishia huduma watanzania wengi zaidi ili waweze kuingia kwenye mfumo rasmi wa kifedha na kunufaika na huduma za kibenki hasa ukizingatia matumizi sahihi ya teknolojia.

Endelea kuwa pamoja nasi na tusaidie kuwafikishia habari watanzania wengi zaidi kuwa sasa wanaweza kujiunga na benki yao kupitia kiganjani tu kwa kutumia *150*66# na kufungua akaunti kwa urahisi zaidi au kutumia NMB KLIK App inayopatikana iOS Store na Google Play.

Tunaendelea kuwa karibu yako zaidi #NMBKaribuYako
Hivi NMB mna online payment options like mtu akitaka kuunga na PayPal or kufanya direct online purchases?
 
Mi mbona nilifungua account ndani ya nusu saa?
Itakua madhaifu ya branch moja, na meneja wa branch ni hovyoo
 
Hakuna bank yenye customer service mbovu kama CRDB. Wale wadada wanaona raha kukiwa na foleni ndefu. Ukifata huduma tafadhali usiwe na haraka au jukumu jingine. Tenga siku nzima kwa ajili hiyo tu.
Alafu huwa majitu hayajui sio ujanja wateja kukaa kwenye foleni muda mrefu... kila mahali ni mafileni tu..kazi tufanye saa ngapi sasa!
 
Kwangu mm kwa benki za tz crdb ndo benki bora kabisa maana wanahuduma nzuri sana ukiondoa mabenki madogo madogo kama exim, backlays nk. Crdb wanaongoza. Nishakuwa na benki nbc, backlays, postal na crdb. Postal wana huduma nzuri ila kwa mikopo0 kabisa ukikopa utashangaa malipo hayaeleweki mf. Mm nlikopa tukaelewana wanakata laki5 kila mwezi cha kushangaza mpaka namaliza walikuwa wanakata laki7 mkopo wa miaka 3 na miezi haikupungua nikaambiwa watazirudisha sijarudishiwa hata cent nimeshaandika barua zinafika 10
 
Hello Wanajukwaa,

Asante sana Avogadro kwa kutambua jitihada zinazochukuliwa na viongozi wetu hapa NMB, ni faraja kwetu kuskia kuwa juhudi zetu zinatamalaki kila kona na kuwanufaisha Watanzania wengi zaidi kwa kwa kupitia maboresho ya huduma na bidhaa zetu. Pia bila kusahau salaam zako tutazifikisha kwa Mkurugenzi Mtendaji Bi Ineke Bussemaker

Tunaendelea kuweka mipango na mikakati thabiti kuweza kuwafikia na kuwafikishia huduma watanzania wengi zaidi ili waweze kuingia kwenye mfumo rasmi wa kifedha na kunufaika na huduma za kibenki hasa ukizingatia matumizi sahihi ya teknolojia.

Endelea kuwa pamoja nasi na tusaidie kuwafikishia habari watanzania wengi zaidi kuwa sasa wanaweza kujiunga na benki yao kupitia kiganjani tu kwa kutumia *150*66# na kufungua akaunti kwa urahisi zaidi au kutumia NMB KLIK App inayopatikana iOS Store na Google Play.

Tunaendelea kuwa karibu yako zaidi #NMBKaribuYako
Mkuu mfikishieni salam huyo mkurugenzi
Pia napenda kutoa pongezi kwa tawi lenu la Mwanhuzi wilaya ya Meatu.

Kuna Jamaa pale ni bank Teller, mwembamba na mweupe sana.

Aisee, nina accounts benk 3, NMB, CRDB na Diamond Trust.

Lkn ktk bank zote na Branch nilizowahi pata huduma sijawahi pata customer care nzuri kama ya yule jamaa.

Kwanza jamaa anaioenda kazi yake, anasikiliza kila mtu.

Hachoki kukuhangaikia kutatua shida yako.

Kiukweli nilitokea kupenda utendaji kazi wake.

Jina lake silifahamu ila kila mwezi naonaga anashinda kuwa mfanyakazi bora.

Ni mweupe sana na mwembamba.

Salam zimfikiee.
 
Kwangu mm kwa benki za locals Tanzania, CRDB is the best ikifuatiwa na NBC, wewe inaonekana kuna document hukuwa nazo z utambulisho wakati unaenda kufungua AC
NBC hawa hawa? Mimi walinishinda...
 
CRDB benki tatizo ni management wamefungua vibranch vingi lakini ufanisi zero.,,ndio shida ya ajira za kindugu
 
Kuna siku niliendackutoa pesa, kufika pale wakaniambia akaunti imefungwa hivyo nifanye process za kuactivate, nikawaluliza kwanini imefungwa waksema sijatumia muda mrefu, nikawauliza ni muda gani mrefu ambao akaunti hufungwa,? Wakasema miezi sita, nikasema mbona mimi mara ya mwisho kutoa hela ilikuwa wiki iliyopita, wakasema basi siyo muwekaji ni mtoaji..nikacheka sana, baadaye nikawaambia mimi sina muda wa kufanya huo ujinga wa kuactivate account, hayo ni makosa yao na waactivate wao, la sivyo mimi nakwenda mahakamani.......waliwasiliana na makao makuu haraka mpaka suluhu ikapatikana ila walinichelewesha sana kufanya mambo yangu
 
Back
Top Bottom