Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara, ambaye aliwahi kuwa mwanachama wa Chadema kabla ya kujiunga na CCM, ameibua tuhuma nzito dhidi ya wakili maarufu Fatma Karume, akimtuhumu kwa kushiriki kile alichokiita "utapeli wa kisiasa" unaohusiana na mzozo wa wachimbaji wa Nyamongo.
Akizungumza bungeni leo, Aprili 11, Waitara amedai kuwa Fatma Karume ameingia ubia na baadhi ya watu wa Nyamongo kufungua kesi nchini Canada kwa madai ya kutetea haki za wakazi wa eneo hilo.
"Wale watu ambao wamefanya ziara kule kusini, Makamu Mwenyekiti yule kijana bwana mdogo ni muongo na mbinafsi. Na kama akija kwenye jimbo lako, kiboko yake nipo. Yule nimemgonga 2008, nimemgonga 2015, nimemgonga 2020 na mwaka huu kichapo kipo pale pale,"
"Huyu ameenda kwenye hifadhi ya Serengeti, anajua kuna sheria anawaambia chukueni ng'ombe mkachunge hifadhini, zilikamatwa ng'ombe na watu waliumia yeye akala kona hakuwasaidia... Huyu ni mbinafsi".
Akizungumza bungeni leo, Aprili 11, Waitara amedai kuwa Fatma Karume ameingia ubia na baadhi ya watu wa Nyamongo kufungua kesi nchini Canada kwa madai ya kutetea haki za wakazi wa eneo hilo.
"Wale watu ambao wamefanya ziara kule kusini, Makamu Mwenyekiti yule kijana bwana mdogo ni muongo na mbinafsi. Na kama akija kwenye jimbo lako, kiboko yake nipo. Yule nimemgonga 2008, nimemgonga 2015, nimemgonga 2020 na mwaka huu kichapo kipo pale pale,"
"Huyu ameenda kwenye hifadhi ya Serengeti, anajua kuna sheria anawaambia chukueni ng'ombe mkachunge hifadhini, zilikamatwa ng'ombe na watu waliumia yeye akala kona hakuwasaidia... Huyu ni mbinafsi".