Wajue Mashujaa na Maadui wa Katiba Mpya, Madui wa Muungano/Mashujaa wa Zanzibar!

Omutwale

JF-Expert Member
Feb 4, 2008
1,429
1,045
Watanganyika tuna ugonjwa mbaya sana wa kupuuzia tahadhari za msingi wakati zinapotolewa na kusahau haraka kiasi kwamba tunashindwa kukumbuka hata baada ya madhira kutufika> Tunakuwa utadhani hatukuwahi kupewa tahadhari.

Kwenye suala la Katiba na Uhai wa Muungano sitasahau kamwe jinsi Tundu Lissu alivyotaanabaisha mara nyingi juu ya athari na maana ya mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar. Leo hii mkwamo utakaopelekea Mchakato wa Katiba mpya kuvunjika ni suala la Zanzibar kujitambulisha kama nchi kwenye Katiba yake mpya. Kama kuna muujiza haujapata kutokea duniani na unasubiriwa kwa hamu utokee basi ni muujiza wa Bunge la Katiba kubadilisha Sura ya Sita ya Rasimu ya Katiba na kisha kupata 2/3 ya kura za Wajumbe ili kunusuru Muungano wa nchi mbili na Serikali mbili!

Mpaka hatua hii ya mchakato wa Katiba nawatunuku wafuatao vyeo vifuatavyo:

Mzee Joseph Sinde Warioba -- Baba wa (Rasimu ya) Katiba ya Wananchi
Mh. Tundu Lissu --Shujaa wa Kulinda Katiba ya Muungano
Mh. Jakaya Kikwete --Mwanamageuzi Yabisi/Adui wa Muungano
Mh. Ismail Jussa -- Shujaa wa Dola ya Zanzibar

Changia kwa kuongeza orodha!!
Julai, 2012 katika Bunge Mh. Tundu Lissu alisema haya:

Archieve
: Jumuiya ya UAMSHO Zanzibar

Lakini kabla mnamo Novemba 2011 Mh. Tundu Lissu alikwisha onya kwa kuandika haya:

 
Last edited by a moderator:
Jk hangeweza kuwakemea wazanzibar kwa kuvunja muungano kutokana na katiba yao kuitambua Zanzibar kuwa ni nchi.Kwani hakuna kitu kilichofanywa na Zanzibar bila ya idhini yake.Jk alikuwa ana jaribu kukiokoa chama chake ambacho kinatapatapa kama mtu aliye kabwa na kuishiwa pumnzi.
 

ni sahihi alichosema tundu lisu lakini ndio mamuzi ya WAZANZIBAR .KUpunguza mbawa muungano maana kila tukidai mabadiliko ni kebehi na dharau .kilichofanywa ni hatua ya makusudi ya upande mmoja kulinda utambulisho wa zanzibar kama TAIFA na kwa hilo sote waznz tunakubaliana (ZANZIBAR KUENDELEA KUBAKI KUWA NCHI).
KUMBUKENI mwaka mmoja tu baada ya muungano baba wa taifa la tanganyika Nyerere aliaza kuvunja makubaliano ya muungano kwa kuahirisha undwaji wa katiba ya muungano kwa mda usiojulikana kwa kutumia bunge ambalo halikupewa mamlaka hayo na mkataba wa muungano. yeye aliyatoa wapi mamlaka hayo mtatueleza kwenye bunge la katiba mjadala ukiaza ,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…