Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Waandaaji wa filamu nyingi za bongo mnaboa sana, hivi hamjajua tu kuwa hadithi za filamu zenu nyingi hazivutii? Unaweza kuwa na kipaji cha kuigiza, halafu usiwe mtunzi mzuri. Kila mtu mungu kampa kipaji chake. Hadithi ndio msingi wa filamu bomba, nchi inao watunzi waziri wa hadithi waliobobea. Mfano Erick Shigongo, Beka Mfaume, Hussein Tuwa, Juma Kidogo, Sultan Tamba na wengineo. Mkiwatumia hawa, mnaweza kujikuta mnatengeneza filamu zenye viwango na ubora wa hali ya juu.