Wahanga wa Mlipuko wanalala wapi leo!

Petu Hapa

JF-Expert Member
Jan 2, 2008
714
55
Kunawale wanaoendelea kutafuta sababu ya janga la mlipuko ambalo ni jambo la msingi kabisa. Lakini hali halisi ni kwamba kunawatu ambao wameathirika na mlipuko huo, ambao hawatakuwa na mahala pa kulala kwa siku chache zijazo, wengine watakuwa hawana chakula, wakati wengine watakuwa wamepoteza mali na ndugu zao ama watoto wato. Jambo la msingi ni kufikiria hawa watu watalala wapi, watakula nini na familia zao zisipoteana na serikali kuonyesha uwezo wake wa kuwalinda wananchi wake ikishirikiana na taasisi mbalimbali za kijamii!

Maoni yangu

Vyombo vya kijamii pamoja na serikali zile za mitaa ikishirikiana na watu binafsi watoe maeneo machache ambayo watu watalala humo! Watu wajitolee magodoro, vyakula, na maswala ya afya ili watu waishi humo kwa siku chache mpaka hali itakapokuwa shwari. Hii itasaidia familia kutokupotezana. Serikali kuanza kufanya taathimini ya maafa na kufanyia eneo uchunguzi wa kina, na watu wenyewe kuwa na imani kwamba watakuwa salama!

Makumbi ya kuwaweka wahanga yapo mengi tu ni yale tunayofanyia harusi! hilo ni wazo tu ndugu zangu! Maana akili yangu hanipi picha kabisa watu kuanza kuhangaika wapi watalala ama kula. Watoto wadogo kutangatanga bila mwelekeo. Hofu hii sio ndogo ndugu zangu, na kama jamii tunatakiwa tuwasaidie waliopata janga hili maana sio tu watu hawana chakula ama malazi ila kunawatu hata akili zao zitaathirika hasa pale watakapoachwa mitaani kujilinda wenyewe.

Ile bajeti yetu ya maafa ndio ifanye kazi sasa!
 
bado nauliza hawa wahanga wanalala wapi! Ukiacha serikali juhudi ambazo inazifanya, je wananchi mnakumbana na hao wananchi tunawasaidiaje? Wewe unafanya nini!
 
kuna makazi ya muda yametolewa katika kituo cha polisi Mbagala
 
Safi sana! Kituo cha mbagala kinauwezo wa kuchukua watu wangapi! Lakini mbona taarifa zimeonya watu wakae mbali na maeneo hayo!
 
This is Kikwete's Katrina moment.

Wa organise majumba makubwa yote, PTA Hall, Diamond Jubilee Hall, pamoja na viwanja vya wazi kama uwanja wa taifa (kama ni mbali vya kutosha)etc etc kufanya msaada.

Pia huu ni wakati wa wakazi wa Dar kuonyeshana mshikamano kwa kuhifadhi ndugu zetu hawa, ingawa tahadhari pia inatakiwa kuchukuliwa. In any case wenye ndugu wenye uwezo wa kuwasitiri wajibanze kwa ndugu zao mpaka maafa haya yatakapopita.
 
Last edited:
Brurary,

hapo ndicho nachokisema! serikali itumie wakati huu kuonyesha userikali wake! Actually, ningekuwa political strategist wa kikwete! Ningemshauri hii ndio nafasi ya kuact!
 
Hiki ndicho nilichosema kwenye thread nyingine nilitegemea tayari keshakwenda kwenye tukio na kuwaahidi wananchi maradhi na chakula kama mwezi hivi wakati serikali yake inataka kutumia mabilioni kuwalipa vidia, kwani bima ya twin tower haiwezi kuamishwa na kuingizwa kwenye mabomu ya mbagara
 
Hivi huyu Waziri Mkuu PINDA yuko wapiiii? naona sikumuona kuwa karibu na Wahanga wa Mabomu au hana habariiii? au Kasafiri, ikiwa hakusafiri na yuko DODOMA ni Bora Kesho akatangaza Kujiuzulu kwa sababu hana maana, niliemuona yuko mbele ni LUKUVI, KIMBISA hawa wako na Watu, Rais wetu tunajuwa kuwa yuko ARUSHA Mkutanoni akiwa na Wageni wa Kitaifa.

Waziri Mkuu kama alikuwa dodoma pamoja na Wabunge wapenda posho wa Mkowa wa Dar wakitulia kimya na wao Wajiuzulu kama vile tunavyomtaka PINDA kuwachia ngazi.

Maafa ni makubwa tena sana kiasi ambacho Waziri wa Ulinzi na Naibu wake pamoja na Mwamuyange nao Wajiuzulu kabla ya Tume itakayo Undwa kutizama chanzo cha maafa Makubwa na ya Kutisha kwa Taifa kwani kunusurika kwa Mlipuko Mkubwa kumeinusuru Dar Kuangamia pamoja navilivyomo.

Naungana na wenzangu wote tuwachangie wenzetu Masikini hawa kwa hali na umali hasa katikakipindi hiki kigumu kilichowakuta.
 
You made a very good point, but this should not be a problem to the government because is taxpayers money. Being front line to issues like this is ok but the government need to demonstrate to handle some emergence like this.
 
Back
Top Bottom