bht
JF-Expert Member
- May 14, 2009
- 10,336
- 1,862
Mzee sio utani,
Haya mambo "huria" na "Ubinafsi" tulipaswa kwanza tujifunze kwa wale waliotutaka tufanye. Wenzetu walioendelea wana mfumo mzuri wa kudhibiti ujinga kama huu.
Hivi unategemea nini kama Mhadhiri wa chuo kikuu huria anaishi maisha huria, mhadhiri kasoma kiujanja, ujanja tu kwa kuiba mitihani na kudesa!.
Huyo hawezi kuacha tabia yake. Vigezo vinavyotumika katika vyuo vyetu kupata wahadhiri ni "just awe" na Upper second na tofauti na walimu wa kawaida wanavyuo vya ualimu, wanajifunza pia maadili ya kazi na jinsi ya kufundisha.
Hizi digrii za "chupi" na "rushwa" siku hizi zimeua kabsaaa taaluma.
Nimewahi kufanya kazi na jamaa ana "first class" ya chuo kimoja binafsi (...) lakini mkichwa ni "o" kabisa, anaangalizia mpaka kuandika barua ya kiofisi. Hawezi kujieleza kwa kingereza wala kiswahili, kujibu hoja kwenye jalada hatakutafuta kokote ulipo hata kama umesafiri atasubiri mpaka hurudi.
hapo ndipo tulipofikishwa na mfumo usioleweka wa elimu yetu!!! enrollment uchwara mtupu, lecturers uchwara tu, degree uchwara matokeo yake ndo haya. Vyuo vinapotezA hadhi.
tunapenda njia fupi sie duh!! hata pasipostahili.