Wadhifa mpya wa mheshimiwa Edward N. Lowassa

Wadhifa mpya wa mheshimiwa Edward N. Lowassa

dala dala

Senior Member
Joined
Nov 16, 2011
Posts
106
Reaction score
105
Sina lengo la kutafuta umaarufu kwa kumzungumzia mtu ambaye kwa sasa anaonekana kuwa maarufu zaidi nchini Tanzania. Ana mvuto wa pekee na kajijengea heshima kubwa katika jamii. Anakubalika kila eneo. Bara na Visiwani; Wakristo na Waislamu, Wenye kumcha Mungu na Wapagani; Wazee na Vijana; Wanaume na Wanawake wote wanamkubali.

Hauhitaji kuwa msomi sana, wala tajiri sana ili kupata umaarufu kama alionao Ndg. Edward Nyoyai Lowassa. Naweza kusema bila ya wivu wala donge kuwa Mungu mwenyewe ndiye alimjalia Ndg Lowassa karama hii. Amefanya siasa kwa miaka mingi na tumeona mazuri na mapungufu yake na hivi karibuni alijikita katika kinyang'anyiro cha nafasi ya Urais lakini yaliyotokea sina haja wala sababu ya kuyajadili hapa lakini JIBU kila mmoja wetu analo kwa namna tulivyopokea matokeo.

Kinachonisukuma kuandika waraka huu; ni kuikumbusha jamii na Ndg. Lowassa kuwa Mungu ametujalia kumpata mtu ambaye anaweza kutumika vizuri katika kuleta mtangamano wa Kitaifa. Kwa karama yake ya kukubalika, binafsi, naona ni mtu sahihi wa kufanya usuluhishi yaani MEDIATION. Mwl. J.K. Nyerere alijaliwa kipawa hiki na alitumika kufanya usuluhishi wa ndani na nje ya nchi. Amefariki akiwa ni mpatanishi wa mgogoro wa Burundi. Ninaiona karama hiyo kwa Lowassa. Kwangu mimi hii ni hazina kubwa ambayo hatuna budi kuitumia kwa manufaa ya taifa letu.

Ninatambua wale ambao wanawaza siasa katika kila jambo wanaweza kuja na kejeli nyingi juu ya hiki, lakini ningependa mnipe mbadala wa Lowassa katika kukubalika katika jamii. Je, ni Pinda, Ben, Mzee Ruksa, JK, Salim, Mzee Wassira, au Warioba??? Kwangu mimi, Lowassa ndiye mtu pekee kwa sasa ambaye anaweza kuwaambia watu wenye jazba, tulieni na wakatulia, wenye silaha mikononi kuwa wekeni chini na watu wakaheshimu; anaweza kuwaambia wanaopigana tulieni na watu wakatii.

Baada ya maisha ya siasa, sasa ni wakati muafaka sana kwa Mzee Lowassa ukawatumikia Watanzania kwa njia hii ambayo kwangu mimi naona ina thawabu kubwa sana mbele za Mungu. Tuna migogoro ya muda mrefu hapa nchini mf. Wakulima na Wafugaji, Wachimbaji wa madini na Wawekezaji, misuguano ya kidini ya chini kwa chini nk. Migogoro hii kwa upande mwingine haihitaji mabavu au mkono wa Serikali bali watu wenye busara zao kama Ndg. Lowassa. Kama hili halitoshi, familia ya Lowassa imebahatika kuwa na Mama mwenye mvuto na ushawishi kuliko wanawake pengine wote kwa sasa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anajiheshimu, ana busara na anakubalika mno mno. Hii ni nyongeza kwa Mzee Lowassa katika kukamilisha kazi ambayo naiona imebaki katika kipindi cha maisha yake. Neno la Mungu linasema Heri Wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu!!

Mwenyezi Mungu akupe jicho la pekee Mzee Lowassa ili uweze kutumika kwa namna mpya na yenye manufaa makubwa kwa Taifa, Bara la Afrika na Dunia kwa ujumla. Mungu akuzidishie maisha marefu na wote wenye kuwaza na kupanga mabaya dhidi yako washindwe.
MAISHA MAPYA NDIYO HAYA MZEE LOWASSA, TUTUMIKIE KWA NAMNA HII.
 
Umeipenda sana familia lakini mchezo wa kuomba pesa ufe mtamfilisi baba wa watu.

Hata hivyo mtahani wa kwanza amefeli sijuhi wa upatanishi kama ataweza!
 
Umeipenda sana familia lakini mchezo wa kuomba pesa ufe mtamfilisi baba wa watu.

Hata hivyo mtahani wa kwanza amefeli sijuhi wa upatanishi kama ataweza!

Duh! kumbe wanampiga mizinga sana eee!
 
Amen ubarikiwe ukweli Mungu amempa karama ya pekee mkubali msikubali Edward Ngoyai Lowassa anabusara sana
 
Wakati mwingine kujifariji ni jambo jema, kuliko kulalamika lalamika na maandamano yasiyo na tija kwa Taifa.
 
Ana karama kwa majizi wenzake!

Msifie tu na wewe atakukumbuka!
 
Lowassa kwa sasa ni mchunga ng'ombe maarufu huko monduli.huu ndio wadhifa wake mpya.

Yeye mwenyewe alichukua mashamba makubwa ya watu, je ni jinsi gani atasuruhisha migogoro hiyo, huyo mzee hana jipya tofauti na kusifiwa na wanaonufaika naye kwa kupewa vijisenti-wamemfanya ng'ombe wa maziwa.
 
Acheni kejeli za viroba. Jamaa yuko sahihi, hadi sasa baada ya uchaguzi amani imetawala tofauti na enzi za kina muhogo mchungu. Lowassa anastahili heshima, na ukweli ni kuwa hapana wa kulingana naye.
 
Mawazo yako yafaa yaheshimike na kutumiwa kwa uangalifu mkubwa.
Usuluhishi sio kazi ya kuomba bali ya kuombwa na katika usuluhishi mvuto wa mwenza hauna nafasi bali kukubalika kwake na heshima yake kwa jamii inaweza kuwa na mchango japo kidogo.
Umejaribu kumwelezea Lowassa kwa kadiri ya unavyomjua na unavyomchukulia lakini kwa Mama Lowassa(Regina),umemtaja kwa namna unavyofikiri juu yake.
Hapo sio sahihi kumfikiria mtu katika utendaji bali kufahamu katika hilo.
 
Hiyo ndio ilikuwa kazi yenu kumjazia misifa ya uongo mumlie pesa zake. Kwanza Mwache apumzike atafakari pesa alizopoteza.
 
Nimefungua uzi huu nikidhani kuna kuna taarifa kumbe ni upuuzi mtu. EL anachokiweza ni kupiga dili na ufisadi tu. Hafai hata kushauri wanandoa.
 
Sina lengo la kutafuta umaarufu kwa kumzungumzia mtu ambaye kwa sasa anaonekana kuwa maarufu zaidi nchini Tanzania. Ana mvuto wa pekee na kajijengea heshima kubwa katika jamii. Anakubalika kila eneo. Bara na Visiwani; Wakristo na Waislamu, Wenye kumcha Mungu na Wapagani; Wazee na Vijana; Wanaume na Wanawake wote wanamkubali.

Hauhitaji kuwa msomi sana, wala tajiri sana ili kupata umaarufu kama alionao Ndg. Edward Nyoyai Lowassa. Naweza kusema bila ya wivu wala donge kuwa Mungu mwenyewe ndiye alimjalia Ndg Lowassa karama hii. Amefanya siasa kwa miaka mingi na tumeona mazuri na mapungufu yake na hivi karibuni alijikita katika kinyang'anyiro cha nafasi ya Urais lakini yaliyotokea sina haja wala sababu ya kuyajadili hapa lakini JIBU kila mmoja wetu analo kwa namna tulivyopokea matokeo.

Kinachonisukuma kuandika waraka huu; ni kuikumbusha jamii na Ndg. Lowassa kuwa Mungu ametujalia kumpata mtu ambaye anaweza kutumika vizuri katika kuleta mtangamano wa Kitaifa. Kwa karama yake ya kukubalika, binafsi, naona ni mtu sahihi wa kufanya usuluhishi yaani MEDIATION. Mwl. J.K. Nyerere alijaliwa kipawa hiki na alitumika kufanya usuluhishi wa ndani na nje ya nchi. Amefariki akiwa ni mpatanishi wa mgogoro wa Burundi. Ninaiona karama hiyo kwa Lowassa. Kwangu mimi hii ni hazina kubwa ambayo hatuna budi kuitumia kwa manufaa ya taifa letu.

Ninatambua wale ambao wanawaza siasa katika kila jambo wanaweza kuja na kejeli nyingi juu ya hiki, lakini ningependa mnipe mbadala wa Lowassa katika kukubalika katika jamii. Je, ni Pinda, Ben, Mzee Ruksa, JK, Salim, Mzee Wassira, au Warioba??? Kwangu mimi, Lowassa ndiye mtu pekee kwa sasa ambaye anaweza kuwaambia watu wenye jazba, tulieni na wakatulia, wenye silaha mikononi kuwa wekeni chini na watu wakaheshimu; anaweza kuwaambia wanaopigana tulieni na watu wakatii.

Baada ya maisha ya siasa, sasa ni wakati muafaka sana kwa Mzee Lowassa ukawatumikia Watanzania kwa njia hii ambayo kwangu mimi naona ina thawabu kubwa sana mbele za Mungu. Tuna migogoro ya muda mrefu hapa nchini mf. Wakulima na Wafugaji, Wachimbaji wa madini na Wawekezaji, misuguano ya kidini ya chini kwa chini nk. Migogoro hii kwa upande mwingine haihitaji mabavu au mkono wa Serikali bali watu wenye busara zao kama Ndg. Lowassa. Kama hili halitoshi, familia ya Lowassa imebahatika kuwa na Mama mwenye mvuto na ushawishi kuliko wanawake pengine wote kwa sasa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anajiheshimu, ana busara na anakubalika mno mno. Hii ni nyongeza kwa Mzee Lowassa katika kukamilisha kazi ambayo naiona imebaki katika kipindi cha maisha yake. Neno la Mungu linasema Heri Wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu!!

Mwenyezi Mungu akupe jicho la pekee Mzee Lowassa ili uweze kutumika kwa namna mpya na yenye manufaa makubwa kwa Taifa, Bara la Afrika na Dunia kwa ujumla. Mungu akuzidishie maisha marefu na wote wenye kuwaza na kupanga mabaya dhidi yako washindwe.
MAISHA MAPYA NDIYO HAYA MZEE LOWASSA, TUTUMIKIE KWA NAMNA HII.

Maneno mengi umeongea ila acha kujipendekeza ili umtapeli kama walivyo fanya ukawa
 
Sina lengo la kutafuta umaarufu kwa kumzungumzia mtu ambaye kwa sasa anaonekana kuwa maarufu zaidi nchini Tanzania. Ana mvuto wa pekee na kajijengea heshima kubwa katika jamii. Anakubalika kila eneo. Bara na Visiwani; Wakristo na Waislamu, Wenye kumcha Mungu na Wapagani; Wazee na Vijana; Wanaume na Wanawake wote wanamkubali.

Hauhitaji kuwa msomi sana, wala tajiri sana ili kupata umaarufu kama alionao Ndg. Edward Nyoyai Lowassa. Naweza kusema bila ya wivu wala donge kuwa Mungu mwenyewe ndiye alimjalia Ndg Lowassa karama hii. Amefanya siasa kwa miaka mingi na tumeona mazuri na mapungufu yake na hivi karibuni alijikita katika kinyang'anyiro cha nafasi ya Urais lakini yaliyotokea sina haja wala sababu ya kuyajadili hapa lakini JIBU kila mmoja wetu analo kwa namna tulivyopokea matokeo.

Kinachonisukuma kuandika waraka huu; ni kuikumbusha jamii na Ndg. Lowassa kuwa Mungu ametujalia kumpata mtu ambaye anaweza kutumika vizuri katika kuleta mtangamano wa Kitaifa. Kwa karama yake ya kukubalika, binafsi, naona ni mtu sahihi wa kufanya usuluhishi yaani MEDIATION. Mwl. J.K. Nyerere alijaliwa kipawa hiki na alitumika kufanya usuluhishi wa ndani na nje ya nchi. Amefariki akiwa ni mpatanishi wa mgogoro wa Burundi. Ninaiona karama hiyo kwa Lowassa. Kwangu mimi hii ni hazina kubwa ambayo hatuna budi kuitumia kwa manufaa ya taifa letu.

Ninatambua wale ambao wanawaza siasa katika kila jambo wanaweza kuja na kejeli nyingi juu ya hiki, lakini ningependa mnipe mbadala wa Lowassa katika kukubalika katika jamii. Je, ni Pinda, Ben, Mzee Ruksa, JK, Salim, Mzee Wassira, au Warioba??? Kwangu mimi, Lowassa ndiye mtu pekee kwa sasa ambaye anaweza kuwaambia watu wenye jazba, tulieni na wakatulia, wenye silaha mikononi kuwa wekeni chini na watu wakaheshimu; anaweza kuwaambia wanaopigana tulieni na watu wakatii.

Baada ya maisha ya siasa, sasa ni wakati muafaka sana kwa Mzee Lowassa ukawatumikia Watanzania kwa njia hii ambayo kwangu mimi naona ina thawabu kubwa sana mbele za Mungu. Tuna migogoro ya muda mrefu hapa nchini mf. Wakulima na Wafugaji, Wachimbaji wa madini na Wawekezaji, misuguano ya kidini ya chini kwa chini nk. Migogoro hii kwa upande mwingine haihitaji mabavu au mkono wa Serikali bali watu wenye busara zao kama Ndg. Lowassa. Kama hili halitoshi, familia ya Lowassa imebahatika kuwa na Mama mwenye mvuto na ushawishi kuliko wanawake pengine wote kwa sasa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anajiheshimu, ana busara na anakubalika mno mno. Hii ni nyongeza kwa Mzee Lowassa katika kukamilisha kazi ambayo naiona imebaki katika kipindi cha maisha yake. Neno la Mungu linasema Heri Wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu!!

Mwenyezi Mungu akupe jicho la pekee Mzee Lowassa ili uweze kutumika kwa namna mpya na yenye manufaa makubwa kwa Taifa, Bara la Afrika na Dunia kwa ujumla. Mungu akuzidishie maisha marefu na wote wenye kuwaza na kupanga mabaya dhidi yako washindwe.
MAISHA MAPYA NDIYO HAYA MZEE LOWASSA, TUTUMIKIE KWA NAMNA HII.

mkuu usiwe mnafiki alipokuwa ccm kipaji hiki hamkukiona na kwanini uje kujadili sifa hizi kipindi hiki
 
Mtazamo upo sahihi mtoa post,
ni ukweli usiopingika kuwa lowasa ana karama ya pekee
na akitumika kama msuluhishi ktk mambo yanayoisibu jamii
ita kuwa ni jambo lenye heri hata mbele za mungu.
 
Back
Top Bottom