Wahariri (TEF) Waitaka Polisi Kuchunguza alipo Polepole

Wahariri (TEF) Waitaka Polisi Kuchunguza alipo Polepole

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limetoa wito kwa Jeshi la Polisi nchini kuchunguza kwa haraka na kwa makini taarifa za kutekwa kwa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey polepole

‎Wito wa jukwaa hilo umetolewa Oktoba 7, 2025 na Mwenyekiti wake Deodatus Balile kupitia taarifa iliyotolewa, ikieleza zaidi kwamba ikiwa ni masuala ya kisiasa viongozi wa siasa wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa watanzania

‎"Tunaamini kama ni siasa basi wafuasi wa vyama vya siasa na viongozi wao wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa Watanzania kwa kushindanisha hoja na si kuviziana, kuangushana au kutekana. kwa kauli koja tunasema utekaji haukubaliki Tanzania" imeeleza taarifa hiyo

‎TEF imeeleza zaidi kwamba kutokana na sifa ya muda mrefu kuwa Tanzania ni nchi ya amani, si vyema kuona sifa hiyo inapotea kutokana hali ya sasa kiusalama

‎"Kwa vyovyote iwavyo sisi Jukwaa la Wahariri Tanzania, tunasema maisha na uhai wa Watanzania wenzetu ni kipaumbele namba moja kwa amani ya Taifa letu, amani ni tunda la haki", imebainisha taarifa hiyo

‎Aidha jukwaa hilo limekiri kuona taarifa za kutekwa kwa Balozi huyo mstaafu, huku likibainisha kwamba jamii haijasahau matukio ya mauaji na utekaji wa baadhi ya watu mbalimbali nchini

Soma pia:

1760000463370.png


Chanzo: Jambo TV
 
Hii taka taka ya kuitwa TEF imeshakuwa small branch ya FISIEMU na hakuna mwenye imani nayo tena, tamko lolote watakalolitoa kuhusu hali ya kisiasa hapa nchini obvious ni tamko la kimikakati lenye mlengo wa kusaidia watawala.
 
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limetoa wito kwa Jeshi la Polisi nchini kuchunguza kwa haraka na kwa makini taarifa za kutekwa kwa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey polepole

‎Wito wa jukwaa hilo umetolewa Oktoba 7, 2025 na Mwenyekiti wake Deodatus Balile kupitia taarifa iliyotolewa, ikieleza zaidi kwamba ikiwa ni masuala ya kisiasa viongozi wa siasa wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa watanzania

‎"Tunaamini kama ni siasa basi wafuasi wa vyama vya siasa na viongozi wao wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa Watanzania kwa kushindanisha hoja na si kuviziana, kuangushana au kutekana. kwa kauli koja tunasema utekaji haukubaliki Tanzania" imeeleza taarifa hiyo

‎TEF imeeleza zaidi kwamba kutokana na sifa ya muda mrefu kuwa Tanzania ni nchi ya amani, si vyema kuona sifa hiyo inapotea kutokana hali ya sasa kiusalama

‎"Kwa vyovyote iwavyo sisi Jukwaa la Wahariri Tanzania, tunasema maisha na uhai wa Watanzania wenzetu ni kipaumbele namba moja kwa amani ya Taifa letu, amani ni tunda la haki", imebainisha taarifa hiyo

‎Aidha jukwaa hilo limekiri kuona taarifa za kutekwa kwa Balozi huyo mstaafu, huku likibainisha kwamba jamii haijasahau matukio ya mauaji na utekaji wa baadhi ya watu mbalimbali nchini

Soma pia:



Chanzo: Jambo TV
20251009_110439.jpg
 
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limetoa wito kwa Jeshi la Polisi nchini kuchunguza kwa haraka na kwa makini taarifa za kutekwa kwa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey polepole

‎Wito wa jukwaa hilo umetolewa Oktoba 7, 2025 na Mwenyekiti wake Deodatus Balile kupitia taarifa iliyotolewa, ikieleza zaidi kwamba ikiwa ni masuala ya kisiasa viongozi wa siasa wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa watanzania

‎"Tunaamini kama ni siasa basi wafuasi wa vyama vya siasa na viongozi wao wanapaswa kupewa mafunzo ya kushiriki siasa zenye lengo la kuleta maisha bora kwa Watanzania kwa kushindanisha hoja na si kuviziana, kuangushana au kutekana. kwa kauli koja tunasema utekaji haukubaliki Tanzania" imeeleza taarifa hiyo

‎TEF imeeleza zaidi kwamba kutokana na sifa ya muda mrefu kuwa Tanzania ni nchi ya amani, si vyema kuona sifa hiyo inapotea kutokana hali ya sasa kiusalama

‎"Kwa vyovyote iwavyo sisi Jukwaa la Wahariri Tanzania, tunasema maisha na uhai wa Watanzania wenzetu ni kipaumbele namba moja kwa amani ya Taifa letu, amani ni tunda la haki", imebainisha taarifa hiyo

‎Aidha jukwaa hilo limekiri kuona taarifa za kutekwa kwa Balozi huyo mstaafu, huku likibainisha kwamba jamii haijasahau matukio ya mauaji na utekaji wa baadhi ya watu mbalimbali nchini

Soma pia:



Chanzo: Jambo TV
Mzee Pascal Mayalla aliwahi kutuambia humu 'serious media' inaweza kuwatambua 'wasiojulikana' wanaoteka watu ila mpaka Leo hiyo 'serious media' haijawatambua hao jamaa.

Hili la Balozi mstaafu kupotezwa ni aibu na fedheha kwa hii nchi.
 
Mzee Pascal Mayalla aliwahi kutuambia humu 'serious media' inaweza kuwatambua 'wasiojulikana' wanaoteka watu ila mpaka Leo hiyo 'serious media' haijawatambua hao jamaa.

Hili la Balozi mstaafu kupotezwa ni aibu na fedheha kwa hii nchi.
Msimamo huo bado naushikilia, hii maana yake Tanzania bado hatuna media za seriousness ya kiwango hicho
P
 
Msimamo huo bado naushikilia, hii maana yake Tanzania bado hatuna media za seriousness ya kiwango hicho
P
Mbona kuna miaka hapa katikati(kabla ya awamu ya 5) mlionekana mpo serious mpaka kuitwa Mhimili wa '4' au ilikuwa moto wa mabua tu?..
 
Mbona kuna miaka hapa katikati(kabla ya awamu ya 5) mlionekana mpo serious mpaka kuitwa Mhimili wa '4' au ilikuwa moto wa mabua tu?..
Kila zama na zama zake, kila awamu na kitabu chake!sasa ni awamu ya mama, media zote ni Mama Mama,na mambo ni mwendo wa kimama mama!
P
 
Kila zama na zama zake, kila awamu na kitabu chake!sasa ni awamu ya mama, media zote ni Mama Mama,na mambo ni mwendo wa kimama mama!
P
Okay!... nimekuelewa Kumbe nyie media sio mhimili wa 4 wenye maadili au misingi mnayosimamia isipokuwa nyie ni kama wacheza Ngoma mnaocheza kulingana na mdundo anaochagua mpigaji.
 
Back
Top Bottom