Wagombea 53/244(ubunge) na 1126/3754(udiwani) wa chama kimoja cha upinzani waenguliwa na tume ya uchaguzi nchini Tanzania

pingli-nywee

JF-Expert Member
Sep 16, 2015
11,923
13,344
Wagombea ubunge 18 wa chama tawala(CCM) waingia kwenye kinyanganyiro bila wapinzani. Mgombea urais wa chama cha upinzani, Chadema, Tundu Lisu amesema kwamba kuna njama ya kuhujumu upinzani baada ya 30% ya wagombea udiwani wa chama chake kutupiliwa mbali na tume ya uchaguzi kwenye usajili.

Aliongeza kwamba wagombea ubunge 53 pia kati ya 244, hawakuorodheshwa na tume ya uchaguzi, huku hatma yao ikiwa ya sintofahamu. Taswira ni hiyo hiyo kwenye chama cha upinzani ACT.

Ambayo mgombea urais wake Bernard Membe alieleza kusikitishwa kwake na habari kwamba hakutakuwa na upinzani wowote dhidi ya wagombea ubunge wa CCM kwenye maeneo bunge 18.

Hivi majirani sheria zenu zipoje kwenye suala hili? Rufaa za wagombea walioenguliwa lazima ziwasilishwe kwa mbwa mwitu huyu huyu aliyevalia ngozi ya kondoo? Au ni ruksa kuwasilisha malalamishi mahakamani kama ilivyo nchini Kenya?

Tanzanian opposition alleges irregularities in candidates' enrollment
 
Demokrasia ya Watz ni ya kipekee dunia hii, wanaijua wenyewe. CCM wamepanic balaa, hawakutegemea muziki wanaokumbana nao, japo nahisi kinachowaponza walijitakia wenyewe maana waliwaminya upinzani na kukataza mikusanyiko yoyote ya wapinzani kwa kipindi cha miaka miine, wangeshauriwa vizuri wawaachie wapige makelele hadi wachokwe na wananchi, ila sasa unawaachia miezi michache kabla uchaguzi, hapo wanapokelewa na wananchi kama viongozi wenye mawazo mbadala.

Sasa hivi CCM wanatapatapa na wana hasira balaa, wameanza kutumia chopper, kitu ambacho hawakukusudia maana wlijiaminisha kwamba hata hawahitaji kufanya kampeni. Japo Lissue inawezekana aisiwanyang'anye tonge mdomoni, lakini atawaachia makovu ya kudumu hawa kijani maana wamepoteana.
 
Uchaguzi 2020 - Dar: Helkopta ya Kampeni ya Tundu Lissu, yanyimwa kibali cha kutumia anga, ni baada ya kuomba kibali hapo jana Alafu wanatumia wao ila ikifika kwa upinzani mamlaka inamnyima Tundu Lisu kibali. :D
Demokrasia ya Watz ni ya kipekee dunia hii, wanaijua wenyewe. CCM wamepanic balaa, hawakutegemea muziki wanaokumbana nao, japo nahisi kinachowaponza walijitakia wenyewe maana waliwaminya upinzani na kukataza mikusanyiko yoyote ya wapinzani kwa kipindi cha miaka miine, wangewaachia wapige makelele hadi wachokwe na wananchi, ila sasa unawaachia miezi michache kabla uchaguzi, hapo wanapokelewa na wananchi kama viongozi wenye mawazo mbadala.

Sasa hivi CCM wanatapatapa na wana hasira balaa, wameanza kutumia chopper, kitu ambacho hawakukusudia maana wlijiaminisha kwamba hata hawahitaji kufanya kampeni. Japo Lissue inawezekana aisiwanyang'anye tonge mdomoni, ila atawaachia makovu ya kudumu hawa kijani maana wamepoteana.
 
Back
Top Bottom