wagagagigi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2014
- 890
- 983
Salaam,
Hii ni mara ya tatu naandika huu uzi lakini unafutwa sijui kwa nini!
Ujumbe ninaotaka kuufikisha kwenu ni kwamba wafanyakazi wa serikali Zanzibar na hasa Pemba wameelezwa na mabosi wao wa kazini kwamba ni lazima wamchague Magu pamoja na Mwinyi kwenye uchaguzi huu.
Kwa mujibu wa taarifa tulizonazo ambazo zimethibisha habari hizi kutoka vyanzo tofauti ikiwemo kutoka katika familia yangu binafsi zinasema kwamba; wafanyakazi kutoka wizara mbali mbali ikiwemo wizara ya afya Pemba, vikosi vya SMZ, JKU na wizara nyengine nyingi wameamriwa na mabosi wao bila haya wala soni kwamba ni lazima kura wapige CCM, yaani wapige kwa Magu na Mwinyi. Katika hali isio ya kawaida wafanyakazi wengi wa wizara tofauti wameorodheshwa information zao zikiwemo majina yao kamili, namba za kadi zao za kupigia kura, IDs zao zote za mzanzibari na zile za NIDA, vituo vya kupigia kura pamoja na namba zao za simu katika maofisi yao.
Habari hizi nimezithibitisha mimi binafsi baada ya kuzungumza na wafanyakazi waliokutwa na kadhia hio. Wengi wanasema kwamba wameshtushwa na kadhia hio na wanahofia vibarua vyao kuota majani iwapo wataamua kwenda kinyume na matakwa ya mabosi wao.
Kwa mara nyengine naomba huu uzi mnibakishie
Hii ni mara ya tatu naandika huu uzi lakini unafutwa sijui kwa nini!
Ujumbe ninaotaka kuufikisha kwenu ni kwamba wafanyakazi wa serikali Zanzibar na hasa Pemba wameelezwa na mabosi wao wa kazini kwamba ni lazima wamchague Magu pamoja na Mwinyi kwenye uchaguzi huu.
Kwa mujibu wa taarifa tulizonazo ambazo zimethibisha habari hizi kutoka vyanzo tofauti ikiwemo kutoka katika familia yangu binafsi zinasema kwamba; wafanyakazi kutoka wizara mbali mbali ikiwemo wizara ya afya Pemba, vikosi vya SMZ, JKU na wizara nyengine nyingi wameamriwa na mabosi wao bila haya wala soni kwamba ni lazima kura wapige CCM, yaani wapige kwa Magu na Mwinyi. Katika hali isio ya kawaida wafanyakazi wengi wa wizara tofauti wameorodheshwa information zao zikiwemo majina yao kamili, namba za kadi zao za kupigia kura, IDs zao zote za mzanzibari na zile za NIDA, vituo vya kupigia kura pamoja na namba zao za simu katika maofisi yao.
Habari hizi nimezithibitisha mimi binafsi baada ya kuzungumza na wafanyakazi waliokutwa na kadhia hio. Wengi wanasema kwamba wameshtushwa na kadhia hio na wanahofia vibarua vyao kuota majani iwapo wataamua kwenda kinyume na matakwa ya mabosi wao.
Kwa mara nyengine naomba huu uzi mnibakishie