Wakala wa Vodacom Singida ajiua

Wakala wa Vodacom Singida ajiua

Makamee

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2013
Posts
2,029
Reaction score
1,201
Wakala mkuu wa huduma za vodacom mkoani Singida anaejulikana kwa jina la MASHA COM amejiua usiku wa kuamkia leo kwa kujipiga risasi kwa kutumia silaha aina ya bastola anayoimiliki.

Chanzo cha kujiua kwake inasemekana ni madeni makubwa anayodaiwa toka kwa wafanyabiashara pamoja na taasisi za fedha.

Kamanda wa polisi Mkoa J.KAMWELA amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
 
Pole sana kwa familia na ndugu wa marehemu,Mwenyezi Mungu awape moyo wa faraja na subira!
Tuwe makini na mikopo yunayochukua
 
Pole sana kwa familia na marafiki.
Hivi ukijiua madeni yanakwisha?
 
wakala mkuu wa huduma za vodacom mkoani singida anaejulikana kwa jina la masha com amejiua usiku wa kuamkia leo kwa kujipiga risasi kwa kutumia silaha aina ya bastola anayoimiliki.

Chanzo cha kujiua kwake inasemekana ni madeni makubwa anayodaiwa toka kwa wafanyabiashara pamoja na taasisi za fedha.

Kamanda wa polisi mkoa j.kamwela amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

wanaomiliki basyola mbona haziwasadii?
 
kwa hiyo waliokuwa wakimdai imekula kwao!!!!
kweli kukopesha ni hatari.

pole kwa walioumizwa
 
Pole yake aiseee. Hii imenikumbusha diwani wa Mlangali Ludewa aliyejinyonga ili kukwepa madeni. Tuwe makini tunapochukua mikopo.
 
Pole nyingi kwa wafiwa

Ukweli mikopo ni ya kuwa nayo makini lakini
uamuzi aliochukua sio sahihi.angeshirikisha
watu wawili wangempa mawazo mema.
 
Pole sana kwa familia na marafiki.
Hivi ukijiua madeni yanakwisha?
Kwa sheria zetu za Bongo ukifa wadeni wako watataka kulipwa kutoka kwenye mali ulizoacha,,,na katika mpangilio wa kulipwa serikali ndo inaanza kulipwa,,zikibaki na wengine ndo manapata,,so omba zibaki.
 
Riba kwenye mabenki bado kubwa kwakweli,,,lkn balaa kuna watu binafsi wanakopesha pesa kwa asilimia 20-40,,ukikopa kwa hao watu lazima uchanganyikiwe.Usithubuti, na ukute Marehemu hayo ndo madeni yaliyomchanganya.
 
Hakuna cha Pole hapa!
Tumuhurumie kwa kujipeleka jehanam kichwa kichwa!
 
akamsalimie Lucifer huko
nyuma watauza au assets alizoweka kama amana
hajasalaimika kitu
 
Huyu naye -------- tu, madeni ndiyo unajiuwa?!!!!! Ukiona mambo yamekuwa mazito unakopa pesa nyingi sana halafu unahama nchi unaenda kuanza upya sehemu, la unauza vitu vyako vya thamani kisiri, uza nyumba uza magari ukipata hata 50M tambaa kaanze moja, madeni mtalipana ukirejea! Hivi bongo hakuna utaratibu wa kufile bankruptcy?
 
Riba kwenye mabenki bado kubwa kwakweli,,,lkn balaa kuna watu binafsi wanakopesha pesa kwa asilimia 20-40,,ukikopa kwa hao watu lazima uchanganyikiwe.Usithubuti, na ukute Marehemu hayo ndo madeni yaliyomchanganya.

Hahaha, huyu marehemu ameshindwa kuelewa kuwa dunia ni mashindano, you cant just give up! Yaani suala la kujiramba risasi ndiyo halipo kabisaaa, hayo madeni wawe wapole nitawalipa tu!
 
Hivi ushawahi kudaiwa na ngozi nyeusi? Lazima apige kambi nyumbani kwako.
 
Wakala mkuu wa huduma za vodacom mkoani Singida anaejulikana kwa jina la MASHA COM amejiua usiku wa kuamkia leo kwa kujipiga risasi kwa kutumia silaha aina ya bastola anayoimiliki.

Chanzo cha kujiua kwake inasemekana ni madeni makubwa anayodaiwa toka kwa wafanyabiashara pamoja na taasisi za fedha.

Kamanda wa polisi Mkoa J.KAMWELA amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

safe_image.php
Suicide.jpg
 
Back
Top Bottom