Wajue viumbe wa ajabu waishio angani

"ukweli ni
kwamba huchukuliwa na viumbe hao"

Ukweli huwa na uthibitisho naomba unithibitishie hilo hapo juu.
halafu mkuu ni bora ukabez kwenye suala zima la uthibitisho juu ya uwepo wa aliens hayo mengine yatakuja tuu...
 
Ungekua mwanajiolojia, palaentilogist, ungejua mengi kuhusu Dinosaurs, (kasome geological time scale)
Kasome kuhusu mabaki ya hao wanyama yaliyopatikana duniani ikiwepo tanzania pia. Yule mjusi wetu alieko ujerumani

Popobawa limekaa kishirikina na kiroho zaidi, nguva yupo ila sio yule kama mwanamke(nguva ni samaki anayenyonyesha)

Hii kesi ya alliens bado inaniweka njia panda, sometimes naamin sometimes siamin

Ila huwa nawazia hiz Unidentified Flying Objects (UFO) ni vitu gan, mana ufo zimeshaonekana sana ila ndio not identified, so orign yake ni nini, hap ndo napata was was isije kuwa hizi stor za alliens ni kweli.
Mkuu ishu ya Dinosaurs wanasayansi wanadai species hiyo imetoweka miaka million 60+ huko

Inakuwaje kupitia mifupa waweze kufahamu classifications ,namna wanavyozaliana,kula ,life style yao nk

Mifupa haiozi lkn zaidi ya miaka million60 hizo mifupa zibaki tu hvy hvy lzm zingeteketea na kuwa dust

Hii ishu ya dinosaurs ni kutupumbaza kama nadharia ya mtu wa kwanza alikuwa nyani

Zaidi ya million60+ Leo utambue classifications ,maisha ya mnyama huyu mpaka documentary wametengeneza

Sikubaliani na hao archeologies
 
4ab48c7e1c1894387afea677d143b4b4.jpg

MPENZI mwanajamiiforums ungana nami katika simulizi hii mpya ya kweli inayohusu viumbe wa ajabu waishio angani. Kama ni msomaji wa vitabu vitakatifu, Mungu aliumba vitu vinavyoonekana na visivyoonekana. Inahisiwa kuwa visivyoonekana ni vingi kuliko vinavyoonekana.

Viumbe hao wa ajabu waishio angani wanaitwa Aliens. Wana muonekano kama binadamu isipokuwa hawafanani moja kwa moja na binadamu. Viumbe hao waliogundulika karne kadhaa zilizizopita wameshatengenezewa filamu nyingi na wasanii mbalimbali duniani (tutazichambua huko mbele).



Aliens wapo wa rangi tofauti kama kijani, weupe, weusi, njano, zambarau na kila aina ya rangi.

Inaaminika kuwa Aliens wanaoishi angani wana akili nyingi kuliko binadamu. Wana mfumo wa kompyuta uitwao Alien Software na wapo juu kiteknojia kuliko binadamu tatizo tuu hawavai nguo!!

bbef6c4ab3333b9205c1a0d618bd5ca0.jpg

Tofauti na binadamu ambaye anafanya kazi kwa hatua moja kwenda nyingine, Aliens wao hufanya mambo kinyume kabisa. Kwa mfano wakitaka kusema ‘naomba maji’ husema ‘maji naomba’ yaani cha nyuma kinakwenda mbele na cha mbele kinarudi nyuma. Kama tunavyowashangaa, nao pia wanatushangaa na kutuona viumbe wa ajabu.

Wachambuzi wa mambo ya anga walishaandika ripoti nyingi kuhusu viumbe hao ambao huja duniani na kurudi angani.

Swali ni je, viumbe hao wanaishi katika sayari gani? Wataalam hao wanalijibu swali hilo kwa kusema haijulikani moja kwa moja wanaishi sayari gani lakini kwa uhakika siyo kwenye mwezi (kumbuka mwezi siyo sayari).
Inawezekana bado hujaelewa simulizi hii. Bermuda Triangle ni eneo la pembetatu la bahari lililopo kati ya nchi tatu katika Bahari ya Atlantiki. Miaka kadhaa huko nyuma viumbe hao waliwahi kutua eneo hilo na kuweka historia (nitaisimulia huko mbele).

Pia waliwahi kuonekana Kisiwa cha Bermuda pwani ya Mashariki mwa Marekani, Kisiwa cha Puerto Rico kilichopo Kaskazini mwa Carrebian na Fort Lauderdale huko Florida, Marekani.
4cd821c932ba24f4754d6ba2fc593351.jpg

Umewahi kusikia vitu mbalimbali duniani vikisemekana vimepotea katika mazingira ya kutatanisha? Aliens wanahusishwa na upoteaji wa meli baharini hasa za mizigo huku watu wakiamini huwa zinazama lakini uchunguzi ukifanyika meli hizo huwa hazionekani hata ndani ya maji baharini.

Aliens wanatajwa kuhusika na upotevu wa watu duniani ikiaminika kuwa labda watu hao walikufa lakini ukweli ni kwamba huchukuliwa na viumbe hao.
Ndege za kijeshi zimeripotiwa mara nyingi kupotea au kutokuonekana milele katika eneo la Bermuda Triangle ikieleza kuwa Aliens ndiyo wahusika wa upotevu huo.
866a511132ae2accfa8036c0c5a4d82a.jpg

Ujio wa Aliens katika eneo la Bermuda Triangle ulisababisha kisiwa hicho kupata umaarufu duniani na kupewa jina la Devil’s Sea (Bahari ya Shetani) ambapo binadamu wamekuwa wakiamini au kujenga imani potofu kuwa shetani amekuwa na makazi katika eneo hilo na kuwapoteza wasafiri wa majini. Wengine huhisi ni ushirikina.

Wapo binadamu wanaoamini kuwa Aliens walikuwepo duniani tangu enzi hizo kabla ya binadamu na hawajaondoka.
Si sehemu hizo pekee lakini wamekuwa wakitua maeneo mbalimbali duniani na kuna baadhi ya serikali duniani zinawajua.
Wataalam wa anga wanadai Aliens wako mbali kimaendeleo na wanafanya wanavyotaka.

Je, hawa ni viumbe gani? Ndiyo kwanza simulizi imeanza.
INAENDELEA
MKUU wangu unaitaji kujisomea sana kupitia report za vyanzo vya kuaminika sio ku Google tu ukasoma ujui kaandika nani unakuja kufungua thread. kifupi uko juu juu sana kwenye mambo haya na utakua na busara kama usipoleta muendelezo wako Ila ukafanye research ili siku nyingine ufungue Uzi wenye mashiko. SHUKRANI
 
Wanasayansi wanasema Dinosaur walikuwepo miaka million 243 iliyopita , kisha miaka million 66 walipotea

Lakini Leo hii kupitia mifupa wanayosema ni ya dinosaurs wameweza kuwa classify kwa makundi mbali mbali ,wameeleza namna walivyokuwa wanazaliana na facts nyingi bla bla
.
Ishu ya Dinosaurs ni kuwashika watu akili tu na kuwapumbaza ,wao wanadai species hiyo ilitoweka miaka 60 huko how come wajue mambo kibao kuhusu huyo mnyama

Pia mifupa ikikaa muda mrefu ina decay ina maana miaka million 60 huko hyo mifupa haiozi tu

Haha Yale yale binaadamu wa kwanza nyani ..
kwa namna hali ilivyo mashaka yamekuwa mengi siku hizi. mfn, kuna hii kitu imeibuka siku hizi ya masalia ya binadamu mwenye mwili mkubwa, ni kweli unaona wataalamu wa mambo ya kale wako busy kuchimba masalia. baadae utaona kweli picha nyingi tu za masalia ya mifupa ama fuvu ambalo pengine hata kwenye pickup haliingii, ila zimebaki hadithi tu! kwa wanao fatilia program moja mystery at the musium katika ch ya viasat history wamepata kuona baadhi ya vitu ambavyo watu waliwahi kuvichonga au kutengeneza na kisha kufukia ardhini kwa miaka kadhaa. kisha huvifukua na kutangaza wamechimbua masalia ya kale, badae huanza kutoza fedha kwa watakao taka kuona. walitengeneza pesa za kutosha, ila walio kuwa wanastukiwa wengi walitoroka ama kuhukumiwa vifungo.
mfn; kama mtakumbuka miaka ya karibuni kuna artist alitengeneza nguva kwa material maalum na kisha kumtupa pwani ya moja ya ufukwe (Ujerumani, 'sina hakika') nadhani wengi wanaikumbuka hii issue ilivyovuma kwenye mitandao, ila baadae jamaa alikuja kitoa clip namna alivyofanikisha zoezi lake.
hayo ni kwa yale tunayojua, je! ni mangapi tumefichwa?
safari bado ni ndefu ndugu, kama bado kuna wanao amini hata hili la allien dunia ya leo basi kazi ipo...
 
yaani unaenda mbele unarudi nyuma umesema wanaishi angani je mmewahi kuona wanapo ishi??????? pia umesema wana teknolojia kubwa kupita ya binadamu je mmeshawahi kuiona hiyo teknologia yao????????????????
kamammeshaona wanapoishi na hivyo vitu vingine leteni na uthibitisho sio maneno matupu tu..... hatudanganyiki:D:D:D:D
 
4ab48c7e1c1894387afea677d143b4b4.jpg

MPENZI mwanajamiiforums ungana nami katika simulizi hii mpya ya kweli inayohusu viumbe wa ajabu waishio angani. Kama ni msomaji wa vitabu vitakatifu, Mungu aliumba vitu vinavyoonekana na visivyoonekana. Inahisiwa kuwa visivyoonekana ni vingi kuliko vinavyoonekana.

Viumbe hao wa ajabu waishio angani wanaitwa Aliens. Wana muonekano kama binadamu isipokuwa hawafanani moja kwa moja na binadamu. Viumbe hao waliogundulika karne kadhaa zilizizopita wameshatengenezewa filamu nyingi na wasanii mbalimbali duniani (tutazichambua huko mbele).



Aliens wapo wa rangi tofauti kama kijani, weupe, weusi, njano, zambarau na kila aina ya rangi.

Inaaminika kuwa Aliens wanaoishi angani wana akili nyingi kuliko binadamu. Wana mfumo wa kompyuta uitwao Alien Software na wapo juu kiteknojia kuliko binadamu tatizo tuu hawavai nguo!!

bbef6c4ab3333b9205c1a0d618bd5ca0.jpg

Tofauti na binadamu ambaye anafanya kazi kwa hatua moja kwenda nyingine, Aliens wao hufanya mambo kinyume kabisa. Kwa mfano wakitaka kusema ‘naomba maji’ husema ‘maji naomba’ yaani cha nyuma kinakwenda mbele na cha mbele kinarudi nyuma. Kama tunavyowashangaa, nao pia wanatushangaa na kutuona viumbe wa ajabu.

Wachambuzi wa mambo ya anga walishaandika ripoti nyingi kuhusu viumbe hao ambao huja duniani na kurudi angani.

Swali ni je, viumbe hao wanaishi katika sayari gani? Wataalam hao wanalijibu swali hilo kwa kusema haijulikani moja kwa moja wanaishi sayari gani lakini kwa uhakika siyo kwenye mwezi (kumbuka mwezi siyo sayari).
Inawezekana bado hujaelewa simulizi hii. Bermuda Triangle ni eneo la pembetatu la bahari lililopo kati ya nchi tatu katika Bahari ya Atlantiki. Miaka kadhaa huko nyuma viumbe hao waliwahi kutua eneo hilo na kuweka historia (nitaisimulia huko mbele).

Pia waliwahi kuonekana Kisiwa cha Bermuda pwani ya Mashariki mwa Marekani, Kisiwa cha Puerto Rico kilichopo Kaskazini mwa Carrebian na Fort Lauderdale huko Florida, Marekani.
4cd821c932ba24f4754d6ba2fc593351.jpg

Umewahi kusikia vitu mbalimbali duniani vikisemekana vimepotea katika mazingira ya kutatanisha? Aliens wanahusishwa na upoteaji wa meli baharini hasa za mizigo huku watu wakiamini huwa zinazama lakini uchunguzi ukifanyika meli hizo huwa hazionekani hata ndani ya maji baharini.

Aliens wanatajwa kuhusika na upotevu wa watu duniani ikiaminika kuwa labda watu hao walikufa lakini ukweli ni kwamba huchukuliwa na viumbe hao.
Ndege za kijeshi zimeripotiwa mara nyingi kupotea au kutokuonekana milele katika eneo la Bermuda Triangle ikieleza kuwa Aliens ndiyo wahusika wa upotevu huo.
866a511132ae2accfa8036c0c5a4d82a.jpg

Ujio wa Aliens katika eneo la Bermuda Triangle ulisababisha kisiwa hicho kupata umaarufu duniani na kupewa jina la Devil’s Sea (Bahari ya Shetani) ambapo binadamu wamekuwa wakiamini au kujenga imani potofu kuwa shetani amekuwa na makazi katika eneo hilo na kuwapoteza wasafiri wa majini. Wengine huhisi ni ushirikina.

Wapo binadamu wanaoamini kuwa Aliens walikuwepo duniani tangu enzi hizo kabla ya binadamu na hawajaondoka.
Si sehemu hizo pekee lakini wamekuwa wakitua maeneo mbalimbali duniani na kuna baadhi ya serikali duniani zinawajua.
Wataalam wa anga wanadai Aliens wako mbali kimaendeleo na wanafanya wanavyotaka.

Je, hawa ni viumbe gani? Ndiyo kwanza simulizi imeanza.
INAENDELEA
Ni mapepo tu
 
Hakuna cha alliens wala cha nini

Hakuna aliyewahi kumuona alliens ni kama vile dhana ya popobawa au nguva ..

Kama alliens wapo mbona hakuna uthibitisho wa picha au video.

Hata dinassour pia ni dhana ..

Alliens,popobawa,dinassours,nguva kiuhalisia hawapo bali wametungwa tu na wanaadamu ..miaka yote tunasikia nguva,alliens,popobawa lkn picha zao hatuzioni
Umesema vyema lakini cha ajabu mtu kama wewe utakuta unaamini kwamba mungu yupo.!
 
Umesema vyema lakini cha ajabu mtu kama wewe utakuta unaamini kwamba mungu yupo.!
Ishu ya Mungu tofauti na dhana ya aliens nk

1.kuna uthibitisho nitakupa,duniani hakuna jambo la chance kila kitu kinatengenezwa mfano meli,gari,silaha,nyumba hazijatokea by chance bali zilitengenezwa na wanaadamu

Robot haikutokea by chance Bali mtu ndio aliyoitengeneza

Pia milima ,bahari,dunia,sayari, viumbe havijatokea by chance yupo aliyetengeneza na kuumba
So dhana nzima ya dini yeyote ile ni kuabudu basi huyo aliyetengeneza na kuumba hii dunia ndio anapaswa kushukuriwa

Jibu ya uthibitisho wangu Mungu ana exist sababu hakuna kitu kinachoitwa creation by chance..
 
Mystical stories, no credible source imeconfirm uwepo wa Ellien.
By the way according to space expertise definition ya ellien ni kitu chochote chenye uhai kilichopo nje ya dunia ( ambacho kijatoka duniani). Kiwe mmea,mnyama, bacteria nk...na co lazima kiwe na intelligence!!
 
Hakuna cha aliens wala nini. Huko ni kutufumba macho ili tusitafiti kwa yale yanayotokea, Hiyo ni mipango ya NASA
 
Alien ni jina la kiumbe wa kubuni, alibuniwa na watengeneza muvie, hakuna ili kunogesha muvie kwa kusimulia viumbe wa ajabu wasiowahi kuthibitika
 
Sasa wanaakili kuzidi binadamu inamaana huku juu kuna magari ya kisasa kuliko haya, na akili yao wanatumia kufanyia nn? Yasiwe ya akina Alpha holela au Abunuasi.
 
IsNani..a Mungu tofauti na dhana ya aliens nk

1.kuna uthibitisho nitakupa,duniani hakuna jambo la chance kila kitu kinatengenezwa mfano meli,gari,silaha,nyumba hazijatokea by chance bali zilitengenezwa na wanaadamu

Robot haikutokea by chance Bali mtu ndio aliyoitengeneza

Pia milima ,bahari,dunia,sayari, viumbe havijatokea by chance yupo aliyetengeneza na kuumba
So dhana nzima ya dini yeyote ile ni kuabudu basi huyo aliyetengeneza na kuumba hii dunia ndio anapaswa kushukuriwa

Jibu ya uthibitisho wangu Mungu ana exist sababu hakuna kitu kinachoitwa creation by chance..
Atakuuliza-huyo Mungu yeye kaumbwa/katengenezwa na nani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom