Wafanyabiashara ya madini hawana tofauti na wa madawa ya kulevya, tutaraji vita kali na Serikali

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Serikali ilipoanzisha mapambano dhidi ya Madawa ya Kulevya, tumeshuhudia baadhi ya watu hata waliopo Serikalini wakigeuka kuwa maadui. Yesterday nimeweka mada hapa nikieleza kusikitishwa kwangu kwa jinsi vita ya Madawa ya Kulevya ilivyomharibu Nape Nnauye mpaka akafikia hatua ya kuasi mwajiri wake. Tumeshuhudia pia viongozi wa Serikali wakizushiwa kashfa mbalimbali kisa tu kuwa frontline katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya.

Sasa limekuja hili la majangili wanaoliibia taifa letu kwenye sekta ya madini. Nakumbuka shauku kubwa ya Watanzania kumtaka Rais azame huko kwenye madini ambako ndiko mapato mengi yanapotea. Watanzania wazalendo walimsihi Rais kutoangalia sura ya mtu katika kulinda Raslimali za Taifa.

Hata hivyo, kwa sasa naanza kuona dalili za watu kugeuza mapambano dhidi ya wahujumu uchumi kupitia madini kama vita ya mihadarati. Wamejipanga kuhakikisha Serikali haifanikiwi katika hili kwa vile wanajua dhahiri kuwa kufanikiwa kwa Serikali ni anguko la Wapinzani.

Kwa upande mwingine, waathirika wa mapambano hayo wakiwemo ACCACIA na GGM, wameanza pilika za kupata watetezi kupitia majukwaa ya siasa na mitandao ya kijamii. Hata hivyo, ni dhahiri kwamba wameshachelewa. Rais amechukua hatua stahiki kwa wakati muafaka.

CCM ya Magufuli hata mchanga utapanda thamani
 
Eleza sababu za kitaalamu kama mkurugenzi wa ACACIA achana na maswala ya ukataji viuno wa pale lumumba haya ni mambo ya kiuchumi na kitaalamu
 
Mkuu eliza bon punguza siasa kwenye mambo ya kitaalamu

Ni vyema wataalam wafanye shughuli zao bila siasa kuingiliwa


Km tunaibiwa kweli hata mimi namuunga mkono ngosha kwa hili
Ukiona Mkuu wa nchi anaongea basi ujue ameshalifanyia kazi. Tumuunge mkono Rais wetu. Tusimkatishe tamaa kama tulivyofanya kwenye vita dhidi ya madawa ya kulevya
 
Wazee wa kukurupuka, kwa hili pia mmekurupuka!!

Tafuta uzi huu.
Mkurugenzi wa Uendeshaji ACACIA aeleza sababu za kitaalamu kwanini wanasafirisha mchanga wa dhahabu.
 
Lakini nachokiona kwa uongozi huu hawa watu hawatashinda kamwe jpm kasimama imara kweli lazima wakae tu.
 
Vita ipi hyo ya madawa ya kulevya?muanzisha mada una uwezo mdogo sana wa kufikiria,mambo mengne hatuhitaji sisi kuambiwa tunahitaji kuona utendaji kazi,sasa huyo rais wako yy kila siku anataka kuonekana kwenye media,wanatakiwa wakae huko wizara husika na wataalam wapange vitu watambue hasara na faida za hlo katazo,hatupingi rais kutoa kauli za mwisho,bali kauli hzo ziwe wameshazifanyia kazi kwa kina ndio aje atueleze,hizi kauli za majukwaani bila tathmin ni hatar sana kwa mustakabali wa nchi....
 
Hizi ndo think tank zinazotegemewa.

Issue ya drugs ni one cartel was trying to eliminate another cartel. Mission impossible tayari. Washaelewana wamekaaa wamejadiliana Tahari, back door wanagonga glass. Wewe endelea kuimba mapambio tuu wenzio wanashare billions of drug money.

Back to concentrate issue.
Hakuna hata mtanzania mmoja anayepinga huo mchanga kuwekewa stop order. Issue ni approach je ni sahihi, matokeo ya hayo maamuzi tutaweza kukabiliana endapo kutakuwa na issue ya fidia ama la!!! Mfano ni issue ya Tanesco je hizo kesi hela za kulipa Nani atalipa kama sio tax payers money.

Guys tuache ushabiki tufanye kazi, kuhusisha vyama na issues za msingi kitaifa ni kunajisi Taifa.
 
Ukiona Mkuu wa nchi anaongea basi ujue ameshalifanyia kazi. Tumuunge mkono Rais wetu. Tusimkatishe tamaa kama tulivyofanya kwenye vita dhidi ya madawa ya kulevya
That is too pathetic. Blah blah blah zisizo na msingi. Vita haikatishwi na maneno. Huku ndio kunaitwa kuchelea mwana kulia. Mara zote linapofanyika jambo lenye walakini lazima mtangulize vijisababu kwa kuwa dhana mnayoisimamia imekosa mashiko.

Kama hazipo sababu zinazoeleweka kwa jambo lolote lazima kufeli kufuatie
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Serikali ilipoanzisha mapambano dhidi ya Madawa ya Kulevya, tumeshuhudia baadhi ya watu hata waliopo Serikalini wakigeuka kuwa maadui. Yesterday nimeweka mada hapa nikieleza kusikitishwa kwangu kwa jinsi vita ya Madawa ya Kulevya ilivyomharibu Nape Nnauye mpaka akafikia hatua ya kuasi mwajiri wake. Tumeshuhudia pia viongozi wa Serikali wakizushiwa kashfa mbalimbali kisa tu kuwa frontline katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya.

Sasa limekuja hili la majangili wanaoliibia taifa letu kwenye sekta ya madini. Nakumbuka shauku kubwa ya Watanzania kumtaka Rais azame huko kwenye madini ambako ndiko mapato mengi yanapotea. Watanzania wazalendo walimsihi Rais kutoangalia sura ya mtu katika kulinda Raslimali za Taifa.

Hata hivyo, kwa sasa naanza kuona dalili za watu kugeuza mapambano dhidi ya wahujumu uchumi kupitia madini kama vita ya mihadarati. Wamejipanga kuhakikisha Serikali haifanikiwi katika hili kwa vile wanajua dhahiri kuwa kufanikiwa kwa Serikali ni anguko la Wapinzani.

Kweli majabali wa madawa ya kulevya ogopa. Yana pesa ya kununua hata viongozi?

Kwa upande mwingine, waathirika wa mapambano hayo wakiwemo ACCACIA na GGM, wameanza pilika za kupata watetezi kupitia majukwaa ya siasa na mitandao ya kijamii. Hata hivyo, ni dhahiri kwamba wameshachelewa. Rais amechukua hatua stahiki kwa wakati muafaka.

CCM ya Magufuli hata mchanga utapanda thamani
 
That is too pathetic. Blah blah blah zisizo na msingi. Vita haikatishwi na maneno. Huku ndio kunaitwa kuchelea mwana kulia. Mara zote linapofanyika jambo lenye walakini lazima mtangulize vijisababu kwa kuwa dhana mnayoisimamia imekosa mashiko.

Kama hazipo sababu zinazoeleweka kwa jambo lolote lazima kufeli kufuatie
Serikali ya CCM imedhamiria. Nyie wapinzani subirini kama mtafanikiwa kutwaa dola ndo mfanye mnayoyataka
 
Back
Top Bottom