Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,399
- 40,295
Wahahitajika vijana watano kwa ajili ya kutembeza nguo, viatu, mabegi ya mitumba maeneo mbalimbali mkoani Arusha. Aina ya kazi iko hivi:-
- Asubuhi utakabiziwa mzigo kutokana na uwezo wako, na utapewa malengo ya mauzo; kama utauza zaidi, kile kinachozidi ndio malipo yako; mfano suruali ya 5,000 ukauza 10,000, ile 5,000 iliyozidi ni ya kwako. Cha muhimu utimize malengo.
- Kazi hii inawafaa hasa wale wapambanaji wa kweli wa maisha wasiokuwa na aibu
- Kama malazi yatahitajika, ofisi inaweza kuwafikiria kwenye majengo yake.