Waitara: Wanasiasa wanaokaa chama kimoja muda mrefu ni Manungayembe

Waitara: Wanasiasa wanaokaa chama kimoja muda mrefu ni Manungayembe

Chinga One

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2013
Posts
11,493
Reaction score
12,453
Kupitia kipindi cha Jahazi,cha Clouds fm,Mbunge wa zamani wa Ukonga kwa tiketi ya CDM, Mwita Waitara amesema wanasiasa wanaodumu kwa muda mrefu kwenye chama kimoja ni "Manungayembe".

Waitara amesema huwezi kuwa awamu zote we upo upinzani tu lazima ubadilike..."huwezi kuwa miaka yote upo upinzani tu kaja Nyerere we ni mpinzani, kaja Mwinyi we ni mpinzani, kaja Mkapa bado uko upinzani, mzee Kikwete we upo upinzani hadi Magufuli bado unapinga tu we huwezi kuwa mwanasiasa we ni Nungayembe tu" amesema Waitara.

Waitara alijiuzulu nafasi yake ya ubunge na kujivua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM mapema mwezi huu, kwa madai ya kuunga mkono juhudi za rais Magufuli
 
Anamaanisha jina lisipopita mwaka 2020 atarudi upinzani?

Sijui kama atapokelewa maana hana akiba ya maneno ila angeondoka kimya kama Shibuda huenda angepokelewa
 
Ngoja hela ziishe maana za bwana yule zilikate ikabidi aje sasa kuanza kuharibu

Ukishiba kaa kimya maana kesho nayo siku
 
Back
Top Bottom