Wagombea warushiana matusi Marekani

Wagombea warushiana matusi Marekani

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,586
Reaction score
28,748
160311011452_trump_rubio_cruz_kasich_640x360_ap_nocredit.jpg


Wagombeaji wawili wa Urais wa chama cha Republican nchini Marekani wamegombana vikali na kurushiana matusi juu ya wake zao.
Seneta wa Texas, Ted Cruz, amemlaumu mpinzani wake, mfanyabiashara Donald Trump kwa kuzusha uvumi kuwa yeye alikuwa mzinifu na kumdanganya mkewe, Heidi.

Bwana Cruz alisema uvumi huo ni takataka na akasema kuwa anaelewa kuwa uvumi ulianzishwa na Bwana Trump ambaye alisema hastahili kuwa Rais.
Bwana Trump alisisitza kuwa hakuhusika vyo vyote na uvumi huo.

Mapema juma hili, Bwana Trump alimlaumu Seneta Cruz kwa kuweka picha za mkewe, Melania, akiwa uchi kwenye mtandao ili kumharibia sifa.

Source: BBC
 
Back
Top Bottom