Wafuatao wajiuzulu sasa

Wafuatao wajiuzulu sasa

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Katika Mkutano wa watanzania wapigania Katiba bora uliofanyika Viwanja vya Kibanda Maiti-Zanzibar,mambo yamekuwa mambo. CCM na Serikali yake imedhalilishwa,imeumbuliwa na kuchafuka. Hata Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar nayo iko hatarini kutawanywa na upepo mkali wa Katiba mpya. Mkutano husika ulihudhuriwa na kuhutubiwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa nchini.Lakini,Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar naye alikuwepo.Ni Ndugu Abubakar Khamis Bakari.

Huyu ndiye ninayemlenga. Akiwa jukwaani Kibanda Maiti leo,Ndugu Bakari amesema kuwa Waziri Mathias Chikawe (Katiba na Sheria) na Naibu Spika Job Ndugai ni waongo na wamelipotosha Taifa.Walidai kuwa Wazanzibari walisikilizwa wakati wa mchakato wa kuandaa Muswada wa Sheria ya Katiba mpya uliopitishwa 'kimagumashi' Bungeni Dodoma. Ingawa hawa hawakutajwa na Waziri Bakari,lakini mkumbo wa 'uongo' wa kuwasikiliza Wazanzibari ni pamoja na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Idd pamoja na Waziri Mkuu Pinda.

Balozi Idd alialikwa Dodoma(inasemekana na Waziri Mkuu Pinda) kwenda kutamka kuwa Zanzibar imesikilizwa na Muswada umeandaliwa ipasavyo. Akafanya hivyo.Akapigiwa makofi sana.Wapinzani wakabezwa na kuonekana wakorofi. Leo,Waziri ambaye ni mhusika wa kwanza wa masuala ya Sheria Zanzibar (Ndugu BAKARI) amepasua jipu. Amekanusha.Ametofautiana na Makamu wake wa pili wa Rais wa Zanzibar-Balozi Idd.Amesema Zanzibar haikuwahi kusikilizwa.Muswada ni batili!

Kukanusha maneno ya Balozi Idd ni kuuharibu na kuusawajisha msimamo wa CCM na Serikali yake kuwa Wazanzibari walisikilizwa(na kutoa maoni yao juu ya Muswada huo). Ni kuiumbua Serikali na chama. Ni aibu kubwa kwa chama na Serikali.

Kama maneno ya Waziri Bakari hayatakanushwa kwa ushahidi mujarabu,nategemea wafuatao wajiuzulu mara moja:Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar,Waziri Mkuu, Waziri Chikawe,Mwanasheria Mkuu-Jaji Fredrick Mwita Werema na wote walioshupalia kuwa Wazanzibari walisikilizwa.Halafu,Rais Kikwete hana haja ya kusaini Muswada huo uliopitishwa 'kiujanjaujanja'. Na kama Waziri Bakari amesema uongo leo Viwanja vya Kibanda Maiti-Zanzibar,basi naye ajiuzulu haraka.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Hii Habari ni ya kweli???? Ngoja nisubiri nione uhakika wake kabla sijatoa maoni yeyote!
 
Tanzania Tanzania,nakupenda kwa moyo wote,ila mashetani ccm yamekupenda zaidi
 
Mzee Tupatupa hebu tupe uhakika wa hii Habari maana Kama hii Habari ni kweli basi Ccm imeisha! Maana Hawa wapinzani watashikilia hapo hapo!
 
Mzee Tupatupa hebu tupe uhakika wa hii Habari maana Kama hii Habari ni kweli basi Ccm imeisha! Maana Hawa wapinzani watashikilia hapo hapo!
Mkuu Ntuzu,Waziri Bakari alikuwepo na kusema nilichoandika
 
Last edited by a moderator:
Maji ukichanganya na mafuta,mafuta hubaki yameelea juu ya maji,ndio oungo ulivyo kama mafuta kwenye maji
 
Ccm ni majanga lakini kwa hawa wapinzani ccm wamekufa kibudu maana wanaachwa uchi mara zote.
 
Huu mziki sijui utaishaje jamani ila ccm hawana aibu walimzaliliza yule mzee balozi s.idd pale bungeni dodoma kumbe jamaa wameshachomeka vipengele kazaa kwenye mswaada kwa siri.
 
Hii Habari ni ya kweli???? Ngoja nisubiri nione uhakika wake kabla sijatoa maoni yeyote!

ni kweli tupu, mh abubakar (cuf)wazir wa katiba na sheria smz amesema wazi kibanda maiti.
 
Mkuu Ntuzu,Waziri Bakari alikuwepo na kusema nilichoandika

Huyu Waziri Bakari ni mwanachama chama gani? Cuf au Ccm? Kama atakua ni wa Ccm hizi serikali zitakua sasa zimeanza kupingana! Alafu hapa ndipo ninapouona ubovu wa Serikali ya mseto. Malim Seif yuko kimya tena Kama haoni! Kweli huu muafaka ulikua wa Malim Seif peke Yale! Kumbukumbu inaonesha Raila Odinga alichemka kutokana na mseto na pia Morgan Tsavangirai nae kachemka! Sasa zamu ya huyu Mh Malim Seif 2015 kuchemka! Ndio maana Hamadi Rashid alikua Sawa kumpinga na Cdm Walikua sawa kuukataa mungano wa kutengeneza kambi ya upinzani bungeni! Mh Lipumba unasemaje juu ya hili swala?
 
Last edited by a moderator:
huo msamiati 'kujiudhuru' hii nchi bado hatuufahamu vema !
...tutawafundisha mpaka watauelewa tu kama walivyoelewa maana halisi ya katiba mpya na mambo ya kujadili kwenye kuunda katiba...
 
Mkuu habari za lumumba bhana , Tambwe hiza hajambo ? Naam , baada ya salaam naomba nikwambie kwamba hakujawahi kutokea mwanaccm kujiuzuru kwa hiyari yake , labda tuwatimue .
 
Back
Top Bottom