Kenya 2022 Wagombea Binafsi Waivuruga Kenya

Kenya 2022 General Election

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,215
3,587
Dhana ya ugombea binafsi ni tamu masikioni lakini chungu kutekelezeka. Kenya yenye sheria hiyo imetoa ushahidi, funzo na alarm kwamba ni dhana ngumu kutekelezeka baada ya IEBC na wapigakura kuchanganyikiwa na kutamani ugombeaji kupitia mfumo wa vyama. Takwimu za IEBC zilizotolewa jana kwa umma zinaonyesha kwamba kuna zaidi ya wagombea binafsi 1500 na wale wa kiti cha urais wanafika 47.

Msingi wa hofu ni nini:-

1. Wamegundua kuwa wapigakura wamechanganyikiwa kwa kushindwa kujuwa historia za wagombea binafsi hao Kenya kutokana na idadi hiyo kubwa na inayozidi kuongezeka kila uchao; ili kura za wananchi zisikose target.

2. IEBC imepata kazi ngumu ya kuwafanyia vetting idadi hiyo ambayo inazidi kuongezeka.

3. Kuna hatari ya matapeli kugombea (kumbuka nahau ile kwamba: hakuna ajuaye kiungurumacho kwenye kifua cha Simba)

4. Kuna hatari ya Mahakama kupokea kesi nyingi za kuchezeana rafu na kwamba mzigo wa idadi kubwa ya kesi za uchaguzi huenda ikavunja rekodi na kuipa IEBC gharama kubwa za chaguzi za marudio kama Mahakama itaamuru hivyo.

5. Kuna sintojuwa kwamba matapeli wenye njaa wanaweza kutumia mwanya wa ugombea binafsi ili wakikosa ushindi basi wanafungua madai ya kuhujumiwa na kudai ama kupewa ushindi au fidia ya gharama za kuendesha kesi (ujasiriamali wa uchaguzi).

6. Kuna hofu kuwa baadhi ya wagombea binafsi wanatumia mwanya huo kama chambo/mtego kwa wale wenye vyama ili kwamba wenye vyama wanapohisi hawana wafuasi wengi katika ngome fulani basi watoe ela ndefu kwa wagombea binafsi ili wawaachie wafuasi wao kwenye ngome hizo.

7. Wananchi na asasi husika na uchaguzi wamekubaliana kwamba kumbe mfumo wa ugombeaji kupitia tiketi za vyama ni mzuri kwa maana chama ndicho kwa niaba ya wapigakura kinamfanyia vetting ya msingi (kabla ya ile ya IEBC) mgombea na kumuuza kwa wapigakura.

NB.
Kenya hivi sasa mpigakura ni bidhaa-adimu, vyama ni vitega uchumi-adhimu.

Kenya imesajili vyama 90 na takriban 40 maombi yao yako mezani kwa Msajili wa Vyama vya Siasa. County ya Mlima Kenya inaongoza kwa idadi kubwa ya vyama vya siasa 10 vikubwa na vidogovidogo zaidi ya 10.

Mwaka 2007 Kenya ilikuwa na vyama vya siasa 160 vyenye usajili wa kudumu.

Kuna maeneo Kenya ambayo chama cha kisiasa kiko hai kwenye wilaya/county moja tu au tarafa/division moja tu au kata/sub-division moja tu.

Hii ukichanganya na ukabila inafanya Kenya kuwa na biashara ya binadamu kama ya utumwa vile.

Wasomi wengi waliokosa ajira wameingia kwenye biashara ya siasa ya kuanzisha na kusajili vyama na kurubuni wasio na ajira kuwa wafuasi wao kwa malengo hayo ya kuvuna pesa za ama ruzuku au za uchaguzi ambapo wengine hawagombei lakini wanaweka wafuasi wao sokoni kwa ajili ya vyama vikubwa kuwanunua au kumuahidi mwenye chama cheo katika serikali endapo chama-mnunuzi kitashinda na kuunda serikali.

Wenzetu wame-advance.
 
Chukulia Rais kashinda mgombea binafsi afu vyama vimeshinda wabunge,huyo mtu anaongozaje Nchi? Ajenda zake zitapitaje?

Harafu huu ni ujinga,mgombea binafsi atasukuma vipi ajenda zake binafsi?

Sio kila kitu ni cha kuiga.
Ikiwa hivyo hua president ana join side yenye anataka (mara nyingi yenye wabunge wengi na interest sawa) na kutengeneza serikali ya makubaliano na kuteua baadhi ya viongozi wa juu wa serikali kutoka kwa hicho chama so anaendelea kama kawaida.
 
lini tutawafikia Kenya nasisi?mbona kama nishavutiwa hivi? kumenoga huko kwa wavaa suti na tai huku mfukoni kuna kitambaa cha kufuta jasho tu!!

Ila for now sisi watz tuko bize kuwapiku Kenya kiuchumi kupitia Mama Samia Royal Tour, Mt Kilimanjaro na Wildebeests viko Tanzania si Kenya, umeme mpya toka Nyerere Dam, Bomba la mafuta to Uganda na SGR yetu kuchukua masoko ya nchi za maziwa makuu!!

siasa za ushindani Mwendazake alizizika tz! kwasasa hatuhitaji hizo ishu!!

Wakenya tafadhali endeleeni na siasa siku mkiamka mtakuta Watz tuna pesa nyingi tunasema jamani Wakenya tukae mezani tuuzieni Nairobi , kwani bei gani ati!

willing to sell willing to buy si ndio sera yenu ya manunuzi! tunawajua mnavyopenda pesa mtatuuzia Nairobi 😀😀
 
Ikiwa hivyo hua president ana join side yenye anataka (mala nyingi yenye wabunge wengi na interest sawa) na kutengeneza serikali ya makubaliano na kuteua baadhi ya viongozi wa juu wa serikali kutoka kwa hicho chama so anaendelea kama kawaida.
Wabunge wengi na interest sawa ndio nini? Ya Chisekedi wa DRC uliyaona?
 
Ila for now sisi watz tuko bize kuwapiku Kenya kiuchumi kupitia Mama Samia Royal Tour, Mt Kilimanjaro na Wildebeests viko Tanzania si Kenya, umeme mpya toka Nyerere Dam, Bomba la mafuta to Uganda na SGR yetu kuchukua masoko ya nchi za maziwa makuu!!
Hakuna utalii kukuzwa na filamu bila shirika imara la ndege. ATCL ni kama iko ICU, KQ imechukuwa SAA.

KQ ina safari za kimataifa 41.

SAA ina safari za kimataifa 38.

Jumla KQ ambayo imechukuwa SAA ina safari 79 za kimataifa. ATCL inazo ngapi?

KQ imeweka sharti kwamba ukipanda ndege zake tokea duniani kuja EAC lazima kwanza ushukie JKIA. Wageni watapokuja JNIA tokea JKIA watakuwa wamebakiza chenji tu mfukoni kutuletea baada ya kukamuliwa kenya.
 
Chukulia Rais kashinda mgombea binafsi afu vyama vimeshinda wabunge,huyo mtu anaongozaje Nchi? Ajenda zake zitapitaje?

Harafu huu ni ujinga,mgombea binafsi atasukuma vipi ajenda zake binafsi?

Sio kila kitu ni cha kuiga.
Let democracy prevail, RAIS atajua la kufanya akishindwa uchauzi unatishwa tena, ndiyo demokrasia
 
Sipati picha karatasi za kupigia kura zitakuwa ni kitabu chenye kurasa. mtu atapata tabu Sana kutafuta jina la mgombea wake.
Kuna hatari ya kupata viongozi wabovu (kwenye msafara wa mamba wengi kenge hujipenyeza)

Watu wanaoishi na ulemavu hasa wa macho uchaguzi huu utawa-stigmatize kwa utaratibu huu wa mgombea binafsi.

Ila kwa ukomavu na activeness ya demokrasia hii Kenya inaelekea pazuri na itakuwa Mwl wa demokrasia Afrika kwa kuwa watakuwa wametangulia kuonyesha njia.

Ninachoona ni kwamba system waliyoijenga itafika sehemu ita-crash alafu watatafuta ergonomic ya kuondoka kwenye mkwamo huo na hiyo ergonomic itakuwa role-model ya Afrika.

Si unaona walivyofanikiwa kwenye mfumo mpya wa county (ugatuzi) ambao zamani haukuwepo, sasa kuna even-development (maendeleo sawia nchini)

Aidha, wame-overhaul education system yao toka 7-4-2-3 kama ya Tz kwenda 8-4-4 na sasa kwenda CBC 2-3-3-3-3-3.
 
Kuna hatari ya kupata viongozi wabovu (kwenye msafara wa mamba wengi kenge hujipenyeza)

Watu wanaoishi na ulemavu hasa wa macho uchaguzi huu utawa-stigmatize kwa utaratibu huu wa mgombea binafsi.

Ila kwa ukomavu na activeness ya demokrasia hii Kenya inaelekea pazuri na itakuwa Mwl wa demokrasia Afrika kwa kuwa watakuwa wametangulia kuonyesha njia.

Ninachoona ni kwamba system waliyoijenga itafika sehemu ita-crash alafu watatafuta ergonomic ya kuondoka kwenye mkwamo huo na hiyo ergonomic itakuwa role-model ya Afrika.

Si unaona walivyofanikiwa kwenye mfumo mpya wa county (ugatuzi) ambao zamani haukuwepo, sasa kuna even-development (maendeleo sawia nchini)

Aidha, wame-overhaul education system yao toka 7-4-2-3 kama ya Tz kwenda 8-4-4 na sasa kwenda CBC 2-3-3-3-3-3.
Naona unaifuatilia siasa za Kenya kwa ukaribu sana.
 
tuendelee kuwasifia wakenya wasiufute huyo mpango wao ili wawe bize na siasa sie uchumi
FDI ya Kenya ndiyo inayoongoza Tz ikifuatiwa na South Africa. Hata EAC Kenya ndiyo muwekezaji mkubwa, South Sudan ni 100% kwa sababu mataifa mengine yanaogopa vita pale lakini Kenya kajitoa muhanga na sasa amekamata South Sudan yote.

KQ ina safari duniani 41 na imenunua SAA ambayo in a safari duniani 38, jumla KQ ina safari duniani 79, ATCL inazo ngapi?
 
FDI ya Kenya ndiyo inayoongoza Tz ikifuatiwa na South Africa. Hata EAC Kenya ndiyo muwekezaji mkubwa, South Sudan ni 100% kwa sababu mataifa mengine yanaogopa vita pale lakini Kenya kajitoa muhanga na sasa amekamata South Sudan yote.

KQ ina safari duniani 41 na imenunua SAA ambayo in a safari duniani 38, jumla KQ ina safari duniani 79, ATCL inazo ngapi?
Ngoja waje ATCL watujuze
 
Back
Top Bottom