Wakala wa meli ya ‘wezi’ wa samaki ajisalimisha

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,921
22,074
Wakala wa meli ya ‘wezi’ wa samaki ajisalimisha

Na Festo Polea

HATIMAYE Wakala wa Meli ya Tawariq1, iliyokamatwa hivi karibuni ikijihusisha na uvuvi haramu katika ukanda wa Tanzania ambaye ni raia wa China, Ho Hanqing (39) amejitokeza na kujisalimisha kwa Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es salaam.


Kujisalimisha kwa wakala huyo kunafanya idadi ya watuhumiwa wanaotarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni kwa tuhuma za kufanya uharamia wa samaki katika eneo la bahari Tanzania kufikia 36.


Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema wakala huyo alijisalimisha juzi akiwa na nyaraka mbalimbali zinazohusiana na meli hiyo ambazo alifahamisha kuwa zinachunguzwa ili kufanikisha uchunguzi wa polisi dhidi ya watuhumiwa hao.


Alisema pamoja na kujisalimisha wakala huyo atajumuishwa katika kesi inayowakabili watuhumiwa 35 ambao kati yao 15 ni raia wa China, watatu Vietnam, nane Philippine, Sita Indonesia na watatu ni raia wa Kenya.


Akizungumzia kuhusu kuchelewa kwa watuhumiwa hao kufikishwa mahakamani, Kamanda Kova alisema tatizo limesababishwa na lugha zao kutoeleweka kwa sababu wanazungumza lugha ambazo zimelazimu watafutwe wakalimani ili uandikishaji wa maelezo yao ufanyike kwa usahihi na kila mmoja apate haki yake.


“Tayari tumeshapata wakalimali na kwa kuwa linahusisha watu wa kimataifa, uchunguzi huo unatakiwa kufanyika kwa umakini kwa kuwashirikisha wanasheria wa kimataifa pamoja na kuchambua na kuzingatia sheria za baharini na za mipaka,” alisema Kova.


Kamanda Kova alisema kwa kuwa suala hilo linamuonekano na mvuto wa kimataifa linashughulikiwa kwa uangalifu mkubwa na baada ya upelelezi kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani, huku kila mmoja akijua makosa yanayomkabili.


“Kwa sasa bado ni mapema kuzungumzia zaidi jambo hilo, kwa sababu uchunguzi wa sakata hilo unaendelea vizuri. Tuna kundi kubwa la wapelelezi ambao wanafanya kazi kwa umakini zaidi na kwa muda mfupi kwa ajili ya kutengeneza mashitaka yatakayowakilishwa mahakamani dhidi ya watuhumiwa hao,” alisema Kova.


Katika hatua nyingine, upakuaji wa samaki zaidi ya tani 70 waliokutwa katika meli hiyo uliendelea. Samaki hao wakihifadhiwa katika kiwanda cha Vick Fish kilichopo Mwenge jijini Dar es salaam na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi walionekana wakichunguza samaki hao mara kwa mara kiwandani hapo.


Upakuaji wa samaki hao aina ya Jodari (Tuna) na Sord (Nduaro), unatarajiwa kukamilika leo.


Kwa mujibu wa Waziri wa wizara hiyo, John Magufuli mmiliki wa meli hiyo atashitakiwa kwa sheria za kimataifa kwa kuwa imekiuka sheria za kimataifa na adhabu yake ya chini ni kulipa dola bilioni 20 ama kutaifishwa meli yake ama vyote kwa pamoja.


Meli hiyo ilikamatwa hivi karibuni ikiwa katika Bahari ya Hindi ukanda wa Tanzania, haikuwa na bendera ya kuonyesha nchi ilikokuwa ikitoka, vibali vya uvuvi na hata vibali vya kufanyia shughuli hiyo katika Bahari ya Hindi na ilifikishwa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa ukaguzi zaidi.


Kukamatwa kwa meli hiyo kunatokana na juhudi za serikali kukamata maharamia wa samaki katika Bahari ya Hindi. Ili kufanikisha azma hiyo, serikali ilikodisha meli maalumu kwa kazi hiyo kutoka Afrika Kusini na kushirikisha wanamaji wa Tanzania, Afrika Kusini na Msumbiji ambao walifanikiwa kuinasa meli hiyo ikivua samaki ndani ya eneo la bahari la Tanzania karibu na mpaka wa visiwa vya Mauritius.
 
Wakala wa meli ya ‘wezi’ wa samaki ajisalimisha

Na Festo Polea

HATIMAYE Wakala wa Meli ya Tawariq1, iliyokamatwa hivi karibuni ikijihusisha na uvuvi haramu katika ukanda wa Tanzania ambaye ni raia wa China, Ho Hanqing (39) amejitokeza na kujisalimisha kwa Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es salaam.


Kujisalimisha kwa wakala huyo kunafanya idadi ya watuhumiwa wanaotarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni kwa tuhuma za kufanya uharamia wa samaki katika eneo la bahari Tanzania kufikia 36.


Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema wakala huyo alijisalimisha juzi akiwa na nyaraka mbalimbali zinazohusiana na meli hiyo ambazo alifahamisha kuwa zinachunguzwa ili kufanikisha uchunguzi wa polisi dhidi ya watuhumiwa hao.


Alisema pamoja na kujisalimisha wakala huyo atajumuishwa katika kesi inayowakabili watuhumiwa 35 ambao kati yao 15 ni raia wa China, watatu Vietnam, nane Philippine, Sita Indonesia na watatu ni raia wa Kenya.


Akizungumzia kuhusu kuchelewa kwa watuhumiwa hao kufikishwa mahakamani, Kamanda Kova alisema tatizo limesababishwa na lugha zao kutoeleweka kwa sababu wanazungumza lugha ambazo zimelazimu watafutwe wakalimani ili uandikishaji wa maelezo yao ufanyike kwa usahihi na kila mmoja apate haki yake.


“Tayari tumeshapata wakalimali na kwa kuwa linahusisha watu wa kimataifa, uchunguzi huo unatakiwa kufanyika kwa umakini kwa kuwashirikisha wanasheria wa kimataifa pamoja na kuchambua na kuzingatia sheria za baharini na za mipaka,” alisema Kova.


Kamanda Kova alisema kwa kuwa suala hilo linamuonekano na mvuto wa kimataifa linashughulikiwa kwa uangalifu mkubwa na baada ya upelelezi kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani, huku kila mmoja akijua makosa yanayomkabili.


“Kwa sasa bado ni mapema kuzungumzia zaidi jambo hilo, kwa sababu uchunguzi wa sakata hilo unaendelea vizuri. Tuna kundi kubwa la wapelelezi ambao wanafanya kazi kwa umakini zaidi na kwa muda mfupi kwa ajili ya kutengeneza mashitaka yatakayowakilishwa mahakamani dhidi ya watuhumiwa hao,” alisema Kova.


Katika hatua nyingine, upakuaji wa samaki zaidi ya tani 70 waliokutwa katika meli hiyo uliendelea. Samaki hao wakihifadhiwa katika kiwanda cha Vick Fish kilichopo Mwenge jijini Dar es salaam na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi walionekana wakichunguza samaki hao mara kwa mara kiwandani hapo.


Upakuaji wa samaki hao aina ya Jodari (Tuna) na Sord (Nduaro), unatarajiwa kukamilika leo.


Kwa mujibu wa Waziri wa wizara hiyo, John Magufuli mmiliki wa meli hiyo atashitakiwa kwa sheria za kimataifa kwa kuwa imekiuka sheria za kimataifa na adhabu yake ya chini ni kulipa dola bilioni 20 ama kutaifishwa meli yake ama vyote kwa pamoja.


Meli hiyo ilikamatwa hivi karibuni ikiwa katika Bahari ya Hindi ukanda wa Tanzania, haikuwa na bendera ya kuonyesha nchi ilikokuwa ikitoka, vibali vya uvuvi na hata vibali vya kufanyia shughuli hiyo katika Bahari ya Hindi na ilifikishwa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa ukaguzi zaidi.


Kukamatwa kwa meli hiyo kunatokana na juhudi za serikali kukamata maharamia wa samaki katika Bahari ya Hindi. Ili kufanikisha azma hiyo, serikali ilikodisha meli maalumu kwa kazi hiyo kutoka Afrika Kusini na kushirikisha wanamaji wa Tanzania, Afrika Kusini na Msumbiji ambao walifanikiwa kuinasa meli hiyo ikivua samaki ndani ya eneo la bahari la Tanzania karibu na mpaka wa visiwa vya Mauritius.

Inaelekea hii meli ilikuwa inavua na kupeleka mali hii china.
Kwa sababu walitujengea uwanja, mi nawambia mtasikia tu kuwa sirikali imeamua kuwaachia waende. Subirini mtaona wenyewe. Hii ni nchi ya wacheza sinema:)
 
Hapo wafuasi wa Sultani CCM lazima watapigania kuwa mashahidi ,dola bilioni ishirini yaani wafuasi wakikatiwa dau la Milioni 10 tu mtasikia kimya ,ndio imetoka hiyo. :D
Kila mmoja amekuwa kiranja kumbe kuna ulaji .Ni ulaji tu hapo akuna lingine naamini mwenye meli kishazungumza nao sasa uone uchunguzi utakavyokuwa mrefu.
 
Hapo wafuasi wa Sultani CCM lazima watapigania kuwa mashahidi ,dola bilioni ishirini yaani wafuasi wakikatiwa dau la Milioni 10 tu mtasikia kimya ,ndio imetoka hiyo. :D
Kila mmoja amekuwa kiranja kumbe kuna ulaji .Ni ulaji tu hapo akuna lingine naamini mwenye meli kishazungumza nao sasa uone uchunguzi utakavyokuwa mrefu.


UKIONGEZA NA HILO HAPO JUU,hili swala litakuwa transormed kwenye POLITICS!..........ukishaingiza siasa kwenye serious matters kama hizi YOU ARE FINISHED THEN!

Ndio tatizo letu waswahili
 
Back
Top Bottom