Wadau mnazimalizaje Weekend zenu kistaarabu?

Wadau mnazimalizaje Weekend zenu kistaarabu?

Habari za jioni wana-JF,

Nimeona nije hapa jukwaani kuandika haya machache, huenda kuna wanaopitia hali kama yangu au waliowahi kuivuka wakashare nami namna ya kukabiliana nayo.

Mimi ni mtu ninayependa sana kuwa busy na majukumu yangu. Kipindi cha nyuma, nilikuwa na vitu vingi vilivyonipa burudani na kunichangamsha; nilikuwa mpenzi mkubwa wa kusikiliza Music [emoji444], kuangalia filamu, na hata kutoka mara moja moja. Upande wa pombe nilishaamua kuacha kabisa huko nyuma.

Hata hivyo, siku hizi mambo yamebadilika kabisa. Kila Ijumaa inapoingia , kwangu inakuwa ni mwanzo wa stress na boredom ya hali ya juu.

Yale mambo yote yaliyokuwa yananipa furaha mwanzo (muziki, muvi, mitoko) sasa hivi vimepoteza ladha kabisa, nikijaribu kuvifanya nahisi upweke na muda hauendi.

Hata upande wa mahusiano umekuwa na changamoto sana, kwani imekuwa ngumu kukutana na watu wenye uelewa na ukomavu wa akili unaoenda sawa na mimi.

Kimbilio langu pekee limebaki kwenye kazi. Hamu yangu kubwa kila weekend inakuwa ni kutamani Jumatatu ifike haraka ili nirudi kwenye majukumu yangu ya kila siku, kwa sababu huko ndiko akili yangu inapotulia.
ni muhimu sana kumaliza weekend kwa kua bize kwenye nyumba za ibada au mahali pako pa siri kumshukuru Mungu kwa namna alivyokupigania wiki nzima iliyoisha, na kumuomba baraka na neema zake tena katika kazi na majukumu ya wiki inayokuja.

nadhani huu ndio unapaswa kua ustaarabu muhimu zaidi wa kumaliza weekend, na Mwenyezi Mungu awabariki sana wadau wa JF wote 🐒
 
Hiyo ilikuwa option 1. Option 2. Ila hii make sure miguu yako isikusaliti. Nenda mpaka kituo chochote cha polisi useme i want mafwele here or else nachoma kituo afu utoke mbio kimbia pita kwako uende uendee yan u imagne kwamba unafukuzwa hata kama hawakufukuz kweli wewe nenda tu kilomita nyingi then rudi pole pole uoge ulale cku imeisha na jpil utafute mahindi makavu na maharage uchemshe had saa sita mchana au saa nane. After hapo yaunge fresh ule. Si hapo masaa yatakua yamesogea. Saa kumi shka simu yako ulete mrejesho tukoment tena. Sema fire!!¿
 
ni muhimu sana kumaliza weekend kwa kua bize kwenye nyumba za ibada au mahali pako pa siri kumshukuru Mungu kwa namna alivyokupigania wiki nzima iliyoisha, na kumuomba baraka na neema zake tena katika kazi na majukumu ya wiki inayokuja.

nadhani huu ndio unapaswa kua ustaarabu muhimu zaidi wa kumaliza weekend, na Mwenyezi Mungu awabariki sana wadau wa JF wote 🐒
Nyumba za ibada huko mnafata nini????

Ova
 
1) Fanya biashara - weekend zote zitayeyuka
2) Tafuta mke
Hapo kwenye kutaguta mke/mwenza ndipo anasema hakutani na mtu mwenye levels za kiakili kama yeye. Hapo kwenye biashara ninkweli aisee ukijiajiri hauna wikiend
 
Habari za jioni wana-JF,

Nimeona nije hapa jukwaani kuandika haya machache, huenda kuna wanaopitia hali kama yangu au waliowahi kuivuka wakashare nami namna ya kukabiliana nayo.

Mimi ni mtu ninayependa sana kuwa busy na majukumu yangu. Kipindi cha nyuma, nilikuwa na vitu vingi vilivyonipa burudani na kunichangamsha; nilikuwa mpenzi mkubwa wa kusikiliza Music [emoji444], kuangalia filamu, na hata kutoka mara moja moja. Upande wa pombe nilishaamua kuacha kabisa huko nyuma.

Hata hivyo, siku hizi mambo yamebadilika kabisa. Kila Ijumaa inapoingia , kwangu inakuwa ni mwanzo wa stress na boredom ya hali ya juu.

Yale mambo yote yaliyokuwa yananipa furaha mwanzo (muziki, muvi, mitoko) sasa hivi vimepoteza ladha kabisa, nikijaribu kuvifanya nahisi upweke na muda hauendi.

Hata upande wa mahusiano umekuwa na changamoto sana, kwani imekuwa ngumu kukutana na watu wenye uelewa na ukomavu wa akili unaoenda sawa na mimi.

Kimbilio langu pekee limebaki kwenye kazi. Hamu yangu kubwa kila weekend inakuwa ni kutamani Jumatatu ifike haraka ili nirudi kwenye majukumu yangu ya kila siku, kwa sababu huko ndiko akili yangu inapotulia.
Ingia viwanja mzee mwenzangu. Sio lazima unywe pombe. Suala la mahusiano kumpata mwanamke great thinker kwa Tanzania hii ni ngumu sana sana sana. Inabidi uvumilie level zao za uelewa hawa hawa tulionao mtaani
 
Nikikosa hela ya pombe weekend huwa nashinda geto nahesabu matundu ya net yako mangapi,mpaka kumaliza kuhesabu tayari weekend ishaisha
 
Wewe mtu weekend yako iliishaje. Yani kusema kweli j3 ilivyo ngumu hivi mtu anasema yaye anafurahia ifike arudi kazini mda mwingne nabaki na hali ya @¿!.€!1 yaan mshangawaoo,!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom