Waislamu wazindua program 2010

Mbona unaweka tafsiri yako mwenyewe wala siyo ya shura ya maimamu? nikupe ufafanuzi kwa ufupi wa maswali yako 1-5
1. Muadilifu hawezi kuwa Mdini

2. Anatakiwa awe anafahamu historia ya ubaguzi Tanzania hapo kuna tatizo gani? au wewe unapenda sana kupendelewa pasipo haki? ulishaona kupendelewa ni haki siyo?

3.Tume huru inatakiwa kudhibitisha kama waislamu walianza kufanya fujo au walifanyiwa fujo kwa maagizo kutoka kwa watu wenye nia mbaya na nchi hii ambao wanaweza kukimbia nchi na kujificha huko wanakoficha waovu?? hapo kuna tatizo gani? kufanya uchunguzi ili jamii iridhike

4. Uchunguzi wa kanisa kuchomwe ulishafanyika na wenye kanisa wameridhika na hatua zilizochukuliwa ndio maana hakuna malalamiko yeyote kutoka kwao lakini uchunguzi kwa upande wa waislamu haukufanyika na hawataki kufanya hivyo, shura inataka mtu ambaye hafichi uchafu huo awe mkristo au muislamu??

5. kumzuia Osama bin laden na kazi yake chafu haina maana kuwanyima haki zao waislamu na kuwakandimizi kwa kutumia external forces..je wewe utafurahia kwasababu LRA wanafanya fujo uganda wakristo wote wa Tanzania watungiwe sheria mbaya?

"Si kweli kwamba sifa ya kiongozi wa shura ya waislamu lazima awe muislamu ila ni Mtanzania mwenye kudhamini utu wa watu wote wakiwemo waislamu" hatundanganyiki na propanda zako...


Huna Lolote Tumaini...Mnajichanganya tu! Yani hiyo report huwezi kuilinganisha na ile ya katoliki hata tone, yao ilikua ya kitaalam na kisomi zaidi, yani ilikua ngumu kujua wanamtaka mtu wa dini yao...it was so general tofauti na nyie yani ipo live and direct kwamba mnataka kiongozi wa dini yenu, mi nawaambia ubaguzi utawamaliza na hali ya kuendeleza vinyongo ambazo nyie ndio mlitafsiri kipotofu hakutawafikisha popote.

Kitendo cha kusema "awe mtu ambae atachunguza mauaji kwenye maandamano yale yakusema YESU si mungu" that means hamjatambua kwamba mlifanya kosa kuzungumzia dini ya watu wengine, yani mnaona mlichofanya ni haki. sasa tutawaaminije itapotokea pande nyingine(eg christians) watapofanyiwa uonevu, kutukanwa, kuchomewa makanisa yao na daily insults ambazo huwa tunazisikia, je huyo kiongozi mnaemtaka atasimama wapi? kwa maelezo mafupi tu inaonyesha dini nyingine hazitakua na haki...hata huyo kiongozi wenu amesema muongozo unafanya kazi, eti ukiangalia 90% ya waliochaguliwa huko kusini ni watu walioushika vizuri muongozo, tht prove huo muongozo unaonekana kufanya kazi kwa sababu waliochaguliwa ni waislam....

GOD PLS FORGIVE US BECAUSE WE DONT KNOW WHAT WE ARE DOING!
 
Kwa kusoma hii program ya mwongozo ya 2010 sioni kama kuna la kujadili.

Kwani yenyewe imejikita katika kuweka timeframe ya kutekeleza mwongozo hususan katika kutoa elimu ya uraia na haki za mpiga kura na kuchaguliwa kiongozi.

Imejikita zaidi katika kutekeleza na kutoa elimu ya uraia kwa waumini,

Sasa sioni kwa nini mnajadili sana.

nawashauri kila mtu anaweza kupata nakala yake na kuisoma aielewe kisha ndipo mlete debate.

Tuusome marangapi barubaru....haiitaji digrii kujua mlichoandika huko ni ubaguzi...af kitendo cha kulenga wakristo wakati nchi hii inawatu wa dini zaidi ya hizo mbili siwaelewi kabisa.
 
Huo wimbo wa "waislamu wanaonewa" sijui utaisha lini. Hayo ni mambo ya kufikirika tu wala hakuna ukweli wowote. Ushauri wangu kwa waislamu ni kwamba waelekeze nguvu katika kusomesha watoto wao kama wanavyoelekeza nguvu kwenye madrasa. Wenzao wakristo wana-invest kwenye masuala yote; dini na elimu. Hivyo, siyo jambo la kushangaza kuona kuwa asilimia kubwa ya waislamu hawajasoma ikilinganishwa na wakristo. Hii siyo siri ni ukweli tu. Hata hao wanaojiita shura ya maimamu ukiwachambua kwa kina utagundua elimu yao imeishia kwenye masuala ya dini tu. Masuala ya kidunia ni patupu! Ukitaka uamini hoja yangu soma hayo maandishi yao ya kurasa 76 hutaona substance yoyote. Jambo la kushukuru ni kwamba hata waislamu wenzao ambao wameelimika kidunia wanawapuuza hao maimamu.
kama kuna muislamu anaepuuza maimamu wa kiislamu basi huyo amepotea,kwa kipimo cha matashi ya nafsi yako ndo unamuona kaelimika!
 
Kwa kusoma hii program ya mwongozo ya 2010 sioni kama kuna la kujadili.

Kwani yenyewe imejikita katika kuweka timeframe ya kutekeleza mwongozo hususan katika kutoa elimu ya uraia na haki za mpiga kura na kuchaguliwa kiongozi.

Imejikita zaidi katika kutekeleza na kutoa elimu ya uraia kwa waumini,

Sasa sioni kwa nini mnajadili sana.

nawashauri kila mtu anaweza kupata nakala yake na kuisoma aielewe kisha ndipo mlete debate.
Nafikiri issue hapa ni kwamba kabla dola (dola yetu haina dini) haijaingilia kati jambo hili, wasomi walioko huko kwenye vyombo vyetu vya dini ama imani mbalimbali zilizopo nchini wakae chini na kujadili ni kwa namna gani hii miongozo inayoibuka kutoka kila kundi la dini inaweza ikawa harmonized to lead Tanzanians (categorically their worshippers) to a right path of electing their national leader(s) who in turn (national leaders) will serve for national interests as shall be opposed to some group interests which might be the current fuel for such prolifirating miongozo.

Ukiwa na mtazamo mpana zaidi utabaini kuwa ipo haja ya serikali hata watanzania kwa ujumla kuwa makini zaidi na miongozo hii kwani usijeshangaa hapo badae dhana ikapanuka zaidi hata rais itaepata madaraka kwa uwiano wa karibu zaidi na mantiki ya muongozo wa kikundi fulani cha dini akapewa pia mwongozo wa kupata mawaziri na watendaji wengine wa serikali. Hapa itapendeza zaidi kama hayo yametendeka kwa maslahi ya taifa na wala si kwa kuzingatia UDINI ambao kwa namna moja ama nyingine unaonekana kuanza kulalamikiwa na baadhi ya wananchi ndani ya serikali yetu. Hofu yangu nikwamba miongozo hiyo isijekuwa ni vivuli vya huo UDINI.

Lakini pia panaweza kutokea kundi fulani la dini kuunga mkono mwongozo uliotolewa na kundi jingine kama siyo kutaka marekebisho katika mwongozo huo. Hapa tutajikuta badae tunzaanzisha Ofisi ya Msajili wa Miongozo ya Dini Mbalimbali kama ilivyo kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.

Hata hivyo suluhu iliyokubwa zaidi kwa matatizo kama haya (yanayopelekea kuzaliwa miongozo)itakuwa ni kwa wale wenzetu waingiao madrakani kutenda kazi zao ama kufanya teuzi zao kwa kuzingatia maslahi ya taifa badala ya kuweka mbele viaina fulani vya upendeleo kwa makundi fulani ya dini, kabila ama ukanda. Tatizo ni je, viongozi wa aina hiyo tunao? au the beuatyful ones are not yet born? or the beautiful ones will be born but also might become poluted by, among other factors, miongozo?
 
Hivi inawezekana mzaramo kuwa mbunge kule Tarime, au mmakonde kuwa mbunge wa Biharamulo.

kama sasa mambo hayo hakuna basi ndio tunakwenda another stage.

Dhambi ya ubaguzi imeanza kutusurubu.
 
Wanajamvi mtanisamehe si mchango kwenye hii thread kwasababu haisaidii kujenga taifa letu bali kulibomoa kwa faida watu wachache wenye uelewa duni.
 
Hivi inawezekana mzaramo kuwa mbunge kule Tarime, au mmakonde kuwa mbunge wa Biharamulo.

kama sasa mambo hayo hakuna basi ndio tunakwenda another stage.

Dhambi ya ubaguzi imeanza kutusurubu.

Kwa hiyo kama tulivyoanza na shule za kidini basi unataka tufike mahali ambapo tugawane mitaa? Tuwe na maeneo tofauti ya waislamu, wakristu, wasio na dini, wahindu, mabuddha, n.k.? Halafu baadae hayo hayo maeneo yagawanye kwa ajili ya wasunni, washia, mabohora, wakatoliki, waluteri, waanglikana, majehova n.k? Patakalika kweli?

Amandla....
 
Mhhhh! wewe ukiacha kuingiza udini wako na sisi tutaacha lakini wewe unafikiri ukifanya insult kwa uislamu wenye dini zetu tutanyamaza..ikitaka kuheshimiwa jiheshimu
"YOU HIT ME ONCE, I HIT YOU TWICE" ............. Huu ndiyo msemo wa watu wenye kuishi kwa visasi............. Yeye saa zote anawaza JINO KWA JINO........... ngangari kwa ngunguri........... Yaani kwake hana muda wa kusamehe......... So long as mtu kamuanza basi atalipiza kwa kiasi kikubwa sana... simply because ameanzwa.............
 
Hii hoja naona inachangiwa sana na kuungwa mkono na watu walewale..... Kinachonishangaza ni kuwa watu hao hawaishi Tanzania, wao kazi yao ni kutupandikiza chuki na baada ya hapo nina uhakika hawataonekana tena wakati tumeshalikoroga.......... Kwa maana hiyo watatuacha tunalinywa wenyewe. Mtu kama Barubaru, kaja Tanzania kwa siku saba na kurudi huko anakoishi. Hivi unategemea mtu kama huyo tukijiingiza kwenye vita ya kidini atakuja tena..???? Nionacho ni kuwa atabaki huko aliko, na sana sana anatoa misaada ya mabomu kwa watakaokuwa upande wake, lakini distantly.

Tuacheni tunaojuwa hali halisi ya TZ tuichangie hoja hii. Hii habari ya kuifananisha TZ na nchi zinazoongozwa kiislamu muiache kabisa. Hatutumii sharia....bali sheria.

Ni wazi kabisa kwamba kinachoelezwa kwenye hiyo program ni kumchagua kiongozi ambaye ni MUISLAM anayebisha huyo hajaielewa hiyo program na ninamshauri akaisome tena.....

NINA UHAKIKA KUWA PAMOJA NA KWAMBA KINGUNGE ALIUPINGA WARAKA WA WAKATOLIKI, LAKINI AKIGOMBEA NAFASI YOYOTE WAISLAM HAWATAMPA KURA............. Sababu ni kuwa yeye si MUISLAM
 
Hii hoja naona inachangiwa sana na kuungwa mkono na watu walewale..... Kinachonishangaza ni kuwa watu hao hawaishi Tanzania, wao kazi yao ni kutupandikiza chuki na baada ya hapo nina uhakika hawataonekana tena wakati tumeshalikoroga.......... Kwa maana hiyo watatuacha tunalinywa wenyewe. Mtu kama Barubaru, kaja Tanzania kwa siku saba na kurudi huko anakoishi. Hivi unategemea mtu kama huyo tukijiingiza kwenye vita ya kidini atakuja tena..???? Nionacho ni kuwa atabaki huko aliko, na sana sana anatoa misaada ya mabomu kwa watakaokuwa upande wake, lakini distantly.

Tuacheni tunaojuwa hali halisi ya TZ tuichangie hoja hii. Hii habari ya kuifananisha TZ na nchi zinazoongozwa kiislamu muiache kabisa. Hatutumii sharia....bali sheria.

Ni wazi kabisa kwamba kinachoelezwa kwenye hiyo program ni kumchagua kiongozi ambaye ni MUISLAM anayebisha huyo hajaielewa hiyo program na ninamshauri akaisome tena.....

NINA UHAKIKA KUWA PAMOJA NA KWAMBA KINGUNGE ALIUPINGA WARAKA WA WAKATOLIKI, LAKINI AKIGOMBEA NAFASI YOYOTE WAISLAM HAWATAMPA KURA............. Sababu ni kuwa yeye si MUISLAM[/QUOTE]

Nilipo highlight!
Wewe ndio mnafiki kwelikwlei kwako wewe ni halali wakristo na waraka wao kumchagua mkristo lakini ni haramu waislamu na mwongozo wao kumchagua muislam..hypocracy

Huo mwongozo kwanini wewe unatoa tafsiri yako badala ya tafsiri zilizoko kwenye mwongozo..hakuna sehemu wanasema lazima awe muislamu??? ila awe muadilifu mwenye kufahamu historia ya Tanzania na matatizo ya jamii yetu..

Vita vya kidini watakaoanzisha ni maaskofu maana hata mambo ya waraka wameanza wao...elewa in every action there is equal and opposite reaction

tusijadili reaction kawaulize maaskofu kwanini walitaka kiongozi wao awe mkatoliki kwenye waraka wao?
 
Wewe ndio mnafiki kwelikwlei kwako wewe ni halali wakristo na waraka wao kumchagua mkristo lakini ni haramu waislamu na mwongozo wao kumchagua muislam..hypocracy

Huo mwongozo kwanini wewe unatoa tafsiri yako badala ya tafsiri zilizoko kwenye mwongozo..hakuna sehemu wanasema lazima awe muislamu??? ila awe muadilifu mwenye kufahamu historia ya Tanzania na matatizo ya jamii yetu..

Vita vya kidini watakaoanzisha ni maaskofu maana hata mambo ya waraka wameanza wao...elewa in every action there is equal and opposite reaction

tusijadili reaction kawaulize maaskofu kwanini walitaka kiongozi wao awe mkatoliki kwenye waraka wao?

Iko kazi kweli!

Unaji-contradict halafu unasema uongo bila aibu? Wapi katika waraka wa maaskofu waliposema kiongozi wao awe mkatoliki?

Amandla....
 
Kwa kusoma hii program ya mwongozo ya 2010 sioni kama kuna la kujadili.

Kwani yenyewe imejikita katika kuweka timeframe ya kutekeleza mwongozo hususan katika kutoa elimu ya uraia na haki za mpiga kura na kuchaguliwa kiongozi.

Imejikita zaidi katika kutekeleza na kutoa elimu ya uraia kwa waumini,

Sasa sioni kwa nini mnajadili sana.

nawashauri kila mtu anaweza kupata nakala yake na kuisoma aielewe kisha ndipo mlete debate.

Kama wao si wanafiki, wasingepinga waraka wa Wakatoliki. Kimsingi, ukisoma nyaraka zote mbili utaona mmoja unahusu maslahi ya Watz wote na mwingine maslahi ya Waislamu. Na huu wa maslahi ya Waislamu ndio unaopigiwa debe kuwa ni sahihi! Hivi kweli Watanzania tuna akili timamu?
 
KAMATI ya Siasa ya Shura ya Maimamu jana ilizindua programu ya Elimu ya Uraia yenye lengo la kutekeleza kwa vitendo waraka wake kuhusu uchaguzi mkuu wa mwakani.

Programu hiyo inataja sifa za msingi za chama na mgombea anayepaswa kuchaguliwa, masuala ambayo yalisababisha utata mkubwa baada ya nyaraka hizo za Shura ya Maimamu na Kanisa Katoliki kutolewa.

Mpango huo umo kwenye kitabu cha kurasa 76 na unataka Waislaam kuutekeleza kwa vitendo mwongozo uliozinduliwa na kamati hiyo Agosti 26 mwaka huu.

Programu hiyo ilizinduliwa jana kwenye Msikiti wa Mtoro jijini jijini Dar es Salaam na balozi wa zamani wa Tanzania katika nchi za Ufaransa na Italia, Abbass Sykes. Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo, Sykes alisema: "Nchi hii ni ya Watanzania wote, hakuna chama wala mtu mwenye hati miliki ya kutawala nchi hii."

Alisema kila chama na mtu bila ya kujali rangi, dini, kabila au mahali alipotoka, ana haki ya kuomba uongozi ili mradi awe amegombea nafasi ya uongozi kwa kufuata taratibu na sheria zilizopo.

Sifa za mgombea zinatajwa katika mada nambari tano ya kitabu hicho cha 'Elimu ya Uraia' kikitaja bayana sifa za mgombea anayetakiwa kupigiwa kura na Waislamu. "Awe kiongozi mwadilifu, anayejua matatizo makuu ya nchi na wananchi na mjuzi wa kuyatatua.

Matatizo makuu ya nchi ni udini, ubaguzi dhidi ya Waislaam au baadhi ya watu, rushwa, uchafuzi wa mkataba wa Muungano na ukosefu wa maadili kwa viongozi," inasema sehemu hiyo katika ukurasa wa 65.

"Awe kiongozi mwenye utashi wa kuwasaidia wananchi wote bila ya kujali tofauti zao, ajali zaidi maslahi ya umma kuliko ya chama chake, awe tayari kusaidia urejeshaji wa haki za wananchi zilizotaifishwa na serikali ikiwa ni pamoja na shule, ardhi na majengo."

Kitabu hicho kinaeleza kuwa ili mgombea apigiwe kura, anapaswa awe anafahamu haki na dhuruma walizofanyiwa Waislaam kwa kutotendewa haki sawa na dini nyingine na awe tayari kufuta makubaliano baina ya serikali na kanisa.

"Kiongozi huyo lazima awe tayari kutomwaga damu ya Waislaam kama ilivyotokea mara kadhaa katika misikiti, maandamano ya kudai haki au katika mahubiri ya kidini."

Kuhusu chama kinachostahili kuingia madarakani, kitabu hicho kinafafanua kuwa ni kile ambacho serikali yake haitawazuia Waislaam kufuata na kutangaza dini yao kwa uhuru na ambayo haitabadilisha sheria za Waislaam zinazohusu mambo ya mirathi, ndoa na talaka.

Kamati hiyo ya siasa ya Shura ya Maimamu, ilikumbushia migogoro mbalimbali baina ya serikali na Waislaam na kwamba chama kinachofaa ni lazima kiwe tayari kuunda tume huru kuchunguza mauaji ya Waislaam yaliyotokea miaka iliyopita.

"Kiwe chama ambacho serikali yake, itakubali kufanyika kwa uchunguzi wa mauaji ya waislaam katika maandamano ya kutetea Qur-an 1988, mauaji ya msikitini Morogoro 1994, mauaji ya kinyama msikitini Mwembechai 1998, mauaji ya imamu wa msikiti wa Mwembetanga 2001 na mauaji katika maandamano ya Waislaam ya kupinga kufungwa kwa mwenzao aliyesema Yesu si Mungu mwaka 2001," inafafanua sehemu ya kitabu hicho.

"Kiwe chama ambacho serikali yake haitakuwa tayari kupokea maagizo, sheria na misamiati mipya dhidi ya Waislaam kama vile magaidi au siasa kali na kuwasikiliza masheikh na maimamu pamoja na viongozi wengine wa taasisi za kiislaam."

Awali katibu wa kamati ya siasa ya Shura ya Maimamu, Sheikh Ponda Issa Ponda alisema: "Muongozo (wa awali) umefanikiwa sana hasa mikoani, katika mikoa ya kanda ya kusini zaidi ya asilimia 90 ya viongozi walishinda katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji ni Waislaam wanaojielewa."

"Asilimia 75 ya wilaya zote za Tanzania zimefanya warsha na makongamano kuuchambua mwongozo, hotuba za Ijumaa zenye mwelekeo mmoja zimeanza jijini Dar es Salaam, Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislaam limetanga kura ya maslahi kuwa ajenda yao kuu 2010 na Taasisi 15 zimesaini makubaliano ya pamoja kuelekea uchaguzi mkuu."

Kwa mujibu wa sheikh Ponda, program mpya ya elimu ya uraia itatekelezwa katika mifumo ya machapisho, warsha, semina, makongamano, mikutano ya hadhara na hotuba kali za Ijumaa zenye mwelekeo mmoja katika miskiti yote nchini.

Source: Mwananchi

jamani,mbona kimya sana ndugu zangu........afu nadhani Sheikh Yahya anapingana na maoini yenu, tafadfhali tunaomba msimamo wenu pia,kama aliyotuambia Sheikh Yahya ni kweli..
 
Back
Top Bottom