Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limetoa wito kwa Jeshi la Polisi nchini kuchunguza kwa haraka na kwa makini taarifa za kutekwa kwa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey polepole
Wito wa jukwaa hilo umetolewa Oktoba 7, 2025 na Mwenyekiti wake Deodatus Balile kupitia taarifa iliyotolewa, ikieleza zaidi kwamba ikiwa ni masuala ya kisiasa viongozi wa siasa wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa watanzania
"Tunaamini kama ni siasa basi wafuasi wa vyama vya siasa na viongozi wao wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa Watanzania kwa kushindanisha hoja na si kuviziana, kuangushana au kutekana. kwa kauli koja tunasema utekaji haukubaliki Tanzania" imeeleza taarifa hiyo
TEF imeeleza zaidi kwamba kutokana na sifa ya muda mrefu kuwa Tanzania ni nchi ya amani, si vyema kuona sifa hiyo inapotea kutokana hali ya sasa kiusalama
"Kwa vyovyote iwavyo sisi Jukwaa la Wahariri Tanzania, tunasema maisha na uhai wa Watanzania wenzetu ni kipaumbele namba moja kwa amani ya Taifa letu, amani ni tunda la haki", imebainisha taarifa hiyo
Aidha jukwaa hilo limekiri kuona taarifa za kutekwa kwa Balozi huyo mstaafu, huku likibainisha kwamba jamii haijasahau matukio ya mauaji na utekaji wa baadhi ya watu mbalimbali nchini
Soma pia:
Chanzo: Jambo TV
Wito wa jukwaa hilo umetolewa Oktoba 7, 2025 na Mwenyekiti wake Deodatus Balile kupitia taarifa iliyotolewa, ikieleza zaidi kwamba ikiwa ni masuala ya kisiasa viongozi wa siasa wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa watanzania
"Tunaamini kama ni siasa basi wafuasi wa vyama vya siasa na viongozi wao wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa Watanzania kwa kushindanisha hoja na si kuviziana, kuangushana au kutekana. kwa kauli koja tunasema utekaji haukubaliki Tanzania" imeeleza taarifa hiyo
TEF imeeleza zaidi kwamba kutokana na sifa ya muda mrefu kuwa Tanzania ni nchi ya amani, si vyema kuona sifa hiyo inapotea kutokana hali ya sasa kiusalama
"Kwa vyovyote iwavyo sisi Jukwaa la Wahariri Tanzania, tunasema maisha na uhai wa Watanzania wenzetu ni kipaumbele namba moja kwa amani ya Taifa letu, amani ni tunda la haki", imebainisha taarifa hiyo
Aidha jukwaa hilo limekiri kuona taarifa za kutekwa kwa Balozi huyo mstaafu, huku likibainisha kwamba jamii haijasahau matukio ya mauaji na utekaji wa baadhi ya watu mbalimbali nchini
Soma pia:
- Humphrey Polepole adaiwa kutekwa usiku wa kuamkia leo Oktoba 6
- Mama Polepole: Nirudishieni mwanangu akiwa hai au amekufa, alikuwa mtoto wa kipekee
- Wakili Peter Kibatala, azitaka mamlaka za usalama nchini kutoa hali ya usalama ya Polepole inajulikana na kuwekwa wazi kwa umma
Chanzo: Jambo TV